Kwanini Mungu hakurekebisha kilichosababisha shetani akaasi kabla ya kumuumba binadamu?

Habari ya jumapili.

Dini inasema shetani aliasi huko juu mbunguni mahala palipotukuka na palipoinuka juu anapoishi mungu. Baada ya shetani kuasi mungu akamtimua na kumshusha huku Duniani.

Dini inasema baadae mungu akamuumba mwanadamu na kumuweka Duniani, maana yake mwanadamu alipowekwa duniani tayari shetani alikua duniani muda mrefu tu anakula zake maisha.

Hadithi ya shetani kuasi iko one sided, yaani inaelezwa kutoka upande wa mungu, hakuna aliewahi kusikia upande wa shetani(tayari binadam wanamshutumu shetani kwa habari ya kuambiwa, one sided story, hivyo shetani anahukumiwa kua ni mbaya bila kusikilizwa).

Dini haisemi kwa nini shetani aliasi na ilikuaje akaasi. Dini inasema mungu anajua kila kitu, all knowing lakini haisemi mungu alishindwaje kujua kua shetani atakuja kuasi ili asimuumbe. Na kama alijua shetani atakuja kuasi kwa nini alimuacha aasi. Mbaya zaidi huo mgogoro wao umetuingiza na sisi binadam ambao hatujui chanzo cha mgogoro. Yaani mungu anarecruit binadam washirikiane nae mwenye mgogoro wake na shetani huku binadam hawajui chanzo cha mgogoro wao. Na mungu anatishia kua yoyote ambae hatashirikiana nae kwenye mgogoro huo atampanish vikali. Unajiuliza hakuaje involved kwenye mgogoro nisioujua chanzo chake na natishiwa adhabu kali kama sitashiriki huo mgogoro, hivyo watu waoga na wajinga wanalazimika kushiriki mgogoro blindly ili kuogopa adhabu.

Kama mungu anawapenda wanadamu kama dini inavyosema alipaswa kurekebisha kasoro zilizojitokeza kabla ya kumuumba mwanadam, lakini pia alipaswa kujua in the first hand kua shetani atakuja kuasi kabla hajamuumba, vinginevyo hajui kila kitu kinyume na inavyosemekana kua anajua kila kitu.

Tukubali tukatae, maovu yote duniani kama mauaji, wivu, kifo, husda, wizi, matetemeko ya ardhi, tsunami, vimbunga, ukame, magonjwa yote chanzo chake ni mungu. Mbaya zaidi ameyatengeneza alafu ameshindwa kuyaondoa.

Hii mada inaendelea.
Una proof wapi kwamba shetani au Mungi alikosea mpakq pahitajike marekebisho....?

Pili una reference/ushahidi ipi kuonesha uasi mwingine umetokea mbinguni..???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hajaanguka wapi ? Uliza swali lako vizuri.

Kwa uchache,iko hivi kipindi ambacho ana ambiwa amsujudie Adamu,Azzaziri alikuwa kwenye kundi moja na malaika,na kuna sababu iliyomfanya akawekw katika kundi moja na malaika.

Nipo ....


Hajala tunda
 
Manufacturer yeyote anapocreat kitu au anapotengeneza kitu huwa ameitend kuona kitu kile kitumike au kifanye kazi kama ilivyokusudiwa,na hivyo ili kifanye kazi kama ilivyotakiwa huyo manufacturer huwa anaweka manual book/leaflet iliyojaa maelekezo na maonyo juu ya namna ya utumikaji wa kifaa au kitu hicho,pia ndani ya manual book hiyo huwa kuna series of consequence ya kukiuka taratibu za utumiaji wa chombo hicho.

HUWEZI KUMWELEWA MUNGU JUU YA UUMBAJI IKIWA HUWAZI KAMA MANUFACTURER.Kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu duniani kama chombo chake au product yake ilikuwa ni lazima hicho chombo akipe maelekezo ya namna kinavyopaswa kutumika au kusurvive.

