Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,996
Habari kutoka kijijini,
Kuna mwamko mkubwa ambao haujawahi kutokea na nimeona nami nitoe mchango wangu japo kidogo. Baadaye kesho nitawasilisha mchango wangu huo ili kusaidia japo kiduchu katika kuwapa nafasi Chadema ya kufanikiwa. Kwa vile kampeni hii ina gharama kubwa sana ya kifedha naamini bila michango ya wale wanaounga mkono au kushabikia mabadiliko kujitoa kwa namna moja au nyingine.
Ninatoa changamoto kwa yeyote (hata wasiokuwa wanachama wa Chadema kama mimi) kuchangia chochote walicho nacho. Ninawashukuru wale ambao tangu asubuhi wamepokea wito wangu huo kupitia magazeti makubwa mawili nchini. Jaribu kufikia kiwangu changu hicho au jaribu kunipita. Lakini vile vile haijalishi kiasi chochote ulichonacho changia ili angalau uweze kusema kuwa na mimi nilisaidia kununua machungwa ya kusaidia timu ishinde!
Kuchanga ni kuchagua na kuchagua ni kuchangia!
Mabadiliko hayaji kwa kusubiriwa, kuombewa au kungojewa; mabadiliko yanaletwa!
Sehemu katika makala zangu za leo inatoa maelezo yafuatayo:
Kuna mwamko mkubwa ambao haujawahi kutokea na nimeona nami nitoe mchango wangu japo kidogo. Baadaye kesho nitawasilisha mchango wangu huo ili kusaidia japo kiduchu katika kuwapa nafasi Chadema ya kufanikiwa. Kwa vile kampeni hii ina gharama kubwa sana ya kifedha naamini bila michango ya wale wanaounga mkono au kushabikia mabadiliko kujitoa kwa namna moja au nyingine.
Ninatoa changamoto kwa yeyote (hata wasiokuwa wanachama wa Chadema kama mimi) kuchangia chochote walicho nacho. Ninawashukuru wale ambao tangu asubuhi wamepokea wito wangu huo kupitia magazeti makubwa mawili nchini. Jaribu kufikia kiwangu changu hicho au jaribu kunipita. Lakini vile vile haijalishi kiasi chochote ulichonacho changia ili angalau uweze kusema kuwa na mimi nilisaidia kununua machungwa ya kusaidia timu ishinde!
Kuchanga ni kuchagua na kuchagua ni kuchangia!
Mabadiliko hayaji kwa kusubiriwa, kuombewa au kungojewa; mabadiliko yanaletwa!
Sehemu katika makala zangu za leo inatoa maelezo yafuatayo:
Kwa kuchangia Chadema tuma neno "Chadema" kwenda namba 15710 na utakuwa umechangia shilingi 350 kwa kila sms. Hii ina maana gani? Ina maana leo Jumatano wasomaji wapatao elfu kumi tu wakiamua kutuma sms moja tu kwa siku watakuwa wamechangia shilingi milioni 3.5! Na hao tu wakiamua kuchangia kiasi hicho hicho kwa mfululizo wa siku saba (yaani mara moja kila siku) hadi Jumanne ijayo watakuwa wamechangia shilingi milioni 24! Itakuwaje kama wataamua kuchangia mara mbili au mara tatu? Kwa wale wengina nao wanaweza kuchangia kununua "machungwa" kwa kutumia M-Pesa kwa kutumia namba hizi 0758 22 33 44, 0764 77 66 73 au kwa kutumia Benki akaunti ya Chadema M4C - CRDB 0J1080100600 au MNB ni akaunti 2266600140.
Pendekezo langu kwa wale wanaotaka kuchangia ni kutuma neno hilo kwenda hiyo namba, halafu wawatumie marafiki na jamaa zao kwenye simu jumbe kuwa "nimechangia mabadiliko kwa kuchangia Chadema; nawe changia: Tuma sms yenye neno "Chadema" kwenda 15710 uchangie mabadiliko". Nina uhakika kabisa, Watanzania wanaotaka mabadiliko wataona tofauti mitaani; wataona mabango zaidi ya Dr. Slaa, wabunge na madiwani katika siku chache zijazo. Lakini hilo halitatokea kwa kuombewa au kungojewa.
Lakini wale ambao nao wanaona kuwa Chadema haifai kupewa nafasi ya kuongoza na kuwa CCM inatakiwa iendelee kutawala na wao wana haki ya kukichangia kabisa chama hicho ili kiendelee kututawala. Ni lazima wachangie kwa kufuata dhamira zao wala wasione aibu. Si lazima wote wachangie upinzani kwa kufuata mkumbo! Anayechangia CCM achangie kwa sababu anaamini kwa dhamira yake kuwa kwa kufanya hivyo ni vizuri kwake na kwa watoto wake. Na yule atakayetaka kuchangia Chadema au chama kingine naye afanye hivyo hivyo bila ya kumuomba mtu msamaha au kutoa maelezo kana kwamba anafanya uhalifu.