Kwanini Magazeti yanampuuza Kingwangalla?

Kwanini Magazeti yanampuuza Kingwangalla?

rosemarie

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2011
Posts
6,887
Reaction score
3,439
Najiuliza juhudi zinazofanywa na huyu Waziri kwanini zipuuzwe kiasi hiki? Katika magazeti yote ni habari leo peke yake limekuja na habari ya kufungia wafanyakazi nje saa moja na nusu asubuhi.

Kigwangala na ajifunze sasa kupuuzwa huku sio bure,najiuliza hizo kamera anazoenda nazo huko site zimekuwa zimeandaliwa au ni waandishi wanamsubiri getini asubuhi.

Waziri aache kuingilia kazi za watu walio chini yake,ampe jukumu HR ni majukumu yake
 
Wamechoka maigizo yake. Kigwangwalla huenda anataka kushindana na Wasanii wa tasnia ya uugizaji, maarufu kama Bongo Movies.
 
Hivi mpaka leo unasubiria habari za kwenye magazeti??
 
Bahati mbaya sana nimeona jana kwenye taarifa ya habari saa mbili usiku
kiukweli kilichofanyika ni usanii tu hamna lolote
mimi niwaombe mawaziri wangu kwamba wachape kazi sio kuuza sura wapo watu ambao wanapiga mzigo na wala hawahitaji promo ya media
hebu waige mfano kutoka kwao ningewataja majina lakini naamini wtz makini wanawajua mawaziri wachapa kazi
 
wapga mzigo akna magufuli enz zao walkuwa wanapga mzgo bla matangazo lakn waljulikana huyu mwehu anabeba wanahabari anaenda nao site hahaaaa ujana maji ya moto
 
na mimi kesho nashtukiza ziara ikulu...sihitaji waandishi
 
Leo asubuhi Azam TV mapitio ya magazeti ya wiki waandishi waalikwa Alan Mlawa na Jabir Idrisa wamempondelea kwa mbali kwa mmweweseko wake huo.
Aidha, wamewaponda waandishi was magazeti wanaoripoti matukio kama hayo bila kufanyia critical analysis vitendo vya aims hiyo.
Nikiri kuwa nilishangazwa na msimamo imara was Alan - nilidhani no tbccm.....!!!!!
 
Egoistic narcissistic character
That sums him up
 
Habari hiyo nimeiona Jambo Leo, Habari Leo na Mtanzania.
Hivi Magazeti ni yapi?
 
Kigwangala ni MD ambaye hajawahi kuajiriwa serikalini na akakaa hospital kama mtumishi. So kifupi he know no nothing about that organization. Msitegemee kipya hajui hata muundo tena hiyo wizara kwa sasa ilitakiwa kupata waziri ambaye either amewahi kuwa mtumishi hata kwenye halimashauri yaani cheo chochote kati ya DMO, DNO, DLT, DPharm au mkoani RMO na wenzake wanaounda RHMT hapo ndo angejua pa kuanzia. Kigwangala alikuwa WAMA (NGO) ya magumashi then akapata ubunge basi. Mdudu MSD na mauzo ya vifaa kwenye taasisi za umma hazijui na huyo Ummi ndo kabisa. Hiyo wizara inahitaji mtu anaye ijua nje ndani. Lasivyo maigizo yataendelea.
 
Tatizo Ni Kuwa Hawa MAWAZIRI Karibia Wooote Tu, Wanataka KUMUONYESHA Aliyewateua Kuwa Wanafanya Kazi Zao Kwa UMAKINI! Kumbe Wanajitia Ktk MIGOGORO Na WATENDAJI WAO!!! Hivi Wizara Ya Kigwangwala Tatizo Lake KUBWA Ni Wafanyakazi Wake Kuchelewa Kufika KAZINI Hasa Pale HQ!!!!??? Mbona Hii Ni Wizara Yenye Changamoto, Shida, Kero Na Matatizo Lukuki TANZANIA NZIMA, Kuanzia MIJINI Hadi VIJIJINI!!! Hiyo TC SCAN Na MRI Ziko Muhimbili Tu, VITANDA, MASHUKA, DAWA, VIFAA TIBA Na MAJENGO Ni Tatizo KUBWA TANZANIA NZIMA!!! Badala Ya Kujipanga KUTEKELEZA Ahadi Ya KUJENGA Vituo Vya Afya Kila Kata, Zahanati Kila Kijiji, Hospital Kila Wilaya Na Hospital Ya Rufaa Kila Mkoa!!! MATOKEO Yake Wanahangaika Na WATU Ambao Wana Impact Ndogo Kwa WATANZANIA!!!!! MAWAZIRI, MAKATIBU WAKUU, WAKURUGENZI, WAKUU WA MIKOA NA WILAYA Wafanye Kazi Zao UTARATIBU Na SHERIA, WASIISHIE Kuwa Vituko Kwa KUHOFU Kutenguliwa Uteuzi Wao Na Aliyewateua!!!
 
Nilidhani ni mimi mwenyewe nimempuuza kumbe kuna watu makini kama mimi wamempuuza.
 
Yeye anafikiri watumishi wote wanaishi magomeni!???
 
Ni UTOTO tu, akikua atajitambua na kuacha maigizo. Kuna kazi nyingi kweli za kufanya ktk Wizara hiyo,dogo hazioni badala yake anaigiza aliyoyafanya Mzee Magu. Ubunifu ni muhimu ktk kusimamia maendeleo ya Nchi na Wananchi, siyo maigizo. Anyway, ni mwanzo, labda watabadilika.
 
Kigwangala ameamua kutumia tasnia ya maigizo kumfunika Waziri wake Mh.Ummy.
Akimalizana na Ummy atamfunika Mh.Waziri Mkuu ili ile ndoto yake ya Urais itimie.
 
Acha uongo kuna waziri aliyeweza kushindana na Magu kwa promo hadi sasa hivi?
 
Dada ngoja ufike wakati wako wa kujifungua alafu uende hospital ukakute hamna daktari ndo utajua umuhimu wa alichofanya Kigwangala,,,, hii nchi inasikitisha sana kuona uchama umetugawa kiasi kwamba anachofanya mpinzani wako hata kama ni shaihi unaona si sahihi!

Kumbe hawa wafanyakazi wanafanya watakayo huko maofisini wakijua Mitanzania ni mijinga, haitafanya lolote, na mtu akitokea kujaribu kuwaweka sawa, watatetewa na Mitanzania hiihii inayolalamikia huduma mbovu!
 
Dada ngoja ufike wakati wako wa kujifungua alafu uende hospital ukakute hamna daktari ndo utajua umuhimu wa alichofanya Kigwangala,,,, hii nchi inasikitisha sana kuona uchama umetugawa kiasi kwamba anachofanya mpinzani wako hata kama ni shaihi unaona si sahihi!

Kumbe hawa wafanyakazi wanafanya watakayo huko maofisini wakijua Mitanzania ni mijinga, haitafanya lolote, na mtu akitokea kujaribu kuwaweka sawa, watatetewa na Mitanzania hiihii inayolalamikia huduma mbovu!
Kama kuchelewa kazini ni tatizo basi abuni mfumo wa kuwafanya watu wawahi kazini nchi nzima katika hospitali zote.Sio kufanya ukorokokoroni ili apata umaarafu katika vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom