GE2025 Kwanini ndoto za Mange za Jeshi la Tanzania kuasi haziwezi kufanikiwa?

GE2025 Kwanini ndoto za Mange za Jeshi la Tanzania kuasi haziwezi kufanikiwa?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Getrude Mollel

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2022
Posts
308
Reaction score
424
Jeshi la Tanzania haliwezi kuasi kwa sababu limejengwa juu ya msingi wa historia, umoja na falsafa ya kitaifa iliyopandikizwa tangu enzi za ukombozi.

Wakati mataifa mengi ya Afrika yalirithi majeshi ya kikoloni yaliyokuwa vyombo vya ukandamizaji, Tanzania ilijenga Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) kutoka wapigania uhuru waliokuwa na dhamira ya kuwatumikia wananchi, si kutafuta madaraka. Hilo ndilo tofauti kuu.

Tanzania haikuwa na jeshi lililoachwa na wakoloni. Badala yake, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha jeshi jipya lililotokana na wananchi wa kawaida waliopigana kwa imani ya kujenga taifa moja. Hivyo, JWTZ liliibuka likiwa na roho ya uzalendo, nidhamu na utii wa kiraia. Hadi leo, linafundishwa falsafa ya “Jeshi ni sehemu ya jamii”, likiwa chombo cha kulinda Katiba, si cha kuchukua madaraka.

Kinyume chake, nchi nyingi zilizoathiriwa na mapinduzi kama Burkina Faso (1983, 2022), Mali (1968, 2020, 2021), Guinea (2021) au Sudan (1989, 2021) zilikuwa na majeshi yaliyogawanyika kikabila, yameingiliwa na siasa au yanayohisi kukosa haki kiuchumi.

Mara nyingi, wanajeshi wameona ni jukumu lao “kuokoa taifa” pale viongozi wanaposhindwa. Lakini Tanzania ilijenga taasisi imara za kiraia, mfumo wa vyama, na uwiano wa kijamii unaozuia jeshi kujiweka juu ya serikali.

Zaidi, JWTZ limekuwa likihusishwa moja kwa moja na umoja wa kitaifa, halina upendeleo wa kikabila wala wa kisiasa. Linashirikiana na wananchi kwenye miradi ya maendeleo, elimu ya uraia, na ulinzi wa amani ndani na nje ya nchi (kama Kongo DRC na Lebanon). Hivyo, wanajeshi wanaona fahari yao katika ulinzi wa taifa, si katika mapinduzi.

Kwa msingi huo wa historia, nidhamu, umoja na falsafa ya utii wa kiraia, mapinduzi ya kijeshi Tanzania ni jambo lisilowezekana kimuundo wala kimaadili.
 
Jeshi la Tanzania haliwezi kuasi kwa sababu limejengwa juu ya msingi wa historia, umoja na falsafa ya kitaifa iliyopandikizwa tangu enzi za ukombozi.

Wakati mataifa mengi ya Afrika yalirithi majeshi ya kikoloni yaliyokuwa vyombo vya ukandamizaji, Tanzania ilijenga Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) kutoka wapigania uhuru waliokuwa na dhamira ya kuwatumikia wananchi, si kutafuta madaraka. Hilo ndilo tofauti kuu.

Tanzania haikuwa na jeshi lililoachwa na wakoloni. Badala yake, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha jeshi jipya lililotokana na wananchi wa kawaida waliopigana kwa imani ya kujenga taifa moja. Hivyo, JWTZ liliibuka likiwa na roho ya uzalendo, nidhamu na utii wa kiraia. Hadi leo, linafundishwa falsafa ya “Jeshi ni sehemu ya jamii”, likiwa chombo cha kulinda Katiba, si cha kuchukua madaraka.

Kinyume chake, nchi nyingi zilizoathiriwa na mapinduzi kama Burkina Faso (1983, 2022), Mali (1968, 2020, 2021), Guinea (2021) au Sudan (1989, 2021) zilikuwa na majeshi yaliyogawanyika kikabila, yameingiliwa na siasa au yanayohisi kukosa haki kiuchumi.

