Kwanini Mengi alipata utajiri: Nimebaini sababu

Kwanini Mengi alipata utajiri: Nimebaini sababu

Niambie kwanza kama you stand with Prof Assad maana sie badala ya kuwatia nguvu watu wetu wazidi kufanya vyema tunawafanyia mambo ya hovyo
 
Binafsi naona kilichomtajirisha Dk Mengi;

1. Kuzifahamu na kuzitumua fursa ambazo wengine hawakuzifahamu. Dk Mengi alianza ujasiriamali katika miaka ya 1980, hapo tayari alishaziona fursa, huku wengine wakiwa wamelala na ujamaa wao. Kuimba nyimbo za chama cha jenga nchi.

2. Kwa kujumlisha akili za kuzaliwa, mazingira maskini ya Tanzania kwa kipindi hicho yalimbeba Dk Mengi. Wanasema, mazingira maskini yana fursa nyingi sana. Sasa, kwa miaka 1980 uchumi wa Tanzania ulikuwa mbovu, vitu muhimu viliadimika. Hapo, mengi alianza kutengeneza na kuuza kalamu.

3. Safari ya kwenda Uskochi kusoma miaka ya 1970 ilikuwa ni exposha kubwa sana kwa Mengi. Kumbuka, kipindi hicho Watanzania wengi walikuwa wamefungwa na fikra za ujamaa, ilikuwa ni kuunga mkono juhudi tu za mwalimu wakati huo. Ulaya iliendelea zamani sana, hivyo mazingira na marafiki wa Ulaya walimuinsipaya sana Mengi.

4. Mwisho kabisa, Dk Mengi alikuwa ana akili ya kuzaliwa ya ujasiriamali, maana wapo Watanzania wengi walienda Ulaya miaka hiyo lakini hawakufanya ujasiriamali zaidi ya kupewa vyeo na Mwalimu.
 
Usemalo ni Kweli ila wanawapa tabu wafrika wenzetu [emoji23][emoji23][emoji23]
Mswahili huwa haaminiki na Mhindi kwa sababu amekaa kikupiga piga kila muda...ukimpa Lori aendeshe anawaza atakuibiaje mafuta,matairi na kubadilisha vipuri aweke vibovu vizuri akauze Kariakoo Ilala,...sasa mswahili pale hampendi Mhindi kwa sababu tairi likibasti huko barabarani anataka urudi nalo na liwe na namba zilezile...Mhindi auditing ya assets anaifanya kwa kina ukizingua huna kazi...sasa mswahili atampendea wapi Mhindi...matokeo yake atasema Wahindi wabaguzi kumbe ni yeye kakosa maadili ya kazi...
 
Niambie kwanza kama you stand with Prof Assad maana sie badala ya kuwatia nguvu watu wetu wazidi kufanya vyema tunawafanyia mambo ya hovyo
Sasa Prof. Assad anaingiaje kwenye sledi hii inayomzungumzia Mengi na Uaminifu wa Wahindi/Baniani katika business Management...Hebu dadavua kiyakinifu kabisa tukuelewe kisha tukupe sapoti kama unapaswa!
 
Sasa Prof. Assad anaingiaje kwenye sledi hii inayomzungumzia Mengi na Uaminifu wa Wahindi/Baniani katika business Management...Hebu dadavua kiyakinifu kabisa tukuelewe kisha tukupe sapoti kama unapaswa!
Kwani fani ya Prof Assad huijui? na utendaji wake uliotukuka hadi ma UN huko
 
nasikia sina uhakika benki nbc mengi alilamba hela mpaka benki ikafilisika je ni kweli alivyodaiwa akasema sio mimi ni kampuni ndio iliyokopa na kampuni imefilisika
 
Unawajua wahindi kwenye CV zao! Kule kuna ushindani sana as waliosoma ni wengi. Hivyo kila mhindi huhakikisha CV yake inanona hasa kuwa marketable. Si ajabu kukuta mhindi mmoja ana digrii mbili, masters tatu,postgraduate diploma kadhaa, short courses nyingi sana na phd mbili!
QUOTE="joseph1989, post: 31366333, member: 224824"]
UDART ishatushinda,inabidi tuwape wahindi.Wabongo upande wa kuremba CV tupo vizuri,micertificate kibao,sasa mpe kazi uone mavyongo yake,wazushi,wezi plus undugulization.
[/QUOTE
 
Mhindi anawekwa kulinda na kumbana mwafrika
 
Muhindi ukimuahidi kumsomeshea wanae, kumlipia kodi ya pango na mshahara mzuri atafanya kazi kwa bidii na uaminifu mkubwa sana. Na hata ikitokea kuna magumashi umepiga, hatatoa siri popote pale,

Kuna tajiri mmoja hapa bongo aliajiri mswahili akachoma dili zake... huyo mswahili akatekwa akafanywa kitu mbaya na sasa kaweka wahindi finance dept.
 
