Kwanini Mwarabu na Mreno huwa hawahesabiki kama wakoloni?

yorkshire

JF-Expert Member
Sep 9, 2016
2,445
2,956
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada bila kupoteza muda.

Nimekuta ugomvi mkubwa tu ambao umetokana na kichwa cha habari hapo juu, upande mmoja ukipinga vikali mwarabu kuitwa mkoloni na upande mwingine ukimuhusisha mwarabu moja kwa moja kama mkoloni namba moja tena ambaye ni mbaya kabisa.

Labda turudi kwenye maana ya ukoloni, vitabu vingi vinasema kwamba ukoloni ni kitendo cha nchi moja yenye nguvu kiuchumi, kisiasa , kijamii na kiutamaduni kuitawala nchi nyingine ambayo ni dhaifu kwenye vipengele hivyo vinne. Sasa basi kutokana na hivyo vingepele ni dhahili mwaarabu na mreno wanaingia moja kwa moja kwenye kuitawala Tanganyika.

Bahati mbaya sana vitabu vingi haviwataji waarabu na wareno kama wakoloni hasa waarabu wanatajwa kama wafanyabiashara ili hali waliitawala Zanzibar na Pwani ya Afrika Mashariki kwa miaka nenda rudi katika nyanja zote nne muhimu.

Upande wa watetezi waarabu wanadai kuwa wao (Waarabu) hawakuwa wakibeba rasimali kuzipeleka kwao uarabuni walizitumia hapa hapa Afrika Mashariki kwa kuanzisha makazi Pwani na Zanzibar kwa ujumla wakati huo huo kundi la pili linapinga vikali kigezo hicho likirudi kwenye maana nzima ya ukoloni nini maana yake hata hivyo kundi hili la pili wameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa waarabu hawaingizwi kwenye kundi la wakoloni kwa sababu ya mapenzi binafsi ya waandishi wa vitabu kuwa wanashabihiana nao kwenye suala la dini (Uislamu) ndio maana waarabu hawaandikwi hivyo tofauati na wazungu ambao ni Wakristo.
 
Waarabu wengi walikimbia kwao kuja kuishi huku, arabuni hakukuwa na chochote that time, ilikuwa ni jangwa tu, hkukuwa na chochote cha maana. walivofika afrika walilowea wakawaleta wenzao wakaanzisha makazi, wakafanya sana business ya kuwauza waafrica amerika na ulaya (hata kwao hawakupeleka as cheap labour)

Waarabu, mpaka leo wao ndo wafanya biashara wazuri, Mfano Dubai inapata hela nyingi kwenye utalii kuliko mafuta, ingawa hamna cha maana cha kutalii.
 
Walitawala kipindi amabcho siyo zama za ukoloni(highest stage of capitalism) kipindi wao wantawala kilikuw ni cha ukabaila(feudalism). Kumbuk kwamba ukoloni ulizaliwa n maendleo ya viwanda.je, kipindi cha waarabu Africa mashriki 1700s kushuka karne ya 7 kulikuwep n maendleo y viwanda? Demand yao waarab n Wareno ilikuwa Biashara y dhahab n utumwa kitu ambch wakolon walikipinga(utumwa) n hii ndio mgogoro mkubwa wa wareno,waarab n wakoloni(abolition of slave trade)
 
jibu ni rahisi sana, ukoloni ni kipindi kama “awamu ya tano” hivyo basi kipindi ambacho mwarabu anatawala kile kipindi kiliitwa “slave trade” na mreno nae katawala kipindi chake
hivyo basi mwarabu na mreno hawaitwi wakoloni kwa sababu hawakutawala wakati wa colonialism
 
Walitawala kipindi amabcho siyo zama za ukoloni(highest stage of capitalism) kipindi wao wantawala kilikuw ni cha ukabaila(feudalism). Kumbuk kwamba ukoloni ulizaliwa n maendleo ya viwanda.je, kipindi cha waarabu Africa mashriki 1700s kushuka karne ya 7 kulikuwep n maendleo y viwanda? Demand yao waarab n Wareno ilikuwa Biashara y dhahab n utumwa kitu ambch wakolon walikipinga(utumwa) n hii ndio mgogoro mkubwa wa wareno,waarab n wakoloni(abolition of slave trade)
Elewa kwanza maana ya neno ukoloni halafu tazama na maelezo yko pia ujiulize waliyoyatenda wazungu katika msingi wa neno ukoloni je matendo yale yale hayakutendwa na waarabu?!! Hpo ndipo utata unapoanzia ya kwamba huyu aitwe mkoloni na huyu asiitwe mkoloni ili hali matendo ya hawa wote yanashabihiana



Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Walitawala kipindi amabcho siyo zama za ukoloni(highest stage of capitalism) kipindi wao wantawala kilikuw ni cha ukabaila(feudalism). Kumbuk kwamba ukoloni ulizaliwa n maendleo ya viwanda.je, kipindi cha waarabu Africa mashriki 1700s kushuka karne ya 7 kulikuwep n maendleo y viwanda? Demand yao waarab n Wareno ilikuwa Biashara y dhahab n utumwa kitu ambch wakolon walikipinga(utumwa) n hii ndio mgogoro mkubwa wa wareno,waarab n wakoloni(abolition of slave trade)
On point. Tatizo una andika kama vile sio msomi. Sorry kwa hiyo criticism. Sorry I am not sorry.
 