Mara nyingi, wanajeshi wameona ni jukumu lao “kuokoa taifa” pale viongozi wanaposhindwa. Lakini Tanzania ilijenga taasisi imara za kiraia, mfumo wa vyama, na uwiano wa kijamii unaozuia jeshi kujiweka juu ya serikali.

Zaidi, JWTZ limekuwa likihusishwa moja kwa moja na umoja wa kitaifa, halina upendeleo wa kikabila wala wa kisiasa. Linashirikiana na wananchi kwenye miradi ya maendeleo, elimu ya uraia, na ulinzi wa amani ndani na nje ya nchi (kama Kongo DRC na Lebanon). Hivyo, wanajeshi wanaona fahari yao katika ulinzi wa taifa, si katika mapinduzi.

Kwa msingi huo wa historia, nidhamu, umoja na falsafa ya utii wa kiraia, mapinduzi ya kijeshi Tanzania ni jambo lisilowezekana kimuundo wala kimaadili.

Mimi binafsi sikubaliani na wazo la wanajeshi kuchukua uongozi wa nchi.

Si wazo la kidemokrasia, linatengeneza precedent mbaya, linatumia nguvu sehemu ya kutumia akili, linawategea wanajeshi wafanye kazi ya raia wote, halituhakikishii kuwa wanajeshi watafanya vizuri zaidi, na wakifanya vibaya tunaweza kukisa namna ya kuwatoa.

Tumeshindwa kumtoa Samia, imagine akija mwanajeshibkama Sani Abacha, tutawezaje kumtoa?

Kwa hiyo naona ni wazo la desperation, ni wazo la kivivu kuwategemea wanajeshi kufanya kazi ya wote, ni wazo la watu wasiofikiri sana kuhusu precedents and unintended consequences.

Lakini naweza kuchambua kwa nini Tanzania wanajeshi wawawezi kuchukua uongozi wa nchi kwa hali ya sasa.

Watu wanafikiri kuwa wanajeshi wa Tanzania ni watu tofauti sana na Watanzania wengine.

Wanafikiri wanajeshi wa Tanzania ni kama wametoka sayari tofauti au nchi tofauti.

Wanajeshi wa Tanzania ni Watanzania. Wamelelewa katika tamaduni za Ki Tanzania, wana mazuri na mabaya yaleyale ya Watanzania.

Kama Watanzania wana utamaduni wa kushindwa kuondoa uongozi uliopo, wanajeshi nao wanakuwa na tatizo hilohilo.

Tena wanajeshi wa Tanzania watashindwa zaidi ya raia, kwa sababu tangu maasi ya kijeshi ya 1964, jeshi lilivunjwa na kuundwa kisiasa zaidi. Nyerere alisema ile aibu ya 1964 isijirudie tena. Wanajeshi wakawa wanapigwa sana siasa.

Nikiangalia historia, naona kama maasi ya 1964 yalikuwa ni "a blessing in disguise" kwa Nyerere na Watanzania wasiopenda mapinduzi ya kijeshi. Kwa sababu yalikuwa ni "wake up call" iliyomuwezesha Nyerere kulivunja jwshi na kuliunda upya, bila ya kupata madhara ya kupinduliwa.

Ndiyo maana kama ulivyosema nchi nyingi za Africa zimepata matatizo ya mapinduzi ya kijeshi, lakini Tanzania hatukupata.

Kimsingi raia wa Tanzania wana uwezo mkubwa wa kubadilisha uongozi kuliko wanajeshi. Na hata wanajeshi wakichujua uongozi inatakiwa wananchi ndio waanzishe uasi.

Wanajeshi wa Tanzania na wao ni Watanzania tu.

Ndiyo maana unaona Watanzania wasio wanajeshi wanalialia mitandaoni hawawezi kubadadili kitu, wanawaomba wanajeshi wachukue uongozi wa nchi, na wanajeshi nao wanakuja mitandaoni kulialia.

Kwa hivyo hizi kelele za wanajeshi kuchukua nchi ni fantasy football na political masturbation tu.

Kitu hicho hakiwezi kutokea katika miaka ya karibuni kwa level hii ya uongozi.
 
Julius alitaka Jeshi liwe na muonekano wa kisiasa.....


