Kwanini Prof. Kabudi amerudia hiyo kauli yake?

Kwanini Prof. Kabudi amerudia hiyo kauli yake?

Hii nchi inatakiwa isilinde uhuru wake kisa misaada? Utu wetu upotee kisa misaada?
Sio tutofautishe utu na kutumia akili/busara?.

Kwamba utu utapatikana kati ya Mswahili kwa Mswahili pekee?, kwani hakuna utu kati ya Mzungu na mswahili ?.

Sio kwamba sisi ndio tunakosa utu kwa kupokea pesa za Walipa kodi wa nchi nyingine bila kutekeleza kusudio la pesa hizo?.
 
Nilikuwa nafuatilia sana bunge lililopita na nikasikia kabudi amesema kwamba hakuna vita tulivyo shindwa katika historia alitaja nchi kadhaa ambao JWTZ wamewahi kufanya operation.

Katika diplomasia ya mataifa mbalimbali neno linalohusisha matukio ya jeshi humaanisha kwamba serikali iliyopo madarakani haitaki kukubaliana na sera za kimataifa hasa za magharibi.

Tujikumbushe kuhusu Baba wa Taifa alipokuwa kwenye mvutano na IMF na WB mwalimu akitengeneza vichwa vya wanasiasa ambao hata wangelinda sera za ujamaa wa taifa.

Sasa Kabudi anajaribu sana kutumia nguvu za kijeshi katika diplomasia siasa ambazo zimepitwa na wakati. Hii tuliizoea kwa nchi kama Iran na Korea sasa awamu hii inatokea hapa Bongo Mzee Makamba alitabiri kwamba watu watabatizwa kwa ubatizo wa 🔥 moto.
🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
Tatizo ni kwamba umechukua neno moja na umelitohoa ili kupata ajenda ambayo ndio umeifanyia kuwa ni hoja.

Aliposema kuhusu kutumia jeshi au kushinda vita alikuwa akiwahamashisha waandishi wa habari kuwa tayari kwa vita ya propaganda na kuisaidia serikali katia kujibu hoja za kijinga kama hiyo ya hao wahuni wachache wa EU.

Inajulikana mmoja wa hao wahuni wachache ni wa chama cha CDU ambacho kinaifadhili Chadema.

Na ndo akatoa mifano Tanzania iliposhiriki katika vita ya harakati ya ukombozi kusini mwa Afrika.
 
Wanaotraining Majeshi yetu ndo wanatolewa kauli za kishujaa as if tunajiweza.
Sijui hata kama ss tunamiliki Nyambizi kama hatumili hii jeuri inatoka wapi
 
Nilikuwa nafuatilia sana bunge lililopita na nikasikia kabudi amesema kwamba hakuna vita tulivyo shindwa katika historia alitaja nchi kadhaa ambao JWTZ wamewahi kufanya operation.

Katika diplomasia ya mataifa mbalimbali neno linalohusisha matukio ya jeshi humaanisha kwamba serikali iliyopo madarakani haitaki kukubaliana na sera za kimataifa hasa za magharibi.

Tujikumbushe kuhusu Baba wa Taifa alipokuwa kwenye mvutano na IMF na WB mwalimu akitengeneza vichwa vya wanasiasa ambao hata wangelinda sera za ujamaa wa taifa.

Sasa Kabudi anajaribu sana kutumia nguvu za kijeshi katika diplomasia siasa ambazo zimepitwa na wakati. Hii tuliizoea kwa nchi kama Iran na Korea sasa awamu hii inatokea hapa Bongo Mzee Makamba alitabiri kwamba watu watabatizwa kwa ubatizo wa 🔥 moto.
🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
Anachokitafuta huyu mtu na Baba yake anayemtuma kusema hayo muda si mrefu kitapata dawa yake maana siku si nyingi dawa itaiva
 
Wameyataka maneno wenyewe wacha wajibiwe kwa maneno. Hakuna kukaa kimya

Wazungu wanajidai wanajua kutusema na kutusuta...... hivi wanatuona tumetulia hawatujui eee
Kauli moja tuu ya prof mnakanyagana😁😁😁

Watanzania pekee ndio watu wanaweza kukusema kwa maneno tuu hadi ufe. Kama hawaamini wakawaulize Aston villa yaliyowapata enzi za Samata au wamuulize yule mkandarasi aliyezimiaga kule Dodoma

Sisi ndio wabongo bhana

Nimecheka kwa nguvu.
 
Pumbavu na mpuuzi mkubwa. Hukumsikia aliposema tutashirikiana na mataifa yanayo heshimu utu wetu na taifa letu kama dola huru?
Hela kwanza,majibu ya hela mbona hayatolewi? Mnapuyanga tu.
Huru wa kutaperi pesa za wahisani?
Mmeibia watanzania mkaona mtaperi pesa za wahisani.

Watanzania mmewalaza usingizi kwa madawa ya kichawi.