KUHUSU MUNGU KWAMBA HAJUI YAJAYO,SI KWELI,Unachopaswa uelewe ni kuwa Mungu amejiweka pembeni juu ya human willings,yeye ameumba utashi ndani ya mwanadamu kama kipimo cha utiifu wa yule aliyemuumba,kwahiyo anachokifanya juu ya utashi huo ni kukupa upime na kuamua mwenyewe ikiwa unachokifanya kinaonesha utii na uzuri kwa yule aliyekuumba au la sawa sawa na manual book yake,halafu pia Mungu hujifunga kwa neno lake,yaan yeye ndivyo alivyo uaminifu wake jinsi ulivyo unamzuia kuingilia mambo kadha wa kadha,mfano alipomwambia Adamu kuwa mkila mti wa matunda ule mtakufa,si kwamba wakati wanakula hakuwaona au hakuwa na nguvu za kuwazuia wasile,shida ni kwamba Neno lake akilitoa linamzuia kulivunja
 
Kwanza kabisa fahamu kuwa lile tukio halikuwa rahisi kwa Yesu kwa sababu lilikuwa kimwili pia. Na ndiyo maana unaona alipokwenda mlimani kuomba aliomba kama kikombe kile angeepushiwa lakini Mungu hakujibu kitu. Akafika sehemu akasema Roho I radhi lakini Mwili umegoma. Haiimaanishi kama Mungu akuwepo na wala hakusikia, ila kuna mida ya Mungu kujitukuza na kujichukulia utukufu wake. Kama isingekuwa Mungu kuwepo yamkini tusingekuwa na huu ukombozi.
Kabla ya kukata Roho alisema Baba uwasemehe kwa kuwa hawajui walitendalo (Mungu alikuwepo na Yesu).

Yesu hakukata tamaa Na ndiyo maana unaona alimwambia mmoja wa wale aliokuwa nao msalabani kwamba wangekuwa pamoja kwa Baba yake baada ya pale.

Kibinadamu, ni sahihi kabisa kwa binadamu kukata tamaa katika hali Fulani Fulani lakini iwe mwiko kuamini kama hali hizo ni hali za kudumu kwa sababu Mungu huwa pamoja nasi katika nyakati zote. Chukulia mfano wa Maisha ya Yusufu, Kutupwa na nduguze>kuokotwa na kina potifa> Kupelekwa gerezani > KUWA WAZIRI MKUU. Asingeweza kuwa waziri mkuu kama nduguze wasingemtupa. Asingekuwa Waziri mkuu kama asingesingiziwa kubaka na kupelekwa gerezani ambako ndiko fursa ya kuwa waziri mkuu ilitokea. Katika nyakati ngumu zote Mungu alikuwa na Yusufu na aliujua mpango wake.

Udhihirisho mwingine wa kujua kama Mungu huwa nasi katika magumu yetu ni kupitia kwa kina Meshaki na Abedinego. Walitupwa ndani ya moto watu watatu lakini Nebukadineza akaona watu wa nne, JE WAJUA MTU WA NNE ALIKUWA NANI?? Na hata baada ya kina Meshak kutolewa yule mtu wa NNE alibaki ile sehemu ya shida. Tatizo kubwa letu Binadamu, wakati wa shida huwa hatumuoni Mungu ila SHIDA.

