Kwanini matajiri (watu waliofanikiwa) hudhani masikini ni wavivu?

Kwanini matajiri (watu waliofanikiwa) hudhani masikini ni wavivu?

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
745
Reaction score
1,470
Kabla ya yote, kwanza pita katika Thread 'Diamond Platnumz: Fanyeni kazi, acheni lawama, kila awamu, kila uongozi mnalalamika' kisha ndo tukae kujadili title ya uzi huu hapo juu “Nikwanini Matajiri (Watu waliofanikiwa) Hudhani Masikini ni Wavivu?”

Si Nasibu na Omari pekee ndio wamekuwa wakwanza kuongea suala hili. Mara nyingi katika mijadala ya kijamii na hata mazungumzo ya kawaida, utakuta wale waliofanikiwa wakiwa na dhana kwamba umasikini ni matokeo ya uvivu na kutofanya kazi kwa bidii. Watu wenye uwezo mkubwa kifedha huamini kuwa kila mtu ana nafasi sawa na wao ya kufanikisha maisha, na kwamba wale waliobaki nyuma hawajitumi vya kutosha. Hii imekuwa kama imani iliyojengeka, ingawa ukweli unaweza kuwa tofauti kabisa.

Wapo matajiri waliofanikiwa kutoka chini na kufanikisha maisha kwa bidii kubwa. Lakini changamoto ni kwamba mara nyingi huchukua safari yao kama kielelezo cha wote. Wanashindwa kuona kwamba mazingira hayafanani kwa kila mtu. Kuna watu wanaokua bila elimu bora, bila mtaji, bila mitandao ya kijamii inayowasaidia, au wakiwa wamezuiliwa na changamoto za kijamii na kiuchumi ambazo ni kubwa kuliko jitihada zao binafsi.

Pia, naona mtazamo huu huwasaidia baadhi ya matajiri kuhalalisha nafasi yao (utajiri). Kukubali kwamba bahati, urithi, au mfumo wenye upendeleo uliwasaidia inaweza kuwa ngumu, hivyo ni rahisi zaidi kulaumu umasikini kama matokeo ya uvivu. Kwa upande mwingine, mitazamo ya kitamaduni na kidini pia imechangia. Katika baadhi ya jamii, utajiri huchukuliwa kama baraka na umasikini kama ishara ya gundu, jambo linalofanya umaskini kuonekana kama kosa la mtu binafsi.

PIA SOMA: Thread 'Hivi kwanini hapa Tanzania matajiri au watu waliofanikiwa kimaisha hupenda kutuongopea kuwa wao wanafanya kazi kwa bidii?'

Lakini tukitazama kwa undani, masikini wengi hufanya kazi ngumu kuliko inavyofikiriwa. Wanalima mashamba kwa jembe la mkono, wanabeba mizigo, wanaendesha bodaboda kwa saa nyingi, au kufanya kazi zisizo na kinga wala maslahi bora. Kazi hizi ni ngumu sana, lakini kwa kuwa hazilipi vizuri, mara nyingi hudharauliwa na kuonekana hazina thamani (sa sijui kazi gani Naseeb na mwenzake wanazungumzia).

Hii limeniacha na maswali mengi sana: je, kweli umasikini unatokana na uvivu na kutofanya kazi kwa bidii, au ni matokeo ya changamoto za kimfumo na kijamii ambazo mara nyingi hazionekani kwa macho ya wale waliofanikiwa? Kwa nini baadhi ya matajiri hupuuza jitihada za masikini? Na je, tunawezaje kujenga mtazamo mpya unaotambua mchango wa kila mtu bila kuwapachika majina yenye kudhalilisha?
 
Eeeeh Atassa Atassa Atassa

Screenshot_2025-07-02-02-33-25-17_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12~2.jpg
 
Na kwanini masikini huwa wanawachukia matajiri hata bila sababu yaani? Hata kama hawajawafanya kitu
Si kweli ,huu ni uongo wa wazi ..Maskini hukaa na matajiri ili wapate chochote kitu ila hawapendi dharau...Halfu ishu ya umaskini na tajiri ni Maneno ya kusaidikika hayaba uhalisia.

Kila mtu anaishi maisha yake ,tatizo mnapoanza kulinganisha watu.
 
Iko hivyo duniani kote
Kazi za nguvu zilikuwa na thamani Karne ya 17 na 18.

Walithaminika wakulima makini, wavuvi hodari, wawindaji matata ila Karne ya Sasa akili ndio kila kitu.

Hata mziki wa Mond baada ya kufungiwa na vyombo vya habari Tanzania, alitumia akili kujitoa kwenye huo mkwamo.

Iwe kwetu chachu ya kupambana na sio unyonge wa kuona katuonea
 
Si kweli ,huu ni uongo wa wazi ..Maskini hukaa na matajiri ili wapate chochote kitu ila hawapendi dharau...Halfu ishu ya umaskini na tajiri ni Maneno ya kusaidikika hayaba uhalisia.

Kila mtu anaishi maisha yake ,tatizo mnapoanza kulinganisha watu.
Haya baada ya maelezo yote haya we ni tajiri au masikini tuanzie hapo kwanza
 
Hela inayopatikana kwa jasho na nguvu nyingi huwa haipigi kelele....
 
