Kwanini masikini hudharaulika kwenye jamii zetu?

Kwanini masikini hudharaulika kwenye jamii zetu?

Desire Dizaya

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2015
Posts
6,476
Reaction score
11,672
Habari wanajukwaa

Mimi leo napenda kushea nanyi hili suala linalonitatiza. Kwanini katika jamii zetu za sasa kama mtu ni wa kipato cha chini anadharauliwa ilhali mwenye pesa au tajiri anaheshimiwa na kuogopwa??

Je aina hii ya maisha iliwahi kuwepo tangu enzi za mababu zetu?

Utakuta mtu na pesa zake anafanya jambo sio zuri bali watu wanamchekea tu "oooh hamna tatizo." Sasa ukute ni maskini muokota makopo ama msukuma guta hapo uone hiyo mitusi.

Hata katika koo zetu za sasa, familia yenye pesa ndo wanapewa kipaumbele wale wa kubangaiza wanaachwa nyuma; kwanini? Jiangalie leo huna kitu umepanga Tandale kijumba kinakaribia kuanguka unavaa nguo za mia tano Manzese dharau utazopata na mitusi kwa walimwengu halafu fikiria Mungu akajibu maombi yako ukajenga mansion Mbezi unatembelea gari la bei mbaya, nguo zako sijui Uturuki uone watakujaje kwako.

Kwanini binadamu tu wanafki hivi? Katika maisha yangu mimi kamwe siwezi kumsimanga mtu sababu ya umaskini ama hali duni. Nanyi nawaasa muwe hivi kwani maskini na matajiri wameumbwa na Mungu mmoja.

Katika kitabu cha mithali 14;20 imeandikwa:- Maskini huchukiwa hata na jirani yake bali tajiri ana rafiki wengi! Sijui kwenye Quran wameandikaje anayejua aweke.

Mpende mtu kwa utu wake sio hali yake. Love u all JF members
 
Uzuri ni kwamba maskini duniani tupo wengi kuliko hao wenye kitu! Wakati kuna matajiri 10 wanaonidharau, nyuma yangu kuna maskini wenzangu 90 wanaoniheshimu na kunithamini!! Sasa ya nini nijishughulishe na hao 10 wakati nina jeshi la watu 90 nyuma yangu? Uzuri ni kwamba, ukiwa maskini basi kuna uwezekano mkubwa na familia yako nayo ikawa ni ya kimaskini... hivyo nao wanakuwa ni sehemu ya wale 90!
 
Asilimia kubwa ya masikini ni kwenda motoni, masikini kila wakati hawezi kukuwazia mema wewe uliye juu

Masikini wengi wao ni wachawi, roho mbaya na husda, masikini ana tabu kwenye maisha yake na hata baada ya kufa atapata shida kwani muda mwingi ni kuwazia mabaya kwa mwenzio

Usifanye dili na Mwenye njaa/masikini utaumbuka, kwani hawana misimamo kabisa

Omba kwa Mungu umasikini upungue ktk kizazi chako na ukoo wenu, mtaishi kwa amani sana maana MTU ana kitu chake
 
Uzuri ni kwamba maskini duniani tupo wengi kuliko hao wenye kitu! Wakati kuna matajiri 10 wanaonidharau, nyuma yangu kuna maskini wenzangu 90 wanaoniheshimu na kunithamini!! Sasa ya nini nijishughulishe na hao 10 wakati nina jeshi la watu 90 nyuma yangu? Uzuri ni kwamba, ukiwa maskini basi kuna uwezekano mkubwa na familia yako nayo ikawa ni ya kimaskini... hivyo nao wanakuwa ni sehemu ya wale 90!
Tafuta pesa mkuu
 
Asilimia kubwa ya masikini ni kwenda motoni, masikini kila wakati hawezi kukuwazia mema wewe uliye juu

Masikini wengi wao ni wachawi, roho mbaya na husda, masikini ana tabu kwenye maisha yake na hata baada ya kufa atapata shida kwani muda mwingi ni kuwazia mabaya kwa mwenzio

Usifanye dili na Mwenye njaa/masikini utaumbuka, kwani hawana misimamo kabisa

Omba kwa Mungu umasikini upungue ktk kizazi chako na ukoo wenu, mtaishi kwa amani sana maana MTU ana kitu chake
Hutaki kuwa mnafiki naona umefunguka.
 
Mwisho wa yote jibu ni Umasikini mbaya sana kuliko jambo/kitu chochote hapa duniani
 
Hii habari yote umeandika mwenyewe dadaangu
 
Ikiwa biblea imesema hivyo sasa hujalijua jibu tu.
Angalia Diamond alivyokuwa akiuza mitumba baba yake hakumtafuta lakini sasa amekuwa maarufu na hela anayo baba yake eti ndio anamjua mwanawe miaka yote alikuwa wapi wakati wa shida. Maskini huwa na hadhi wakati wa kampeni tu kwasababu ya kura yake ikimaliza tupa kulee.
 
1476023502213.jpg
 
Mkuu Baraka bb,acha dharau,

Mungu mwenyewe anataka pesa ndo akusaidie maombi yako kuna sadaka na fungu la kumi yote n kumtolea mungu sasa ww ukiwa masikin yote hayo utayatekeleza vip zaid ya kuweka kiwingu tu hapa dunian
 
Pesa ina nguvu,heshima,mamlaka,amri, Yuda amemsaliti Yesu sababu ya pesa hata hivyo pesa yako ilipo ndipo na moyo wko utakapokuwepo
 
Back
Top Bottom