NOTE: BIBLIA NI MAFUNUO YA YESU/ BIBLE IS REVELATION OF JESUS CHRIST.
1.Yesu ni nani ?
2.
Shetani asikilizwi? Do u hear urself? Hapo tu wewe umeshamsikiliza. Na mbona dini za shetani ziko nyingi tu watu wanajiachia au unataka asikilzwe vp? Watu wanapishana wa waganga kwasabsbu zao mbali mbali, hapo bafo unaniambia shetani hajasikilizwa? Wengine wana wanga usiku na mchana, we unasema hajasikilizwa? Iko hv Mungu hajamlazimisha mtu kumfuata ametupa option either shetani au yy, na uposema ametulazimsha kuingia mgogoro wake na shetan still hauko sahihi au cjui kama hata unaelewa unachoongea, mfano leo hii nduguyo wa kiume kaja nyumban kwako kaanza kumbaka mwanao wa kiume mpaka kamfanya shoga, utampenda mtu huyo? Sasa kama ww hutampenda iweje useme Mungu ametuingiza kwenye mgogoro na shetani usiotuhusu? Wakati anachokifanya Mungu ni kutuepusha na mambo mabaya kama hayo. Na sometimes its not the devil ni mtu mwenyewe mana hata shetani hakushawishiwa na mtu mwingine kumkosea Mungu ni tamaa zake yy mwenyewe na si yy tu kuna malaika wengine waliomkosea Mungu wakatupwa pamoja na shetani, hivyo hata binadamu wengine hufanya maovu wao kama wao bila hata ushawishi wa huyo shetani, ndo mana Mungu kwa kuwa alishajua binadamu aina ya shetani hawataisha (mfano halisi ni wewe) akatupa choice hakutaka kutufanya marobot kumfata kwa lazima, so kama wewe umeamua kutokumuamini Mungu na kwenda kwenye njia zako acha kutafuta ku justfy njia zako ishi tu upendavyo na ss tulioamua kumuamini Mungu tuache tulivyo huna haja ya kutuita wajinga mana tumechagua wenyewe kumuamini Mungu ndo mana ya demokrasia
wewe vitabu vyako vinamjadili shetani kama kiumbe kilichoasisi uovu , nakuuliza swali katika hili ni lini shetani alipewa muda wa kusikilizwa juu ya propaganda hizi mnazomtupia shetani ? yaaani vitabu vyenu , shutuma mtoe nyie kwa shetani halafu mdai mmempa mda wa kumsikiliza braza fikiri sawasawa
 
Lilete kwa kirefu sio kuchagua unachotaka wewe, shetani alijitapa kwamba Ayubu hawezi kumkosea Mungu kwa Mungu kampa kila kitu, Mungu akampa shetani go ahead take everyrhing uone kama mtu huyu atanisaliti. Na iko hv usizani kumuamini Mungu na kuzifuata njia zake means utastarehe, ufalme wake unatekwa na wenye nguvu, sio za kupigana ngumi nope, mana vitu yetu ss si ya damu na nyama bali ya kiroho hivyo watakaouteka ufalme wake ni wale watakaovumilia mpaka mwisho katika kumtii, imani na kuomba no matter what, ili kuchuja yale makapi
Kumbe pamoja na shetani kutupwa kumbe wanayajenga na Mungu kwa nafasi hivi
 
Mambo mengine yamebaki kuwa siri za mbinguni ambazo binadamu kwa akili zake za kawaida hawezi kuelewa wala kuamini kiurahisi. Kumbuka sisi ni wanadamu na tuna upeo fulani ambao hatuwezi kuuvuka tukajua mambo ya Mungu ambayo ni ya siri. Na kuna mahali kwenye biblia inasema siri za mbinguni zitafunuliwa kwa wale wamchao bwana (sijaandika exactly kama ilivyo kwenye biblia) maana sikumbuki ni kitabu gani na fungu gani ila hilo andiko lipo.

