Kwanini Posta wamejaa wazee na ukiritimba mwingi?

Mbona mabasi kote nchini yanatoa huduma hiyo, sasa iweje wewe ubaki na hiyo posta?
 
Mkuu sababu ni mbili tu! Hatujalifanyia shirika watalaamu wanasema bpr yaani business processes re-engineering kitu ambacho kingesababisha tuwekeze kwenye teknolojia pamoja na rasilimali watu. Pili tumeng'ang'ania "business as usual" bila kuamka usingizini tukajilinganisha na wenzetu hata kufanya "benchmarking"! Hivi hatuwezi kweli kuangalia tu DHL wanafanyeje kazi ya ufanisi namna Ile?
 
hao wazee wanaacha kukaa home wauguze visukari vyao..wanang'ang'ania kukaa maofisini
 
Posta, nikadhani unauliza maeneo ya posta kwanini yamejaa mazee!
Tatizo la wazee wengi wanaona dharau, kutumwa na watu wa umri wa chini. Kwa iyo mashirika mengi ya serikali yana wazeee wengi ambao tayari wana umri Mkubwa na hawataki kutumwa na kupewa maelezo
 
Umri wa kustaafu ni miaka 60. Hata wao walikuwa vijana kama wewe. Utazeeka na waliopo primary leo watakwambia wewe Mzee. Uzee ni process. Rais wa Tanzania ana miaka zaidi ya 60.
Unawaona wamechoka kwa sababu ys kubeba mixigo
 
Kuna kipindi hua natamani wazee wote wastaafu kutoka serikalini waachiwe vijana wanaoweza kwenda na kasi ya dunia. Wazee wengi wako slow sana, na waka ka mentality flani ka utumishi wa umma wa miaka ya 80
Utazeeka pia. Mbona wazazi wetu wamezeeka pia nao waondolewe kazini kabla ya wakati?
 
Vijana tena?
 
Kote tu katika ofisi za serikali wazee ni shida and slow. Kuna mmoja pale TRA Iringa, tena frontdesk, ni kazi.
Walivyokuwa vijana walichapa kazi sana. Msingeyakuta haya mashirika.
Hata wazazi wetu umri umeenda na kasi ya utendaji imepungua. Mzaxi wako nyumbani hasinzii sebuleni? Nijibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…