Kwanini Membe na Makamba walishindwa kufurukuta NEC?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,121
35,130
Mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM umekamilika na tayari John Magufuli ameibuka mshindi.
Jambo la ajabu kabisa ni kuwa mchakato huo umeacha machungu makubwa kwa baadhi ya wagombea na pia umeacha maswali makubwa juu ya mazingaombwe ya siasa za ndani ya CCM.

Familia ya Rais Kikwete ilikuwa tayari na mgombea wake Benard Membe huku akisindikizwa na January Makamba. Hizi ni kambi kubwa kabisa ndani ya CCM baada ya Edward Lowassa.

Jambo la ajabu kabisa ni namna Jina la Membe na Makamba lilivyoshindwa kufurukuta ndani ya Halmashauri kuu kiasi cha kuona wagombea dhaifu kabisa kama Amina Salum na Asharose Migiro wakipita.

Inawezekana kabisa nguvu ya kambi ya Lowassa iliwatengua kwenye Halmashauri kuu, lakini pia mwisho wa mchakato wa kumpata Mgombea urais katika mkutano mkuu ilipelekea John Magufuli kushinda kwa kishindo (87%) Je ni kura za kambi ipi zilizombeba Magufuli?
 
Lowasa ndo jibu... lakini Tanzania yetu haijengwi na jina la MTU,,, tunahitaji kiongozi sasa anayejua Umaskini wa wa tanzania
 
Cha muhimu ni kwamba mgombea wa familia ya ikulu alikatwa manina.. Asante lowasa umetuepusha na janga la bakari..
 
wanamtama wangewashangaa sana member wa nec kumpitisha membe
 
Tumempaisha Magufuli kuanzia mwanzo hadi mwisho. Kila mtu anajua hili. Tumemwadhibu JK kwa utovu wa nidhamu kwa timu kubwa, ndo tukaamua kuwala vichwa watu wake wote. Na kwa hasira yule aliyetegemewa zaidi ndo tumemfanya wa mwisho. Next time afahamu sisi hatupimiwi kwa kijiko!
 
CCM INA WENYEWE.
DSC09752.jpg
 
Mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM umekamilika na tayari John Magufuli ameibuka mshindi.
Jambo la ajabu kabisa ni kuwa mchakato huo umeacha machungu makubwa kwa baadhi ya wagombea na pia umeacha maswali makubwa juu ya mazingaombwe ya siasa za ndani ya CCM.

Familia ya Rais Kikwete ilikuwa tayari na mgombea wake Benard Membe huku akisindikizwa na January Makamba. Hizi ni kambi kubwa kabisa ndani ya CCM baada ya Edward Lowassa.

Jambo la ajabu kabisa ni namna Jina la Membe na Makamba lilivyoshindwa kufurukuta ndani ya Halmashauri kuu kiasi cha kuona wagombea dhaifu kabisa kama Amina Salum na Asharose Migiro wakipita.

Inawezekana kabisa nguvu ya kambi ya Lowassa iliwatengua kwenye Halmashauri kuu, lakini pia mwisho wa mchakato wa kumpata Mgombea urais katika mkutano mkuu ilipelekea John Magufuli kushinda kwa kishindo (87%) Je ni kura za kambi ipi zilizombeba Magufuli?


Membe Maembe Aliyokula Yalimvimbia Akashindwa Kujipanga Huku Makamba Nae Kamba Nyingi Zilifunga Uwezo Wake Wa Kupanga Mikakati.
 
Kweli lowassa ni nouma kikwete adi kufa kwake hataka asahau lowassa ni zaidi ya mwana jeshi kwa mipango ya kawaida tu ilepesa ya membe isingekamatwa ile el nimekukubali
 
Tumempaisha Magufuli kuanzia mwanzo hadi mwisho. Kila mtu anajua hili. Tumemwadhibu JK kwa utovu wa nidhamu kwa timu kubwa, ndo tukaamua kuwala vichwa watu wake wote. Na kwa hasira yule aliyetegemewa zaidi ndo tumemfanya wa mwisho. Next time afahamu sisi hatupimiwi kwa kijiko!

kauli za kupunguzia maumivu. Yaani kweli kwa akili yenu mlidhani EL au Membe mlitegemea wateuliwe na ccm!? Hilo lingewezekana tu iwapo JK angekuwa alishinda 2010 kwa kura halali za wananchi. Uozo na ubovu wa JK ni carboncopy ya EL na Membe.
 
Back
Top Bottom