"
Political army under TANU/CCM

The new army was built by recruiting mainly members of the youth union of TANU and was named the Tanzania People's Defense Force (TPDF). [10] This new army was placed under the supervision of the TANU party (later CCM) following the style of countries like Russia and China. The first commander was Mrisho Sarakikya who had stood on the side of the government during the rebellion and was promoted from lieutenant to colonel, later to general. Nyerere wanted an army with a political character. Every soldier was expected to be a TANU cadre"
 
N kwel Tanzania tuna watu wenye uvivu wa kufikiri kama ww

Suala la jeshi kuasi halitokan na shinikizo la mtu ila unatakiwa kujua kuwa wanajeshi nao n watu na Wana tamaa kama ulivyo wewe kwahy suala la kuasi iwapo akitokea captain yeyote akashawishi n dhahiri wataasi labda kama huko jeshini Kuna maroboti na sio watu
Kumbuka tamaa ya mtu huchanua wakat wowote ule
 
N kwel Tanzania tuna watu wenye uvivu wa kufikiri kama ww

Suala la jeshi kuasi halitokan na shinikizo la mtu ila unatakiwa kujua kuwa wanajeshi nao n watu na Wana tamaa kama ulivyo wewe kwahy suala la kuasi iwapo akitokea captain yeyote akashawishi n dhahiri wataasi labda kama huko jeshini Kuna maroboti na sio watu
Kumbuka tamaa ya mtu huchanua wakat wowote ule
 
Jeshi la Tanzania haliwezi kuasi kwa sababu limejengwa juu ya msingi wa historia, umoja na falsafa ya kitaifa iliyopandikizwa tangu enzi za ukombozi.

Wakati mataifa mengi ya Afrika yalirithi majeshi ya kikoloni yaliyokuwa vyombo vya ukandamizaji, Tanzania ilijenga Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) kutoka wapigania uhuru waliokuwa na dhamira ya kuwatumikia wananchi, si kutafuta madaraka. Hilo ndilo tofauti kuu.

Tanzania haikuwa na jeshi lililoachwa na wakoloni. Badala yake, Mwalimu Julius Nyerere alianzisha jeshi jipya lililotokana na wananchi wa kawaida waliopigana kwa imani ya kujenga taifa moja. Hivyo, JWTZ liliibuka likiwa na roho ya uzalendo, nidhamu na utii wa kiraia. Hadi leo, linafundishwa falsafa ya “Jeshi ni sehemu ya jamii”, likiwa chombo cha kulinda Katiba, si cha kuchukua madaraka.

Kinyume chake, nchi nyingi zilizoathiriwa na mapinduzi kama Burkina Faso (1983, 2022), Mali (1968, 2020, 2021), Guinea (2021) au Sudan (1989, 2021) zilikuwa na majeshi yaliyogawanyika kikabila, yameingiliwa na siasa au yanayohisi kukosa haki kiuchumi.

Mara nyingi, wanajeshi wameona ni jukumu lao “kuokoa taifa” pale viongozi wanaposhindwa. Lakini Tanzania ilijenga taasisi imara za kiraia, mfumo wa vyama, na uwiano wa kijamii unaozuia jeshi kujiweka juu ya serikali.

Zaidi, JWTZ limekuwa likihusishwa moja kwa moja na umoja wa kitaifa, halina upendeleo wa kikabila wala wa kisiasa. Linashirikiana na wananchi kwenye miradi ya maendeleo, elimu ya uraia, na ulinzi wa amani ndani na nje ya nchi (kama Kongo DRC na Lebanon). Hivyo, wanajeshi wanaona fahari yao katika ulinzi wa taifa, si katika mapinduzi.

Kwa msingi huo wa historia, nidhamu, umoja na falsafa ya utii wa kiraia, mapinduzi ya kijeshi Tanzania ni jambo lisilowezekana kimuundo wala kimaadili.
Takataka🚮🚮🚮🚮

Sasa kama haliwezi kuasi kwanini unaweweseka? Na wewe unadhani ndo mwamuzi wa utendaji wa jeshi?
 
Mimi binafsi sikubaliani na wazo la wanajeshi kuchukua uongozi wa nchi.

