Kwanini Mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi ya HIV Tanzania?

Kwa muda mrefu nimekuwa nikisikia takwimu mbali mbali kupitia vyombo mbali mbali kuwa mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi na waathirika wa UKIMWI.

Swali langu ni la kidadisi(curiosity). Napenda kusikia toka kwa wataalamu na watafiti(kama tafiti zipo), kwanini isiwe majiji na mikoa mikubwa kama Dar, Mwanza, Mbeya n.k? Kama awali ilikuwa mkoa wa Kagera ndiyo ulioripotiwa mgonjwa wa kwanza na baadaye kuwa na waathirika wengi, ilikuwaje HIV iliruka mikoa ya hapo kati(Shinyanga, Tabora, Dodoma, Singida...) na kuufanya mkoa wa Njombe kuongoza?

Kama ni tohara kwa wanaume je, ni mikoa mingapi Tanzania hii walichelea kufanya tohara? Kwanini mikoa hiyo haijaathirika kiasi hicho? Japo kwa zamani(ninavyokumbuka) wilaya ya Makete(Njombe) ndiyo iliyokuwa ikiongoza na kwa sasa sina taarifa rasmi, bado ni jambo ambalo sina majibu yake, ilikuwaje mkoa wa Njombe uongoze kwa maambukizi?

Naomba wenye kufahamu majibu ya swali langu la msingi wanisaidie.

Kwanini Njombe?
Inaongoza kwa waathirika ka sababu ya kupenda kupima pima ukimwi
 
Njombe Hasa Hasa Kule Makete Ndo Kunaongoza Kwa Maambukizo Ya Ukimwi,sababu Hasa Ni Hali Ngumu Ya Uchumi Inayotokana Na Hali Ya Hewa Na Udongo Wa Makete Kutosupport Kilimo Hvyo Kufanya Vijana Weng Kukimbilia Dar Es Salaam Kusaka Maisha Na Huko Ndiko Wanakoambukizwa Na Kurud Nao Makete!.Idadi Kubwa Ya Maho
 
Ni asili na hulka za watu wa njombe kwani bado uelewa wao ni mdogo sana kuhusu ukimwi kwa mf;
1, bado wanatoana funza kwa kushare sindano moja
2, bado ngariba wanakeketa kwa kushare vifaa bila kuchemsha
3, Kurithiana bado wanatabia za kurithi wake za marehemu ambao wengi wamekufa kwa ukimwi.
4, Hulka binafsi (natural distintion) ya watu wa njombe huwa warahisi sana kushawishika kingono especially ladies kuna kale kausemi kao kasemako "we niangushe tu dhambi zako".
5, Mila potofu, wanaamini ni vibaya kutumia kodom ktk kuhondomola sasa hilo ni tatizo kubwa sana.
NB
serikali na NGOs zinajitahidi sana kwa sasa kutoa elimu ya kujikinga na kuepuka maambukizi ya UKIMWI njombe.
 
Njombe wanapenda kugegedana sana uncle zangu wengi wamefariki kwa UKIMWI ukisikia mwanamke ametoka njombe kama hujampima bora usimgegede.
 
Mkuu sidhani kua watu wote wa Njombe walioathirika waliupatia ugonjwa huo mkoani mwao (Njombe)

Bila shaka kuna waliokua wakiishi mikoa mingine nje ya Njombe,lakini baada ya kujigundua kua wameathirika ndipo wakafanya maamuzi ya kurudi mkoani kwao ili kua karibu zaidi na familia zao,
So, linapokuja suala la kuhesabiwa waathirika watahesabiwa ni waathirika wa Njombe na hawatohesabiwa kua ugonjwa huo waliupatia mkoa gani!

Huenda ikawa watu wa Njombe wanatabia ya kurudi mkoani kwao baada ya kuathirika ndio maana idadi ikawa ni kubwa mkoani humo,

Nimejibu kwa mtazamo wangu tu na niko radhi kusahihishwa na wataalamu,

One love.
Kuna mkoa fulani huko kaskazini, inasemekana watu huenda kuhesabiwa kila mwisho wa mwaka. Huoni kuwa hao pia wangekuwa waathirika?
 
Niliwahi kumuuliza daktari flani wa njombe hili swali nilichoambiwa ni kuwa njombe kuna hospital kubwa kama ikonda hosp, bulongwa hosp, kibena hosp, ikelu hosp lugarawa na ilembula hosp. Zote ni hosptali kubwa sana hivyo watu wengi wanafika kupata matibabu huko kutoka sehemu mbalimbali na wakipimwa vvu takwimu zinasoma njombe kwakuwa watu wengi hawatoi taarifa sahihi wanatoka wapi... Ila sijui kama ndo uhalisia wenyewe

Njombe kuna hospitali kubwa na nyingi kuliko Dar?
Njombe kuna watu wengi kuliko Dar?
 
kwa sababu mkoa wa njombe wakristo ni wengi,ushahidi angalia rate za maambukizi especially kwa mikoa yenye waislam wengi kama dar,tanga zanzibar n.k ndo utajua wapi wachafu wa matendo

Njombe inaongoza kwa idadi ya wakristo Tanzania nzima?
Unaweza kutusaidia uwianao wa idadi ya wakristo na dini nyingine kwa jiji la Dar, Arusha na Mwanza?
 
Takwimu zinaonyesha maambukizi njombe ni 14.8% na ndo mkoa unaoongoza. Sababu za maambukizi ya VVU kuwa juu ni:- Biashara ya viazi mviringo. Biashara hii huwaleta wafanyabiashara na madereva, matingo wa malory, na makuli ambao hulala vijijini wakikusanya na kupakia viazi. Watu hawa kwa kuwa na fedha hufanya sana ngono zembe na wanawake wa vijijini. Mbili, Tohara kwa wanaume haikwepo kwa Kabila la wabena, pangwa nk. Tatu, idadi ya wanawake mabinti ni ndogo kulinganisha na wanaume. Mkoa huu nazani ndio unaoongoza kwa kutoa house girls wengi Tanzania. Hivyo unakuta mwanamke mmoja anagombaniwa na wanaume kumi na zaidi no way out. Nne, Ulevi hasa kwa wanawake hasa njombe vijijini, na ludewa na makete pia. , Tano, house girls hurudi kwao na VVU na kwa uchache wa wanawake basi kila mwanaume kijijini ata mlala kwa uzuri wake.. Sita, uhaba wa kondomu vijijini. Maduka mengi vijijini hayauzi kondomu. Unaweza tafuta kondomu ludende siku nzima usiipate. Saba, biashara ya mbao nk
nane. kambi za kuvuna chai. upatikanaji wa pombe kwa bei rahisi ndiyo factor namba moja. ndiyo maana hiyo mikoa yote yenye chakula kingi na kusababisha pombe ya mahindi kuwa cheap na affordable kwa wengi UKIMWI upo juu. tuliowahi kunywa pombe tunajua nguvu yake.
 
Takwimu zinaonyesha maambukizi njombe ni 14.8% na ndo mkoa unaoongoza. Sababu za maambukizi ya VVU kuwa juu ni:- Biashara ya viazi mviringo. Biashara hii huwaleta wafanyabiashara na madereva, matingo wa malory, na makuli ambao hulala vijijini wakikusanya na kupakia viazi. Watu hawa kwa kuwa na fedha hufanya sana ngono zembe na wanawake wa vijijini. Mbili, Tohara kwa wanaume haikwepo kwa Kabila la wabena, pangwa nk. Tatu, idadi ya wanawake mabinti ni ndogo kulinganisha na wanaume. Mkoa huu nazani ndio unaoongoza kwa kutoa house girls wengi Tanzania. Hivyo unakuta mwanamke mmoja anagombaniwa na wanaume kumi na zaidi no way out. Nne, Ulevi hasa kwa wanawake hasa njombe vijijini, na ludewa na makete pia. , Tano, house girls hurudi kwao na VVU na kwa uchache wa wanawake basi kila mwanaume kijijini ata mlala kwa uzuri wake.. Sita, uhaba wa kondomu vijijini. Maduka mengi vijijini hayauzi kondomu. Unaweza tafuta kondomu ludende siku nzima usiipate. Saba, biashara ya mbao nk
Kula like mkuu.
Binafsi naunga mkono hoja ya biashara ya mbao na viazi. Hizo biashara zinafanyika kwa mapana sana na ndipo hapo wafanyabiashara hupata nafasi ya kurubuni wanawake vijijini kwa fedha nyingi na kuwalala.
Unategemea nini kama si kuambukizwa ukimwi?
Kingine ambacho umesahau ni njia panda. Ile ni njia panda ya kuelekea Mbeya na Ruvuma. Hivyo magari mengi hupumzika hapo baada ya kupima kwenye mzani. Sasa kama mjuavyo madereva wetu wakilala sehemu tena yenye baridi kama ile lazima walale na wanawake.
Mengineyo yote naunga mkono hoja zako
 