Ila nasikia ukifanya kazi na wahindi kama umewaajiri kwenye finance dept. jiandae kulipa kodi zote stahiki kwa sababu jamaa huwa hawataki ugomvi na government na huwa hawakwepi kwepi...ndio maana IPP group mara nyingi ilikuwa kinara kwa ulipaji kodi uliotukuka bila kusaza...
 
Wahindi si waaminifu. Ila wanatunza siri.
Ukiweka weusi kwenye hela jamii yote utajua una ngapi.
Pia huwa wako vizuri kwenye magumashi.
Did you know...Kutunza siri kumo ndani ya uaminifu...kwamba usiri ni branch ya uaminifu.
 
Eneo la Uhasibu Reginald Mengi aliajiri Wahindi ambao wanasifika kusimamia kwa uaminifu mkubwa finances...
Mfano mmoja wapo ni Mhasibu wa IPP FM Srinivas Chitanturi na wengine ambao wapo kwenye chain ya IPP kama wahasibu wakiwemo kule kwenye kampuni ya Maji na viwanda vyake...

Mengi sio tajiri wa kwanza kuwatumia watu wa asili ya Asia/India kusimamia kampuni zao...miongoni mwa matajiri wengine wanaotumia
sana raia hawa wa kigeni ni pamoja na Aliko Dangote ambae amekuwa akiweka Chief Finacial Officers kuwa wageni akiwemo Brian Egan aliehudumu kwa weledi wa hali ya juu na kwa uaminifu na kuiwezesha empire ya Dangote kuendelea kuchanja mbuga kama kinara cha uwekezaji Afrika...

Mwafrika mwingine tajiri ambae amekuwa akitumia wageni eneo la finances ni Mzimbabwe Strive Masiyiwa ambae ni miongoni mwa matajiri wakubwa Afrika ambae hapa Tanzania anamiliki TV1/Kwese,Raha nk na huko kwingineko ana makampuni lukuki unaweza kumtafuta wiki utamuona..... Huyu tajiri pia pamoja kwamba Chief Group Finance Officer wake ni mwanamama mwafrika lakini hajaacha kuwatumia wahindi ambapo msaidizi wa Finances za group ni Muhindi aitwae Minnesh Ajoodha....


Ukija kwa mzee wetu tajiri Bakhresa utagundua kwenye Finances pia kaweka Wahindi pale...Mfano Mkaguzi wa Hesabu wa ndani wakati fulani aliitwa Suraj Khandelwal sina uhakika kama bado yupo... lakini huyu ndo anakagua kuona usalama wa mapesa hapo Bakhresani...Lakini pia hapo hapo Bakhresa Mhindi mwingine kwa jina CA. AMAN VOHRA yeye ameshahudumu kwenye Idara ya Mapesa kama Mdhibiti Mkuu wa Rasilimali za kampuni.

MTAZAMO WANGU: Naamini kabisa kwa utafiti huu mdogo kwamba inaonekana kabisa kwamba Indians/Wahindi ni watu waaminifu na watu mahiri katika kupangilia expenditure na income kwenye kampuni...kwa hiyo niamini kwamba kama una plan ya kuibukia kwenye mega business hawa jamaa naamini ukiwaajiri kwenye eneo la finances unaweza kutoboa...Nina wasiwasi kwamba kwenye eneo la Uhasibu huenda sie ngozi nyeusi tunakosa uaminifu au tunashindwa kusaidia ukuaji wa businesses!

I stand to be corrected.






Hizi font colors huwa zinaua stim ya kusima uzi hata kama ni mzuri namna gani
 
Utajiri Wa MTU in siri ya MTU,staff management haina chochote kwenye asili ya utajiri Wa MTU.
Labda ungeweka kichwa cha Uzi wako kuwa staff management hasa ya waeshia imechangia pakubwa kuendeleza utajiri Wa bwana mengi
Utajiri hauna siri I disagree...labda ule wa kwenye hadithi za Alfu Lela Ulela za akina Mwajemi Mzuri na Nurdin au zile hadiths za Unyoya wa Kipanga Aziz...Utajiri una kanuni ambazo ziko wazi kabisa...hauji tu ghafla paa!...uchawi ndio unatufanya Africans tuamini utajiri ni mazingaombwe fulani ambayo anayafahamu tajiri husika pekee.
 
Haistaajabishi wanaongoza kwa kuwa tabaka la kati hasa wanapotoka nje ya taifa lao India...Nidhamu ya fedha sie huku tunaita ubahili.
MD wa bonite bottlers limited nafikiri ni muhindi. Hawa jamaa kwa mahesabu sio wa kuchezewa hata wakinunua peni ya sh 100 wanaandikia kwenye rekodi wana nidhamu ya usimamizi wa ela na mali
 
Back
Top Bottom