Kwanini matajiri wengi wana roho mbaya?

uchunguzi wake sikubaliani nao.....mi nilichunguza nikagundua maskini ndo tuna roho mbaya na ni wabinafsi....wivu....chuki zimetujaaa.....
Tena bila sababu
Maskini hata ikitokea akasaidiwa hudhani ni kwasababu msaidiaji anavyo vya ziada. Na wengi hawana malengo ya kutajirika na hivyo hubakia kuwaonea wivu waliofnikiwa au kuwasema vibaya pale wanaposhindwa kusaidiwa.
 
Kwasababu siri ya utajiri wao wanaijua wao.

Amin nakuambia Tajiri wa haki hawezi kua na roho mbaya isipokua anakua Mkali ,nahii nisababu Ukali husaidia kuendeleza mali.

Nb..ukali sio roho mbaya.
Wengi ukali ndo wanauita roho mbaya. Au ikitokea akakuomba usiweze kutimiza matakwa yake ndo wengi wanaita roho mbaya.
 
Ndio maana wakawa matajiri
 
Mimi ktk harakati zangu nimejifunza mengi. Nitawatetea matajiri. Iko hivi hakuna tajiri anayependa kufilisika. Hivyo fursa yeyote ya kupoteza hela kizembe ni shida kubwa kwake. Sasa mara nyingi watu wasio na uwezo sehemu tofauti iwe mamlaka za serikali au waajiriwa wao nk hufikiri kuwaibia hawa watu JAPO SI WOTE. wapo business partners wataleta deal proposal fake au genuine ila hawako serious.
.kumbuka huyo mtu hadi kufikia mafanikio u ayomuitia tajiri amehenya bin kusota. Sasa ww eti unaona ni rahisi tu ucheze deal umpige HELA. akiwa mpoleaana basi kila mfanyakazi atafanya michezo hiyo na hatimaye atarudi kwenye UMASIKINI. so wanajikuta hawana mbadala zaidi ya kuwa MAFIA. So ukitaka tajiri asiwe na roho mbaya kwako kuwa muungwana kwake
 
Nadhani unaongelea matajiri wa bongo, kweli bongo matajiri wengi wanaendekeza sana ushirikina na dhuluma pengine ni kutokana na ujinga uliotapakaa nchi nzima.
 
ukishakua maskini mara nyingi hukosa akili (sina maana mbaya)
nilikua na mtazamo wa kulaumu matajiri kwann wana roho mbaya isiyojali hali ya walio chini yake kwa saana.

ila wakati flani nilibahatika kua act kama tajiri na nikawa naendesha miradi flani flani nikasema ngoja nijaribu ku act yale yaliyo tofauti na matajiri lakini mwisho wa siku niliaribu ile miradi bila mafanikio.

maskini ukimsikiliza basi kila shida atakwambia imempata yeye hivo atahitaji pesa tuu, maskini kwanza hapendi kazi anapenda kupewa tuu, kuonewa huruma na kubebwa, hivyo wakijua tajiri wao yuko hivo basi jua kazi haito enda.

ili swala nilitamani kuliazishia nyuzi ila kwa kweli kuamaskini ni mkosi jamanii.... hatubebeki
 
Hyo ndo hali halisi kunawatu wajinga sana wanapenda kuleta mazoea kwenye pesa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…