STEIN
JF-Expert Member
- Aug 29, 2010
- 1,770
- 553
Ndugu Zangu wanaJF, wapenda mabadiliko, Wasomi, waliochoka na Uongozi mbovu wa CCM toka Uhuru wa nchi hii miaka 49 iliyopita, naomba niwasilishe kisehemu tu ya utafiti mdogo nilioufanya baada ya matokeo ya uchaguzi.
Kwanza nianze na jamii ya waTZ waliokiunga mkono chadema wakati wa kampeni hadi siku ya kupiga kura ni wa aina kuu tano.
Aina ya kwanza ni vijana ambao waliahidiwa na CCM toka mwaka 2005 kuwa wangeishi maisha Bora ambayo waliamini mara tu baada ya JK kushinda angeweza kuwasaidia wakapata kazi nzuru yenye ujira mzuri, lakini wamekuwa mashahidi wakati huu wa kampeni wakiwa wamechoka na maisha kuzidi kuwa magumu na hata kazi zimekuwa ngumu kupatikana mtaani kwahiyo wakapoteza imani na CCM pamoja na JK wake na kuanza kazi ya kuipigia CDM debbe hata bila malipo yeyote.
Pili ni Vijana ambao ni wasomi wa nchi hii kwa ngazi ya Form Six, Diploma, Degree, Masters, PHD ambao kila moja ana sababu zake za kutoikubali CCM na uongozi wake kwa mfano Form six ana matatizo ya ajira na maisha kuwa magumu, Wengine wamesoma lakini kazi hakuna na sehemu nyingi wanakosa nafasi ya kufanya kazi kutokana na Wageni wengi kuchukua nafasi zao huku waTZ wakihaha huku nakule huku bodi ya mikopo ikiwavutia punzi warudishi mikopo waliyopewa. Kwa hiyo utaona ni vigumu kuwabadilisha watu hawa na kuanza kuishabikia CCM mwaka 2015. Kwa upande wa vijana wenye masters na PhD kwa kweli hawa huwa si watu wa kubadilika maana wanafahamu jinsi hali yao kimaisha ilivyo mbaya kwani mshahara wanayopewa ni midogo mno hata haitoshi.
Tatu ni Wafanyakazi ambao kimsingi ndo wanaifanya CDM ing'ae kutokana na sera zake nzuri na CCM kuonyesha kutowajali ambao wanaamini kwamba hata mabadiliko yeyote yatakayofanywa na CCM kwenye maslahi yao ni kutokana na shinikizo kutoka vyama vyao kama TUCTA, CWT etc na si serikali ya CCM. Na hawa ndio wanatumikia taifa hili na ndo wanakatwa kodi kubwa na kupewa mshahara mdogo. Hawa kimsingi si watu wa kuwahonga kirahisi maana kila utakacho wapa watasema ni haki yao.
Kundi la nne ni wazee ambao wameasi kutoka CCM kwa manyanyaso mbali mbali kama wale wa EAC wanaohangaika siku zote mpaka sasa, kundi hili ni dogo lakini si lakudharau maana ina watoto na wajukuu. hawa kuwabadilisha ni kazi ngumu.
Kundi la mwishi ni watoto wa shule za msingi ambao ni taifa la 2015, hawa waelewa na wanafuatilia sana mambo yanayoendelea kwenye siasa za nchi hii, wanapenda sana wata wanaoshughulikia mafisadi ambao ni Wapinzani wa kweli. Kundi hili kulibadilisha mawazo ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa maana huamini kwa asilimia mia moja wanacho ambiwa na wakubwa zao.
Kwa ujumla ilikuwabadilisha watu hawa mawazo kabla ya 2015 itabidi CCM wafanye yale ambayo CDM na mgombea wake wa Uras wameyahubiri wakati wa kampeni. Kwa kweli waTZ wameielewa CDM na sera yake ya Elimu Bure, Afya Bure, Makazi Bora na kushughulikia mafisadi. Kwa sasa waTZ wanaamini yote haya yanawezekana.
Ukitaka kuhakikisha angalia Coments za watu kwa Zito kupitia mitandao mbali mbali na magazeti.
Kwa watu wengi wa mjini wanafikiri ni kama CCM watafanikiwa kama ilivyo kwa NCCR na CUF, ukweli ni kwamba hizi propaganda za magazetini yanaishia Mjini hapa.