Ngojeni ni wambie watu wengi hawajajuwa kwa nini hizi tafiti zinaonesha hivi
Kwanza kabisa tujiulize mkoa wa njombe unawakazi wangapi halafu jiulize dsm inawakazi wangapi?
Kinacho fanyika nikwamba wakati watu wa miradi ya ukimwi wakienda vijijiini kupima watu serekali ya kijiji inaita watu wote wapime kwa nguvu wala sio hiali halafu wakija dsm wanaema watu wapime kwa hiali utapataje majibu sahihi
Dsm Wakazi 3milion
Njombe wakazi 1milion
Bado hujanidangany kuwa njombe inaongoza labda uniambie mkoa mzima wameathilika

Kwahiyo serikali za vijiji vya mkoani Njombe ndizo zinayoongoza kwa kulazimisha watu kupima UKIMWI kati ya mikoa yote Tanzania?
 
majibu hayaeleweki mi naona inawezekana kuna mikoa ina maambukizi makubwa kuliko njombe isipokuwa rate ya upimaji ni ndogo inawezekana njombe hospital nyingi ukienda kupata tiba ni sharti upime na hiv mfano lindi kuna hospital ukienda lazima upime kipimo kikubwa kwanza
 
Dar kuna watu wangapi kulinganisha na njombe? Hujui kijijini wakifa wanne na mjini wafe 10 wastani wake ni kuwa kijijini wamekufa zaidi?

Unazungumzia kufa
Takwimu zinaonyesha maambukizi njombe ni 14.8% na ndo mkoa unaoongoza. Sababu za maambukizi ya VVU kuwa juu ni:- Biashara ya viazi mviringo. Biashara hii huwaleta wafanyabiashara na madereva, matingo wa malory, na makuli ambao hulala vijijini wakikusanya na kupakia viazi. Watu hawa kwa kuwa na fedha hufanya sana ngono zembe na wanawake wa vijijini. Mbili, Tohara kwa wanaume haikwepo kwa Kabila la wabena, pangwa nk. Tatu, idadi ya wanawake mabinti ni ndogo kulinganisha na wanaume. Mkoa huu nazani ndio unaoongoza kwa kutoa house girls wengi Tanzania. Hivyo unakuta mwanamke mmoja anagombaniwa na wanaume kumi na zaidi no way out. Nne, Ulevi hasa kwa wanawake hasa njombe vijijini, na ludewa na makete pia. , Tano, house girls hurudi kwao na VVU na kwa uchache wa wanawake basi kila mwanaume kijijini ata mlala kwa uzuri wake.. Sita, uhaba wa kondomu vijijini. Maduka mengi vijijini hayauzi kondomu. Unaweza tafuta kondomu ludende siku nzima usiipate. Saba, biashara ya mbao nk

Mkuu ninashukuru kwa majibu yako mazuri. Umejibu sehemu kubwa ya maswali yangu. Nita-bookmark ukurasa huu kwa ajili ya kumbu kumbu zangu. Asante sana.
 
Pamoja na sababu nyinginezo, kwa muda mrefu mkoa wa Iringa/Njombe umekuwa kwa kiasi kikubwa unatoa wafanyakazi wa ndani katika miji mbalimbali hapa Tanzania.

Uwezekano mkubwa ni kuwa mabinti hawa wa ndani pindi wanaporudi nyumbani/vijijini wamekuwa pia wakirudi na virusi. Kwa mazingira ya vijijini kule, msichana akitoka mjini anakuwa na mvuto wa kipekee sana na hivyo kuongeza uwezekano wa kujiingiza kwenye relationships na wanaume zaidi ya mmoja.

Ni wanaume wachache hukumbuka/hujali kutumia condom kwa mwanamke mwenye mvuto mkubwa! Au hata kama atatumia, uwezekano mkubwa ni katika mkutano wa kwanza labda na wa pili...baada ya hapo condom huwa haina nafasi tena.
Nikichanganya maelezo yako na mkuu aliyekutangulia, napata kitu kikubwa sana. Ninawashukuru nyote kwa michango yenu.
Asanteni sana maana nimepata kitu.
 
Kuna mkoa fulani huko kaskazini, inasemekana watu huenda kuhesabiwa kila mwisho wa mwaka. Huoni kuwa hao pia wangekuwa waathirika?
Mkuu usipende kuamini habari za "Inasemekana" jaribu kuhukumu vitu kwa fact au kutoka source zinazoaminika.
 
Back
Top Bottom