Wengi hawajaupata kihalali,
Aliyeupata kihalali anamheshimu maskini, coz anajua ni stage aliyoitoka na akizingua kidogo anarudi.

MUNGU kwanza
 
Na utajiri sio juhudi tu.
Ingekua ni juhudi, kila mtu angeupata.
Watu wana give up kufanya juhudi - kutokana hawaoni matokeo ya juhudi

Mhubiri 9:11 " _ _ _ _ Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili ...
 
Kabla ya yote, kwanza pita katika Thread 'Diamond Platnumz: Fanyeni kazi, acheni lawama, kila awamu, kila uongozi mnalalamika' kisha ndo tukae kujadili title ya uzi huu hapo juu “Nikwanini Matajiri (Watu waliofanikiwa) Hudhani Masikini ni Wavivu?”

Si Nasibu na Omari pekee ndio wamekuwa wakwanza kuongea suala hili. Mara nyingi katika mijadala ya kijamii na hata mazungumzo ya kawaida, utakuta wale waliofanikiwa wakiwa na dhana kwamba umasikini ni matokeo ya uvivu na kutofanya kazi kwa bidii. Watu wenye uwezo mkubwa kifedha huamini kuwa kila mtu ana nafasi sawa na wao ya kufanikisha maisha, na kwamba wale waliobaki nyuma hawajitumi vya kutosha. Hii imekuwa kama imani iliyojengeka, ingawa ukweli unaweza kuwa tofauti kabisa.

Wapo matajiri waliofanikiwa kutoka chini na kufanikisha maisha kwa bidii kubwa. Lakini changamoto ni kwamba mara nyingi huchukua safari yao kama kielelezo cha wote. Wanashindwa kuona kwamba mazingira hayafanani kwa kila mtu. Kuna watu wanaokua bila elimu bora, bila mtaji, bila mitandao ya kijamii inayowasaidia, au wakiwa wamezuiliwa na changamoto za kijamii na kiuchumi ambazo ni kubwa kuliko jitihada zao binafsi.

Pia, naona mtazamo huu huwasaidia baadhi ya matajiri kuhalalisha nafasi yao (utajiri). Kukubali kwamba bahati, urithi, au mfumo wenye upendeleo uliwasaidia inaweza kuwa ngumu, hivyo ni rahisi zaidi kulaumu umasikini kama matokeo ya uvivu. Kwa upande mwingine, mitazamo ya kitamaduni na kidini pia imechangia. Katika baadhi ya jamii, utajiri huchukuliwa kama baraka na umasikini kama ishara ya gundu, jambo linalofanya umaskini kuonekana kama kosa la mtu binafsi.

PIA SOMA: Thread 'Hivi kwanini hapa Tanzania matajiri au watu waliofanikiwa kimaisha hupenda kutuongopea kuwa wao wanafanya kazi kwa bidii?'

Lakini tukitazama kwa undani, masikini wengi hufanya kazi ngumu kuliko inavyofikiriwa. Wanalima mashamba kwa jembe la mkono, wanabeba mizigo, wanaendesha bodaboda kwa saa nyingi, au kufanya kazi zisizo na kinga wala maslahi bora. Kazi hizi ni ngumu sana, lakini kwa kuwa hazilipi vizuri, mara nyingi hudharauliwa na kuonekana hazina thamani (sa sijui kazi gani Naseeb na mwenzake wanazungumzia).

Hii limeniacha na maswali mengi sana: je, kweli umasikini unatokana na uvivu na kutofanya kazi kwa bidii, au ni matokeo ya changamoto za kimfumo na kijamii ambazo mara nyingi hazionekani kwa macho ya wale waliofanikiwa? Kwa nini baadhi ya matajiri hupuuza jitihada za masikini? Na je, tunawezaje kujenga mtazamo mpya unaotambua mchango wa kila mtu bila kuwapachika majina yenye kudhalilisha?
Siku ukiwa tajiri utafahamu kua kweli maskini ni wavivu matajiri wanafanya vitu ambavyo masikini vimewashinda kufanya sababu ya uoga na uvivu
 
MWINGINE ALIKUFURU akasema ETI,
UMASIKINI NI LAANA???

Hata matajiri wengi utajiri wao wameupata kwa NJIA ZISIZO HALALI,kuna MAFISADI MAJIZI ,WALANGUZI,WALA RISHWA..wezi,wakwepa KODIatapeli,waliopata kwa nguvu za giza kishirikina,waganga wa kienyeji,wachawi,freemansory,kumwaga damu za watu,kuzulumu,kuibaa,kutapeli,kuua n..k..boashara haramu,fushwa n
k

TAJIRI kuingia peponi ni vigumu kuliko ngamia kupenya kwenye tundu la sindano.
 
Siku ukiwa tajiri utafahamu kua kweli maskini ni wavivu matajiri wanafanya vitu ambavyo masikini vimewashinda kufanya sababu ya uoga na uvivu
Endelea kukumbatia ujinga, utajirina umaskini sio nguzu za kufanya kazi, ni mambo ya kiroho
 
Back
Top Bottom