Hivyo kuna mambo ambayo kwa akili zetu na upeo wetu wa kibinadamu + dhambi zetu hatuwezi kuyaelewa kirahisi. Ni siri kuu za mbinguni. Kwa wale watakaomwona Mungu naamini hizo siri watafunuliwa. Pia tukumbuke kwamba hata mbinguni kwenye kuna madaraja na siri na uweza huenda kulingana na madaraja. Siyo kila kiumbe kilichopo mbinguni kinafahamu kila siri, Kumbuka hata yesu alipoulizwa na mitume wake kwamba ni lini mwisho wa dunia alijibu na nakuu kitabu cha Matayo Mtakatifu sura ya 24 fungu la 36 "Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye " Kama utaweza kusoma sura nzima ya matayo 24 pia utajifunza mengi.

mkuu kwann mwanadam alipokula tunda mungu alimfukuza bustanini asije kula tunda la uzima akaish wakat usio na kipimo

mkuuu hiiii kitu imekaaje hapo mbona kama mungu alikua na shaka juu ya adam yawezakua kitu kinachomfanya shetan na majin yawepo had leo hiii n kwamba yawezakua wenyewe walijua udhaifu wa mungu kabla alafu vp kama adam angekula tunda la uzima wanadam tungekua imortal

pili warumi 6;23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu ebu njoo unipe madin mkuu kuhusu hiiii kitu
 
Uko sahihi mkuu. Na unazungumziaje ile kauli "eloi eloi lama sabakthani/Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha" iliyotolewa na Mungu mwana (Yesu) kuonyesha kupoteza imani yake juu ya ahadi ya kulindwa na Mungu baba? Kama Yesu mwenyewe ambaye ni sehemu ya Mungu, tena mwanae pekee aliweza kukata tamaa na kusema maneno hayo kuna ubaya gani kwangu mimi binadamu wa kawaida tena dhaifu wa kizazi cha leo kufikia mahali nami nikakata tamaa ya kupata msaada wa Mungu?

Mkuu hii kauli ilitolewa kwasababu ilikuwa ni lazima upatanisho ufanyike kati ya mwanadamu na Mungu ni kwa wakati huo yesu mwana wa Mungu alitwishwa dhambi za ulimwengu wote abebe yeye ambaye hakuwahi fanya dhambi kabisa, ni kwa kitendo kile Mungu alidhihirisha kuwa yeye hafungamani na dhambi na kuuondoa utukufu wake kwa mwanae kwanza ili huo upatanisho ufanyike. Hii ni gharama kuu ya pekee aliyo ilipa Mungu mwenyezi kwa ajili ya wokovu wetu. Hii ni ishara kuu ya pekee kwa Upendo wa Mungu kwetu sisi wanadamu ambao pia hutuita watoto wake.




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
jambo lingine la kushangaza zaid mugu alipowaumba adam na hawa biblia inasema MWANZO 1;28 MUNGU ALIWAAMBIA wazaane na kuijaza dunia

swali linakuja kwann adam na hawa walipotenda dhambi ndio wakajua kua walikua uchi

je kama adam na hawa wasingetenda dhambi agizo la mungu lingetimia vp?
Na kitu kingine kama kweli mungu lengo lake lilikua ni kuinaza dunia ilikuaje akawapa laana ya kuwafupishia maisha yao hatimae kufa kabisa?

Ilikuaje mungu mwenye kusudio la kuwaruhusu binadamu wazaliane ili waijaze dunia ateketeze kizazi cha sodoma na gomora pamoja na kizazi cha nuhu?

Huyu mungu kweli ilikua ni lengo lake tuzaliane na tuijaze dunia kweli?