Waarabu wengi walikimbia kwao kuja kuishi huku, arabuni hakukuwa na chochote that time, ilikuwa ni jangwa tu, hkukuwa na chochote cha maana. walivofika afrika walilowea wakawaleta wenzao wakaanzisha makazi, wakafanya sana business ya kuwauza waafrica amerika na ulaya (hata kwao hawakupeleka as cheap labour)

Waarabu, mpaka leo wao ndo wafanya biashara wazuri, Mfano Dubai inapata hela nyingi kwenye utalii kuliko mafuta, ingawa hamna cha maana cha kutalii.
Dubai hamna cha maana cha utalii,ushawahi kufika Dubai kaka!?.
Dubai walivyoona mafuta yanaelekea kupungua ,wakaamua kuekeza kwenye utalii,na wameijenga nchi yao ile mbaya.
 
Elewa kwanza maana ya neno ukoloni halafu tazama na maelezo yko pia ujiulize waliyoyatenda wazungu katika msingi wa neno ukoloni je matendo yale yale hayakutendwa na waarabu?!! Hpo ndipo utata unapoanzia ya kwamba huyu aitwe mkoloni na huyu asiitwe mkoloni ili hali matendo ya hawa wote yanashabihiana



Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Ukoloni Haibeb maana ya ubabe moj kwa moja kam wabongo tunvymaanisha, ukolon ni mfum w maisha. Ubabe ni sifa mojwapo tu hat kweny udikteta na ukomunist ipooo
 
Waarabu wengi walikimbia kwao kuja kuishi huku, arabuni hakukuwa na chochote that time, ilikuwa ni jangwa tu, hkukuwa na chochote cha maana. walivofika afrika walilowea wakawaleta wenzao wakaanzisha makazi, wakafanya sana business ya kuwauza waafrica amerika na ulaya (hata kwao hawakupeleka as cheap labour)

Waarabu, mpaka leo wao ndo wafanya biashara wazuri, Mfano Dubai inapata hela nyingi kwenye utalii kuliko mafuta, ingawa hamna cha maana cha kutalii.
Umeandika vizuri sana.Warabu ni wajanja wajanja sana.Wamejichanganya na waafrika kuliko race yoyote ile hapa duniani.warabu tangu waingie Africa hawajainua mguu wao Ila wameweka mizizi, kwa kiasi kikubwa warabu wameishakuwa waafrika ni raia wa Afrika(ukanda wote wa Afrika mashariki na kaskazini wamejaa tele) na wanazitawala baadhi ya nchi za Afrika.Warabu wa Asia huwasaidia mitaji ndugu zao wa huku Afrika, hivyo warabu wa hapa Afrika wameendelea kutawala biashara za kati.

Warabu bado wana ekti kama middle man wa Afrika na Ulaya.

Nilopokuwa sekondari sikupata majibu sahihi kuwa mungu aliumbaje warabu barani Afrika,ilikuwaje.Baadae nikatafuta ukweli na kugundua maingoliano ya Afrika na Asia ni ya maelfu ya miaka sio hivi karibuni hivyo kupata jibu la mwarabu ni mkoloni au sio mkoloni unatakiwa uanzie mbali sana sio karne ya saba tu tunayoambiwa ktk historia.Historian inachanganya sana, so find the truth for yourself, do research you will get the answer vinginevyo fuata upepo.
 
Dubai hamna cha maana cha utalii,ushawahi kufika Dubai kaka!?.
Dubai walivyoona mafuta yanaelekea kupungua ,wakaamua kuekeza kwenye utalii,na wameijenga nchi yao ile mbaya.

Amegandisha akili kuwa utalii ni kuangalia wanyama na kupanda milima
 
Ukoloni ulianza rasmi mwaka 1884/85...
Muda huo waarabu wameisha kaa na wanazengo kwan karne kadha... pia mreno yeye Amefika africa1488(Batholomeo diaz).. ukiangalia nature yao hawa walikuja kwa gia ya biashara sio ya ukoloni moja kwa moja.... mfano mzuri ni kujengwa kwa fort Jesus Mombasa ilikuwa ni kulinda biashara zao...
ukoloni uliposimikwa rasmi1884/85... Hakuna koloni ambalo alipewa moja kwa moja mwarabu atawale. kumbukumbu zangu zinanikumbusha habari ya Zanzibar ambayo ilikuwa chini ya waarabu na ukoloni ulipoanza ikawekwa chini ya mwingereza na pia pwani ya Africa mashariki... kutokana na kukosa koloni mwarabu hesabiwi kama mkoloni...
kwa ishu ya wareno.. wareno kipindi hicho walikuwa watu maskini sanaa ulaya hawakuwa na uwezo wa kuendesha miradi mikubwa katika makoloni yake hii ilisababisha makoloni yake kuwa na bendera ya ureno ila wanaofaidi ni wamarekani... kwa mtazamo wangu hii ni moja ya sababu ya wengi kumsahau.. kama mkoloni
ishu nyingine sisi tumemkalili sanaa mwingereza na mgeruman maan ndo walitutawala ila ungeenda msumbiji uko walikoonja joto la jiwe la mreno.. hii habari yako ingeishia ruvuma pale...
 
Waulize Msumbiji, Angola, Guinea-Bissau nani alikuwa mkoloni wao kama si Mreno.
 
Back
Top Bottom