Si wazo la kidemokrasia, linatengeneza precedent mbaya, linatumia nguvu sehemu ya kutumia akili, linawategea wanajeshi wafanye kazi ya raia wote, halituhakikishii kuwa wanajeshi watafanya vizuri zaidi, na wakifanya vibaya tunaweza kukisa namna ya kuwatoa.

Tumeshindwa kumtoa Samia, imagine akija mwanajeshibkama Sani Abacha, tutawezaje kumtoa?

Kwa hiyo naona ni wazo la desperation, ni wazo la kivivu kuwategemea wanajeshi kufanya kazi ya wote, ni wazo la watu wasiofikiri sana kuhusu precedents and unintended consequences.

Lakini naweza kuchambua kwa nini Tanzania wanajeshi wawawezi kuchukua uongozi wa nchi kwa hali ya sasa.

Watu wanafikiri kuwa wanajeshi wa Tanzania ni watu tofauti sana na Watanzania wengine.

Wanafikiri wanajeshi wa Tanzania ni kama wametoka sayari tofauti au nchi tofauti.

Wanajeshi wa Tanzania ni Watanzania. Wamelelewa katika tamaduni za Ki Tanzania, wana mazuri na mabaya yaleyale ya Watanzania.

Kama Watanzania wana utamaduni wa kushindwa kuondoa uongozi uliopo, wanajeshi nao wanakuwa na tatizo hilohilo.

Tena wanajeshi wa Tanzania watashindwa zaidi ya raia, kwa sababu tangu maasi ya kijeshi ya 1964, jeshi lilivunjwa na kuundwa kisiasa zaidi. Nyerere alisema ile aibu ya 1964 isijirudie tena. Wanajeshi wakawa wanapigwa sana siasa.

Nikiangalia historia, naona kama maasi ya 1964 yalikuwa ni "a blessing in disguise" kwa Nyerere na Watanzania wasiopenda mapinduzi ya kijeshi. Kwa sababu yalikuwa ni "wake up call" iliyomuwezesha Nyerere kulivunja jwshi na kuliunda upya, bila ya kupata madhara ya kupinduliwa.

Ndiyo maana kama ulivyosema nchi nyingi za Africa zimepata matatizo ya mapinduzi ya kijeshi, lakini Tanzania hatukupata.

Kimsingi raia wa Tanzania wana uwezo mkubwa wa kubadilisha uongozi kuliko wanajeshi. Na hata wanajeshi wakichujua uongozi inatakiwa wananchi ndio waanzishe uasi.

Wanajeshi wa Tanzania na wao ni Watanzania tu.

Ndiyo maana unaona Watanzania wasio wanajeshi wanalialia mitandaoni hawawezi kubadadili kitu, wanawaomba wanajeshi wachukue uongozi wa nchi, na wanajeshi nao wanakuja mitandaoni kulialia.

Kwa hivyo hizi kelele za wanajeshi kuchukua nchi ni fantasy football na political masturbation tu.

Kitu hicho hakiwezi kutokea katika miaka ya karibuni kwa level hii ya uongozi.
Tunaelewa unaogopa kwa sababu unaishi kwa pesa za ufisadi.

Ila vumilia tu maslahi ya nchi ni muhimu kuliko kuenjoy kwako kwa pesa za ufisadi
 
Mimi binafsi sikibaliani na wazo la wanajwshi kuchukua uongozi wa nchi.

Lakini nawwza kuchambua kwa nini Tanzania wanajeshi wawawezi kichukua uongozi wa nchi kwa hali ya sasa.

Watu wanafikiri kuwa wanajeshi wa Tanzania ni watu tofauti sana na Watanzania wengine.

Wanafikiri wanajeshi wa Tanzania ni kama wametoka sayari tofauti au nchi tofauti.

Wanajeshi wa Tanzania ni Watanzania. Wamelelewa katika tamaduni za Ki Tanzania, wana mazuri na mabaya yaleyale ya Watanzania.

Kama Watanzania wana utamaduni wa kushindwa kuondoa uongozi uliopo, wanajeshi nao wanakuwa na tatizo hilohilo.

Tena wanajeshi wa Tanzania watashindwa zaidi ya raia, kwa sababu tangu ya maasi ya kijeshi ya 1964, jeshi likivunjwa na kuundwa kisiasa zaidi. Nyerere alisema ike aibu ya 1964 isijirudie tena. Wanajwshi wakawa wanapigwa sana siasa.

Kinsingi raia wa Tanzania wana uwwzo mkubwa wa kubadikisha uongozi kuliko wanajeshi.

Ndiyo maana unaona Watanzania wasio wanajeshi wanalialia mitandaoni hawawezi kubdadili kitu, wanawaomba wanajeshi wachukue uongozi wa nchi, na wanajeshi nao wanakuja mitandaoni kulialia.

Kwa hivyo hizi kelele za wanajeshi kuchukua nxhi ni fantasy football nanpolitical masturbation tu.

Kitu hicho hakiwezi kutokea katika miaka ya karibuni kwa level hii ya uongozi.
Taasisi za kiraia zimeoza kwa ufisadi , mahakama, polisi, na vyombo vya uwajibikaji vimekufa, vimeoza. Hakuna wakuwatetea raia.

Hapo hakuna kingine zaidi ya jeshi kufanya transitional military intervention... maana hakuna namna na waliotaka hayo yote ni watawala. Baada ya hapo madaraka yanarejeshwa kwa raia kupitia katiba mpya au uchaguzi huru.

Watu hawataki kusikia, kila anayesema anakamatwa na kutekwa, anauawa , anafichwa pasipojulikana, unataka nini kifanyike?

Kijana anachoma picha anakamatwa na kupotezwa, hivi unaelewa level ya uonevu iliyofikia Tanzania hivi sasa?

Ukimkosoa rais saa 2 asubuhi tiktok au instagram wakajua ulipo basi jua halizami umepotezwa, hii sio US kaka, This is Tanzania.

Wananchi walitaka mabadiliko ya kikatiba kwa amani, lakini imekuwa kama vita... unaposema wananchi wanaweza kufanya hayo mabadiliko kivipi? hali ya kuwa wanatishiwa kwa kauli za vitisho, silaha za kivita na kupewa hofu.

Usiongee vitu ukidhani ni rahisi kama unavyoandika, watu wamechoka, inafikia muda mtu anaona ni bora lolote liwe.

Jeshi ni ngao ya taifa na taifa ni wananchi , ulinzi wa wananchi ni ulinzi wa taifa... acha jeshi liingie kulinda raia.
 
Msimchukulie mange poa, yule mdada ana nguvu kubwa ya kiasili kama mwanamke kushawishi. Wenje anawewesuka na kumdharau kwa wembamba wake, kwani kuwa kibonge na tipwatipwa ndio kuwa na akili? Huyo mdada si wa kumdharau kwa kuwa ni mwembamba
 
Kidampa wa mafisadi upo hoi, hebu angalia mafundi viyoyozi wenu hawa


Samuel Kaaya : Ni kweli nilisema lakini hayapo kwenye maelezo yangu yale ya Polisi.

Mhe. Lissu: Hiyo covering letter umeleta?

Samuel Kaaya : sijaleta kwasababu ni internal communication.

Mhe. Lissu: Kwahiyo haiwahusu Majaji?

Samuel Kaaya : Ni kweli haiwahusu.

Mhe. Lissu: Sasa kama haiwahusu uliisema hapa Mahakamani ili iweje?

Samuel Kaaya : Mimi Sijui.
 
Msimchukulie mange poa, yule mdada ana nguvu kubwa ya kiasili kama mwanamke kushawishi. Wenje anawewesuka na kumdharau kwa wembamba wake, kwani kuwa kibonge na tipwatipwa ndio kuwa na akili? Huyo mdada si wa kumdharau kwa kuwa ni mwembamba
Mange ni kama media tu, anatumika kama msemaji, na wanaompa taarifa ni hao hao waliopo serikalini, hizo risiti, picha, mikataba, taarifa za ufisadi zinatokea huko huko serikalini na wanasalitiana wao kwa wao.

Suala la maandamano ilikuwa si lazima Mange aseme, lakini kila Mtanzania anaelewa mambo hayapo sawa, vyombo vya ulinzi na usalama pia wanaelewa nini kinaendelea.

Kuna watu wana taarifa nyingi sana lakini hawasemi kwa kuhofia usalama wao, suala la kuandamana si matakwa ya Mange.
 
Back
Top Bottom