Sent using unknown device
 
 
Habari ya jumapili.
Dini inasema shetani aliasi huko juu mbunguni mahala palipotukuka na palipoinuka juu anapoishi mungu. Baada ya shetani kuasi mungu akamtimua na kumshusha huku Duniani.
Dini inasema baadae mungu akamuumba mwanadamu na kumuweka Duniani, maana yake mwanadamu alipowekwa duniani tayari shetani alikua duniani muda mrefu tu anakula zake maisha.
Hadithi ya shetani kuasi iko one sided, yaani inaelezwa kutoka upande wa mungu, hakuna aliewahi kusikia upande wa shetani(tayari binadam wanamshutumu shetani kwa habari ya kuambiwa, one sided story, hivyo shetani anahukumiwa kua ni mbaya bila kusikilizwa).
Dini haisemi kwa nini shetani aliasi na ilikuaje akaasi. Dini inasema mungu anajua kila kitu, all knowing lakini haisemi mungu alishindwaje kujua kua shetani atakuja kuasi ili asimuumbe. Na kama alijua shetani atakuja kuasi kwa nini alimuacha aasi. Mbaya zaidi huo mgogoro wao umetuingiza na sisi binadam ambao hatujui chanzo cha mgogoro. Yaani mungu anarecruit binadam washirikiane nae mwenye mgogoro wake na shetani huku binadam hawajui chanzo cha mgogoro wao. Na mungu anatishia kua yoyote ambae hatashirikiana nae kwenye mgogoro huo atampanish vikali. Unajiuliza hakuaje involved kwenye mgogoro nisioujua chanzo chake na natishiwa adhabu kali kama sitashiriki huo mgogoro, hivyo watu waoga na wajinga wanalazimika kushiriki mgogoro blindly ili kuogopa adhabu.
Kama mungu anawapenda wanadamu kama dini inavyosema alipaswa kurekebisha kasoro zilizojitokeza kabla ya kumuumba mwanadam, lakini pia alipaswa kujua in the first hand kua shetani atakuja kuasi kabla hajamuumba, vinginevyo hajui kila kitu kinyume na inavyosemekana kua anajua kila kitu.
Tukubali tukatae, maovu yote duniani kama mauaji, wivu, kifo, husda, wizi, matetemeko ya ardhi, tsunami, vimbunga, ukame, magonjwa yote chanzo chake ni mungu. Mbaya zaidi ameyatengeneza alafu ameshindwa kuyaondoa.
Hii mada inaendelea.
Mungu kujua yote kunahitaji utafiti. Pamoja NA hill la shetani, Mungu alijutia kumuumba mwanadamu hata kuamua kuleta gharika kumwondosha.
 
Nimekupa muda uthibitishe,sambamba na hilo unaweza kunipa njiacwanazo tumia wanasayansi kuthibitisha ukweli wa jambo ?
Njia wanazotumia wanasayansi kuthibitisha ukweli wa mambo unafikiri hata ukipewa utaweza kujua kua ni kweli kama bado akili yako iko mifukoni mwa watu?

Sent using unknown device
 
Habari ya jumapili.

Dini inasema shetani aliasi huko juu mbunguni mahala palipotukuka na palipoinuka juu anapoishi mungu. Baada ya shetani kuasi mungu akamtimua na kumshusha huku Duniani.

Dini inasema baadae mungu akamuumba mwanadamu na kumuweka Duniani, maana yake mwanadamu alipowekwa duniani tayari shetani alikua duniani muda mrefu tu anakula zake maisha.

Hadithi ya shetani kuasi iko one sided, yaani inaelezwa kutoka upande wa mungu, hakuna aliewahi kusikia upande wa shetani(tayari binadam wanamshutumu shetani kwa habari ya kuambiwa, one sided story, hivyo shetani anahukumiwa kua ni mbaya bila kusikilizwa).

Dini haisemi kwa nini shetani aliasi na ilikuaje akaasi. Dini inasema mungu anajua kila kitu, all knowing lakini haisemi mungu alishindwaje kujua kua shetani atakuja kuasi ili asimuumbe. Na kama alijua shetani atakuja kuasi kwa nini alimuacha aasi. Mbaya zaidi huo mgogoro wao umetuingiza na sisi binadam ambao hatujui chanzo cha mgogoro. Yaani mungu anarecruit binadam washirikiane nae mwenye mgogoro wake na shetani huku binadam hawajui chanzo cha mgogoro wao. Na mungu anatishia kua yoyote ambae hatashirikiana nae kwenye mgogoro huo atampanish vikali. Unajiuliza hakuaje involved kwenye mgogoro nisioujua chanzo chake na natishiwa adhabu kali kama sitashiriki huo mgogoro, hivyo watu waoga na wajinga wanalazimika kushiriki mgogoro blindly ili kuogopa adhabu.