Huko kwa mabeberu mmekanyaga umeme wa grid ya taifa
 
Kabudi kwanza umeshinda uchaguzi ki ujanja ujanja...hujachaguliwa na wananchi ila Tume ndiyo imekuchagua.. sasa leo hii unapata wapi nguvu ya kuiongelea Tanzania yetu?
 
Wameyataka maneno wenyewe wacha wajibiwe kwa maneno. Hakuna kukaa kimya

Wazungu wanajidai wanajua kutusema na kutusuta...... hivi wanatuona tumetulia hawatujui eee
Kauli moja tuu ya prof mnakanyagana😁😁😁

Watanzania pekee ndio watu wanaweza kukusema kwa maneno tuu hadi ufe. Kama hawaamini wakawaulize Aston villa yaliyowapata enzi za Samata au wamuulize yule mkandarasi aliyezimiaga kule Dodoma

Sisi ndio wabongo bhana
Kama mmekula pesa yao bila utaratibu wasiwasute? Mtafune tu pesa za walipa kodi wao halafu wanyamaze! Hata kama mna mapenzi na mchwa wenu mkuu, jaribuni kutumia akili. Kilangila.
 
Kama mmekula pesa yao bila utaratibu wasiwasute? Mtafune tu pesa za walipa kodi wao halafu wanyamaze! Hata kama mna mapenzi na mchwa wenu mkuu, jaribuni kutumia akili. Kilangila.
Wapi pesa zimeliwa bila utaratibu? Unaweza kuthibitisha hilo ki mahesabu au ndio na wewe unataka kusutwa?
Utasutwa uzimie..... shauri yako
😂😂😂😂😂😂
 
Hii nchi inatakiwa isilinde uhuru wake kisa misaada? Utu wetu upotee kisa misaada?
Uhuru wa nchi lazima ulindwe kwa gharama yoyote.
Hata hivyo, ni muhimu kutofautisha nchi na serikali. Hilo ni tatizo kwa walio wengi.
Mtanzania yeyote awe wa CCM au chama kingine chochote, ana wajibu wa kuitetea Tanzania kwa gharama yoyote hata kama ni uhai wake.
Vyama lazima vikosoane kwa maslahi ya nchi/taifa na siyo maslahi ya serikali.
 
Nilikuwa nafuatilia sana bunge lililopita na nikasikia kabudi amesema kwamba hakuna vita tulivyo shindwa katika historia alitaja nchi kadhaa ambao JWTZ wamewahi kufanya operation.

Katika diplomasia ya mataifa mbalimbali neno linalohusisha matukio ya jeshi humaanisha kwamba serikali iliyopo madarakani haitaki kukubaliana na sera za kimataifa hasa za magharibi.

Tujikumbushe kuhusu Baba wa Taifa alipokuwa kwenye mvutano na IMF na WB mwalimu akitengeneza vichwa vya wanasiasa ambao hata wangelinda sera za ujamaa wa taifa.

Sasa Kabudi anajaribu sana kutumia nguvu za kijeshi katika diplomasia siasa ambazo zimepitwa na wakati. Hii tuliizoea kwa nchi kama Iran na Korea sasa awamu hii inatokea hapa Bongo Mzee Makamba alitabiri kwamba watu watabatizwa kwa ubatizo wa 🔥 moto.
🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
Yaani anasumbuliwa kichwa na empty head tabulalasa ,profesa uchwara , profesa feki , profesa wa sheria ambaye hakufanya mitihani ya uwakili ? Wala hajui inafananaje ?.
 
Kabudi anatukumbusha kuwa huu sio muda wa kutoa nafasi kwa makanjanja wa Eu
 
Wapi pesa zimeliwa bila utaratibu? Unaweza kuthibitisha hilo ki mahesabu au ndio na wewe unataka kusutwa?
Utasutwa uzimie..... shauri yako
😂😂😂😂😂😂
Euro Mil 27 zilizotolewa na umoja wa ulaya ziko wapi? Kwanini tulimpokea pesa wakati tuliitangazia dunia kuwa kwetu hakuna Corona? Ingia kwenye taarifa za bunge la ulaya upate mahesabu. Usikimbilie kunisuta wakati taarifa hizo ziko wazi kwa yeyete kuzisoma. Tatizo la Kabudi badala ya kujibu hoja anakimbilia mipasho kama wewe.
 
Euro Mil 27 zilizotolewa na umoja wa ulaya ziko wapi? Kwanini tulimpokea pesa wakati tuliitangazia dunia kuwa kwetu hakuna Corona? Ingia kwenye taarifa za bunge la ulaya upate mahesabu. Usikimbilie kunisuta wakati taarifa hizo ziko wazi kwa yeyete kuzisoma. Tatizo la Kabudi badala ya kujibu hoja anakimbilia mipasho kama wewe.
Tuliposema Tanzania hakuna corona wala lockdown hamkuwatafsiria???
Mtasutwa tuu hamna namna
 
Back
Top Bottom