Kwanini mbunge asifukuzwe kazi?

Kwanini mbunge asifukuzwe kazi?

Centrehalf

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2013
Posts
509
Reaction score
145
Nimeshangaa sana na maamuzi ya baadhi ya kamati za bmk kukataa kipengele kwenye rasimu ya katiba kina chowapa haki na mamlaka wananchi kumfukuza mbunge iwapo atashindwa kutimiza ahadi zake kwa wapiga kura wake.

Tangia lini mwajiriwa akajiwekea kinga ya kutofukuzwa kazi na mwajiri wake?kama wananchi wanahaki ya kumchagua mbunge ni kwanini wasiwe na haki ya kumfukuza iwapo atashindwa kutekeleza waliokubaliana au kuhama maeneo yake ya kazi?kwa hii wajumbe wa BMK mumeonesha jinsi mlivyodhamiria kunyonga haki za mwananchi wa nchi hii.

Sijui wenzangu mnaliona je hili?

Nawasilisha.
 
Si shanghai Kwan walishapewa huo mwongozo na jeikei
 
Tunasema tulichagua wabunge sio kwa sababu ya busara ila kwa sababu ya vishawishi vyao! Yanayotendeka BMK ni muujiza. Hivi wanafikiri bila sisi huo mshahara wataupata wapi? Sisi ndio waajiri wao wanatakiwa wawe kwenye vituo vyao vya kazi na watoe mrejesho wa kazi zao (performance indicators) na kama hauridhishi tuna haki ya kuwawajibisha moja kwa moja hakuna cha uonevu wala nini.

Wengine mlichaguliwa kwa kuchakachua/kuiba kura kwa hiyo sifa za kuwa wabunge hamna. Wengi mlihonga sana mkachaguliwa kwa hiyo hamna sifa stahiki.

Ubunge ni kazi kama kazi yoyote ile na ni lazima muwajibike/muwajibishwe!

Hata huo muda wa vipindi vitatu ni mwafaka kwa sababu mkishaingia mjengoni mnabweteka na kujisahau kwamba tuliwatuma mkachape kazi sio usingizi wala matusi. Kukiwa na ukomo ule utofauti utaleta changamoto kwa eneo husika na uwajibikaji utaonekana kwa kila kipindi. Tukubali kuwa ubunge si biashara ya familia. Vipindi vitatu nje na mwenzako akashike usukani zamu yake.
 
Nimeshangaa sana na maamuzi ya baadhi ya kamati za bmk kukataa kipengele kwenye rasimu ya katiba kina chowapa haki na mamlaka wananchi kumfukuza mbunge iwapo atashindwa kutimiza ahadi zake kwa wapiga kura wake.

Tangia lini mwajiriwa akajiwekea kinga ya kutofukuzwa kazi na mwajiri wake?kama wananchi wanahaki ya kumchagua mbunge ni kwanini wasiwe na haki ya kumfukuza iwapo atashindwa kutekeleza waliokubaliana au kuhama maeneo yake ya kazi?kwa hii wajumbe wa BMK mumeonesha jinsi mlivyodhamiria kunyonga haki za mwananchi wa nchi hii.

Sijui wenzangu mnaliona je hili?

Nawasilisha.
ndugu umeona mbali, hii ndiyo maana huwa na waambia hao washabiki wa ccm kuwatukana UKAWA na kukubali mchakato uendelee wajue kabisa kuwa katiba hii ni ya wana siasa na si ya wananchi,hivyo UKAWA wako sawa kabisa kutoka bungeni kwani walishaona mbali.
 
Kwa upande mwingine wa shilingi...nadhani wananchi wakiwa na uwezo wa kuwajibisha/kufukuza mBunge waliomchagua kutafanya wasiwe makini wakati wa kuchagua, kwamba hata wakichagua 'Bomu' bado wana nafasi ya pili na penginme ya tatu kufukuza hao waBunge. Na pia kutaongeza mianya ya rushwa na uhasama kwa walioshindwa kuhujumu walioshinda wafukuzwe. Kama kutaongeza umakini...ni bora mfumo wa sasa wa kutumikia kipindi kizima cha miaka mi5 uendelee, ili tujue tukichagua kwa sababu ya 'Pilau na fulana', then tunalo kwa miaka mi5!
 
Mkuu,CCM wanaandaa katiba yao sio ya wananchi,CCM hawataki uwajibikaji.
CCM wamejitoa ufahamu,kila mwenye akili timamu hawezi kukaa kwenye BMCCM.
Ukitaka kuwa CCM lazima uwe mental fresh (uwe na akili nusu nusu)
 
Back
Top Bottom