Kama mungu anawapenda wanadamu kama dini inavyosema alipaswa kurekebisha kasoro zilizojitokeza kabla ya kumuumba mwanadam, lakini pia alipaswa kujua in the first hand kua shetani atakuja kuasi kabla hajamuumba, vinginevyo hajui kila kitu kinyume na inavyosemekana kua anajua kila kitu.

Tukubali tukatae, maovu yote duniani kama mauaji, wivu, kifo, husda, wizi, matetemeko ya ardhi, tsunami, vimbunga, ukame, magonjwa yote chanzo chake ni mungu. Mbaya zaidi ameyatengeneza alafu ameshindwa kuyaondoa.

Hii mada inaendelea.
Kila kilichotokea ni Mpango wa Mungu na watu wengi hukosa uelewa kwa kudhani kuwa Shetani anashindana na Mungu kitu ambacho sio kweli.
Shetani alimuomba Mungu afe mwisho ili awajaribu wanadamu na Mungu alimkubalia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una udhaifu mkubwa sana wa kulinganisha mambo,na hili sijaanza leo kukukosoa. Linganisha vitu vinavyoendana au kukaribiana na uhalisia.

Kushindwa kutofautisha mambo mawili yenye kufanana au kukaribiana kwa ukaribu sana ni uchache wa Elimu.

Nipo ....

Una udhaifu mkubwa sana wakucheka cheka ovyo nimekua nikikuweka kwenye mstari siku nyingi lakini bado napigia mbuzi gita

Kama kutokujua jibu nalo ni jibu basi kutokula nako ni shibe



Sent using unknown device
 
Habari ya jumapili.

Dini inasema shetani aliasi huko juu mbunguni mahala palipotukuka na palipoinuka juu anapoishi mungu. Baada ya shetani kuasi mungu akamtimua na kumshusha huku Duniani.

Dini inasema baadae mungu akamuumba mwanadamu na kumuweka Duniani, maana yake mwanadamu alipowekwa duniani tayari shetani alikua duniani muda mrefu tu anakula zake maisha.

Hadithi ya shetani kuasi iko one sided, yaani inaelezwa kutoka upande wa mungu, hakuna aliewahi kusikia upande wa shetani(tayari binadam wanamshutumu shetani kwa habari ya kuambiwa, one sided story, hivyo shetani anahukumiwa kua ni mbaya bila kusikilizwa).

Dini haisemi kwa nini shetani aliasi na ilikuaje akaasi. Dini inasema mungu anajua kila kitu, all knowing lakini haisemi mungu alishindwaje kujua kua shetani atakuja kuasi ili asimuumbe. Na kama alijua shetani atakuja kuasi kwa nini alimuacha aasi. Mbaya zaidi huo mgogoro wao umetuingiza na sisi binadam ambao hatujui chanzo cha mgogoro. Yaani mungu anarecruit binadam washirikiane nae mwenye mgogoro wake na shetani huku binadam hawajui chanzo cha mgogoro wao. Na mungu anatishia kua yoyote ambae hatashirikiana nae kwenye mgogoro huo atampanish vikali. Unajiuliza hakuaje involved kwenye mgogoro nisioujua chanzo chake na natishiwa adhabu kali kama sitashiriki huo mgogoro, hivyo watu waoga na wajinga wanalazimika kushiriki mgogoro blindly ili kuogopa adhabu.

Kama mungu anawapenda wanadamu kama dini inavyosema alipaswa kurekebisha kasoro zilizojitokeza kabla ya kumuumba mwanadam, lakini pia alipaswa kujua in the first hand kua shetani atakuja kuasi kabla hajamuumba, vinginevyo hajui kila kitu kinyume na inavyosemekana kua anajua kila kitu.

