Magezeti mengi ya Tanzania hayana maana,yamejaa uwongo na propaganda.Kuna facts nyingi lakini wao hawataki kuandika.Pia waandishi wanaendekeza njaa wananunuliwa hovyohovyo.Mwandishi yuko tayari kuandika habari ya kumchafua mtu kisa kapewa pesa.Taalum ni yakwako lakini mwandishi wa kitanzania kwa maksudi anakubali kutumiwa,ni ujinga mtupu.Watalalamika siku zote,vinginevyo wajirekebishe.Binafsi naishia tu kusoma na kusikiliza vichwa vya habari na kuwaenjoy waandishi uchwara kama mkapa alivyokuwa akiwaita
Halafu ukichunguza kwa umakini magezeti mengi uandishi wake unaweza ukasema yana haririwa na mtu mmoja.Yes,huo ndiyo ukweli.Huwa nachunguza kwa umakini sana magezeti mengi yanarudi.Si kweli kwamba watu hawana hela,angalia kwenye kumbi za starehe,angalia watu wanavyochangamkia bidhaa zingine.Mtu hawezi kutoa 500 au 1000 yake kisha asome habari iliyopikwa.Haya unapeleka sehemu copy 100,hata haziishi hakuna kitu hapa,watu wanaona bora wanunue magazeti ya udaku na michezo kuliko haya yanayojita ya siasa na uchambuzi.
.Kwa maksudi niliamua ninunue pc yangu ili nijitafutie mwenyewe habari,siko tayari kulishwa -----.