Walioko mikoani ni mashahidi wataendelea kutupa data za kutosha.
Naomba kuwasilisha.
Kwanza nianze na jamii ya waTZ waliokiunga mkono chadema wakati wa kampeni hadi siku ya kupiga kura ni wa aina kuu tano.
Aina ya kwanza ni vijana ambao waliahidiwa na CCM toka mwaka 2005 kuwa wangeishi maisha Bora ambayo waliamini mara tu baada ya JK kushinda angeweza kuwasaidia wakapata kazi nzuru yenye ujira mzuri, lakini wamekuwa mashahidi wakati huu wa kampeni wakiwa wamechoka na maisha kuzidi kuwa magumu na hata kazi zimekuwa ngumu kupatikana mtaani kwahiyo wakapoteza imani na CCM pamoja na JK wake na kuanza kazi ya kuipigia CDM debbe hata bila malipo yeyote.
Pili ni Vijana ambao ni wasomi wa nchi hii kwa ngazi ya Form Six, Diploma, Degree, Masters, PHD ambao kila moja ana sababu zake za kutoikubali CCM na uongozi wake kwa mfano Form six ana matatizo ya ajira na maisha kuwa magumu, Wengine wamesoma lakini kazi hakuna na sehemu nyingi wanakosa nafasi ya kufanya kazi kutokana na Wageni wengi kuchukua nafasi zao huku waTZ wakihaha huku nakule huku bodi ya mikopo ikiwavutia punzi warudishi mikopo waliyopewa. Kwa hiyo utaona ni vigumu kuwabadilisha watu hawa na kuanza kuishabikia CCM mwaka 2015. Kwa upande wa vijana wenye masters na PhD kwa kweli hawa huwa si watu wa kubadilika maana wanafahamu jinsi hali yao kimaisha ilivyo mbaya kwani mshahara wanayopewa ni midogo mno hata haitoshi.
Tatu ni Wafanyakazi ambao kimsingi ndo wanaifanya CDM ing'ae kutokana na sera zake nzuri na CCM kuonyesha kutowajali ambao wanaamini kwamba hata mabadiliko yeyote yatakayofanywa na CCM kwenye maslahi yao ni kutokana na shinikizo kutoka vyama vyao kama TUCTA, CWT etc na si serikali ya CCM. Na hawa ndio wanatumikia taifa hili na ndo wanakatwa kodi kubwa na kupewa mshahara mdogo. Hawa kimsingi si watu wa kuwahonga kirahisi maana kila utakacho wapa watasema ni haki yao.
Kundi la nne ni wazee ambao wameasi kutoka CCM kwa manyanyaso mbali mbali kama wale wa EAC wanaohangaika siku zote mpaka sasa, kundi hili ni dogo lakini si lakudharau maana ina watoto na wajukuu. hawa kuwabadilisha ni kazi ngumu.
Kundi la mwishi ni watoto wa shule za msingi ambao ni taifa la 2015, hawa waelewa na wanafuatilia sana mambo yanayoendelea kwenye siasa za nchi hii, wanapenda sana wata wanaoshughulikia mafisadi ambao ni Wapinzani wa kweli. Kundi hili kulibadilisha mawazo ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa maana huamini kwa asilimia mia moja wanacho ambiwa na wakubwa zao.
Kwa ujumla ilikuwabadilisha watu hawa mawazo kabla ya 2015 itabidi CCM wafanye yale ambayo CDM na mgombea wake wa Uras wameyahubiri wakati wa kampeni. Kwa kweli waTZ wameielewa CDM na sera yake ya Elimu Bure, Afya Bure, Makazi Bora na kushughulikia mafisadi. Kwa sasa waTZ wanaamini yote haya yanawezekana.
Ukitaka kuhakikisha angalia Coments za watu kwa Zito kupitia mitandao mbali mbali na magazeti.
Kwa watu wengi wa mjini wanafikiri ni kama CCM watafanikiwa kama ilivyo kwa NCCR na CUF, ukweli ni kwamba hizi propaganda za magazetini yanaishia Mjini hapa.
Walioko mikoani ni mashahidi wataendelea kutupa data za kutosha.
Naomba kuwasilisha.