Tukubali tukatae, maovu yote duniani kama mauaji, wivu, kifo, husda, wizi, matetemeko ya ardhi, tsunami, vimbunga, ukame, magonjwa yote chanzo chake ni mungu. Mbaya zaidi ameyatengeneza alafu ameshindwa kuyaondoa.

Hii mada inaendelea.
Kwanza KABISA
Baada ya Duniani na Wanadamu kuwepo.ndipo Uasi ulitokea na SI,Kweli kwamba ulianza Uasi na kufuata Binadamu HApan

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Navyojua Mimi,Ibilisi amefungwa
Japo Kuna muda atafunguliwa na kupewa Mamlaka
Mimi hiyo pia niliifikiria sana nikajiuliza;

Kwanini Mungu kabla ya kumuumba mwanadamu hakumfungia shetani huko kuzimu mpaka siku ya kyama?

Kwanini Mungu pale Bustani ya Edeni akaweka ule mti wenye yale matunda ambao Adamu na mkewe waliyala na kupata dhambi?

Na kwanini Mungu alipoona Adamu na mkewe wamekula lile tunda na kulikuwa na mti mwingine pale wa uzima wa milele, Mungu akawazuia wasile matunda yake wasije wakasamehewa makosa waliyofanya kwa kula ule wa mema na mabaya?

SIJAPATA JIBU, mwisho nikasema, Mungu anampenda binadamu sana, hivyo hakuna atakayechomwa moto, wote tutaenda peponi siku ya mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naongezea

Kwanini baada ya adam na hawa kula lile tunda walijikuta wapo uchi, halafu akaagiza malaika wawafukuze akihofia wanaweza wakala tunda la mema wakaja kua kama yeye?

Kwanini adam na hawa baada ya kula lile tunda ambalo walishawishiwa na shetani mungu alitoa hukumu ya vifo kwa adamu na hawa tu halafu shetani akamuacha ale bata tu?

Kwanini yesu atoe pepo ahamishie kwenye nguruwe badala ya kuyaua? Huoni kama nguruwe ilifanyiwa fitna kwa serikali ya sasa hivi yesu angehukumiwa kwa kufanya ukatili dhidi ya wanyama na taasisi za haki za wanyama

Kwanini wachungaji wanatoa mapepo badala ya kuyaua? Wangekua wanayaua kulikua na uwezekano mkubwa yakawa yamepotea kwenye uso huu wa dunia, lakini kwanini wayatoe je wameshindwa kuyaua?

Kwanini vitabu vya mungu vinadai kua sisi niwadhambi sana kiasi kwamba hatuwezi kufanya mawasiliano physically na mungu, halafu tunaona huyo huyo mungu anakutana na shetani na wanapiga stori kama ni marafiki wasiokua na uadui?? Je inamaana siye ni wadhambi sana kuliko shetani mwenyewe??



Sent using unknown device
Ukisoma pale kwenye ile story ya Yule aliyepagawa na mapepo wale pepo walisema hivi "Tuna Nini nawe? Eeh Yesu mwana wa Mungu?!,Mbona umekuja kutuhukumu Kabla ya wakati wetu?! Tafadhali turuhusu tuwaingie Hawa Nguruwe!!"

unajua maana yake Ni Nini?!
Pepo/Demons Ni wale malaika waasi wakiongozwa na Lucifer ambao walifukuzwa mbinguni.
Muda wa hukumu yao ni Bado na WAKATI wa kuhukumiwa Bado KABISA
na ndiyo maana wakasema vile "Umekuja kutuhukumu kabla ya wakati wetu"

Kuhusu Swala la wachungaji na watu wa mungu.ipo hivi
Muda wa kuwaua/kuwahukumu mapepo Ni Bado na ndiyo maana wakiwa wanaomba/kukemea huwa wanasema
"Toka, muachie,huna mamlaka etc"
na c kusema Kufa au namna Gani..
Muda wa hukumu na umauti wao Bado

Soma Sana Vitabu vya dini UTAELEWA,

Karibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom