Kwanini Majaji wanaapa mbele ya Rais na sio Jaji Mkuu?

muonamambo

JF-Expert Member
Sep 3, 2010
875
545
Wanabodi kuuliza si ujinga nataka kupata kufahamu tu. Najua kuna Mihimili mitatu kwa Maana ya Bunge , Mahakama na Serikali.

Na naambiwa mihimili hii ina Nguvu sawa na kujitegemea.

Nimeona wateule wa Serikali wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais.

Naona Wabunge wanaochaguliwa na wananchi wanaapa kwa Spika wa Bunge.

Swali sasa kwa nini majaji wateuliwe na Rais? Je kwa nini waape kwa Rais, wakati wapo kwenye Muhimili wa Mahakama?

Je huku si kusema kuwa ni Bunge pekee ambalo labda liko huru kidogo maana wabunge hawapaswi kuapa mbele ya Rais.?

Je, huku ni kusema kuwa Mahakama haiko huru maana Watendaji wake wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais?

Nauliza tu waungwana maana hii inanichanganya?
IMG_4720.JPG


Michango ya Wadau


Naomba nikujibu kwa msingi ya utawala na sio kisheria.
Tanzania kama ilivyo Marekani, Rais ana-play role ya mkuu wa nchi. Kwa kofia ya Ukuu wa nchi, anakua na madaraka ya kuteua na kuongoza kiapo cha utii kwa majaji.

Uingereza (The United Kingdom) majaji wanateuliwa na Malkia au Mfalime. Waziri mkuu (amabe ni mkuu wa serikali) anawajibika kumshauri Malkia nani wa kumteua akishirikiana na tume ya utumishi wa mahakama.

Ujerumani, jaji mkuu anakula kiapo mbela ya Rais wa Germany Federation (na sio Chancellor ambae ni mkuu wa serikali)

Israeli pia, majina ya majaji wanapendekezwa na tume ya kijaji (Judicial Nomination Committee). Anaewateua na Rais wa Israel ambae ni mkuu wa nchi.

Kwa kifupi sana, Tanzania, Rais kwa kofia yake ya Ukuu wa Nchi, katiba inampa nguvu ya kisheria na kiutawala kuchagua/kuteua majaji na kuwaongoza kula kiapo cha utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Niko tarari kukosolewa na kupata ufahamu zaidi toka kwa "wasomi na mawakili"
 
Wanabodi kuuliza si ujinga nataka kupata kufahamu tu. Najua kuna Mihimili mitatu kwa Maana ya Bunge , Mahakama na Serikali.
Na naambiwa mihimili hii ina Nguvu sawa Na kujitegemea.
Nimeona wateule wa serikali wanateuliwa Na Rais na kuapa kwa Rais.
Naona wabunge wanaochaguliwa na wananchi wanaapa kwa Spika wa Bunge.

Swali sasa kwa nini majaji wateuliwe na Rais ? Je kwa nini waape kwa Rais , wakati wapo kwenye Muhimili wa Mahakama?

Je huku si kusema kuwa ni Bunge pekee ambalo labda liko huru kidogo maana wabunge hawapaswi kuapa mbele ya Rais.?
Je huku ni kusema kuwa Mahakama haiko huru maana Watendaji wake wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais?

Nauliza tu waungwana maana hii inanichanganya?View attachment 1008124
Naomba nikujibu kwa msingi ya utawala na sio kisheria.
Tanzania kama ilivyo Marekani, Rais ana-play role ya mkuu wa nchi. Kwa kofia ya Ukuu wa nchi, anakua na madaraka ya kuteua na kuongoza kiapo cha utii kwa majaji.

Uingereza (The United Kingdom) majaji wanateuliwa na Malkia au Mfalime. Waziri mkuu (amabe ni mkuu wa serikali) anawajibika kumshauri Malkia nani wa kumteua akishirikiana na tume ya utumishi wa mahakama.

Ujerumani, jaji mkuu anakula kiapo mbela ya Rais wa Germany Federation (na sio Chancellor ambae ni mkuu wa serikali)

Israeli pia, majina ya majaji wanapendekezwa na tume ya kijaji (Judicial Nomination Committee). Anaewateua na Rais wa Israel ambae ni mkuu wa nchi.

Kwa kifupi sana, Tanzania, Rais kwa kofia yake ya Ukuu wa Nchi, katiba inampa nguvu ya kisheria na kiutawala kuchagua/kuteua majaji na kuwaongoza kula kiapo cha utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Niko tarari kukosolewa na kupata ufahamu zaidi toka kwa "wasomi na mawakili"
 
Kwenye vitabu ni kweli mihimili ni mitatu na inajitegemea kabisa; kila mmoja kwa namna ukivyoainishwa kwenye katiba.

Lakini kwenye uhalisia ndugu yangu hii nchi ina muhimili mmoja tu hiyo mingine ipo lakini mamlaka yanatoka kwenye ule mmoja ambao ndiyo Mkuu.
 
Wanabodi kuuliza si ujinga nataka kupata kufahamu tu. Najua kuna Mihimili mitatu kwa Maana ya Bunge , Mahakama na Serikali.
Na naambiwa mihimili hii ina Nguvu sawa Na kujitegemea.
Nimeona wateule wa serikali wanateuliwa Na Rais na kuapa kwa Rais.
Naona wabunge wanaochaguliwa na wananchi wanaapa kwa Spika wa Bunge.

Swali sasa kwa nini majaji wateuliwe na Rais ? Je kwa nini waape kwa Rais , wakati wapo kwenye Muhimili wa Mahakama?

Je huku si kusema kuwa ni Bunge pekee ambalo labda liko huru kidogo maana wabunge hawapaswi kuapa mbele ya Rais.?
Je huku ni kusema kuwa Mahakama haiko huru maana Watendaji wake wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais?

Nauliza tu waungwana maana hii inanichanganya?View attachment 1008124
Mahakama na Bunge ni vyombo huru ila havijitegemei!
 
Hata Mahakama yenyewe inaapa kwa la Raisi wa JMTZ hivyo haiwezi kumshitaki kwani hata ina Picha yake ukutani ije kuwa Majaji?

Raisi wa JMTZ yuko JUU ya Sheria zu JMTZ!
 
Kwa Tanzania rais ndiyo mkuu wa nchi ( The head of State), ana mamlaka na nguvu kubwa ukilinganisha na mihimili mingine ambayo haina mamlaka za kuteua na kuapisha wateule, Rais ana uwezo wa kisheria wa kuteua na kutengua baadhi ya nafasi za wateule.

Rais kama mkuu wa nchi/ Taifa huapisha wateule wake ili kuwapa mamlaka za kiutendaji zitokanazo na misingi ya haki na sheria.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo murua kabisa lakini kwa kuongezea hapo kwa rais ambaye pia ni mkuu wa nchi anateua hao majaji baada ya kupokea mapendekezo kutoka tume ya utumishi wa mahakama sio tu anajichagulia kwa utashi wake kama anavyoteua viongozi wengine wa serikali bali upelekewa majina kadhaa ambayo wanakidhi vigezo vya kuteuliwa kisha yeye ndio anachagua kadhaa kutoka kwenye orodha ya wale waliopendekezwa
Mkuu, Asante sana kwa nyongeza.
 
Back
Top Bottom