Kwanini Maafisa wa jeshi huongezeka kila mwaka?

Kwanini Maafisa wa jeshi huongezeka kila mwaka?

Jumong S

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
7,449
Reaction score
10,788
Wadau,

Leo Arusha Amiri jeshi Mkuu anawapa kamisheni wanajeshi zaidi ya 400! Kila mwaka si chini ya idadi hiyo wanakuwa Maafisa.

Mshahara unapanda, wanapewa vikundi vya jeshi vya kuongoza, wanapewa nyota moja na kisha kupangiwa vituo vya kazi.

Je, kwa hatua hii, jeshi si linakuwa na maafisa wengi zaidi ya mahitaji? Je, bajeti ya nchi si inakuwa kubwa? Je, hii ni picha ya ukubwa wa jeshi letu ambalo linahitaji Maafisa wengi zaidi?

Nawatakia kazi njema Maluteni Usu wapya!

Karibuni kazini sasa!

Uzalendo kwanza.
 
Ni kwanini madaktari wanaajiriwa kila mwaka?

Ni kwanini waalimu wanaajiliwa kila mwaka?

Majibu ya hayo maswali yanafanana na majibu ya swali lako!
 
Hizo ni ajira za kila mwaka kijana. Na ukumbe jeshi bado linahitaji watu,wengine wanakufa,wanastaafu, wanaacha kazi,wanafukuzwa kazi,wanaugua/ ukilema /unfit na zaidi wengine WANAAMIA KWENYE SIASA.

Ni sawa na kuuliza kwanini kila mwaka wanafunzi wanahitimu?
 
Tena kwa taarifa yako sio kila mwaka tu

Mara nyngne anatoa kamisheni mara mbili au tatu

Toka aingie hii ni kamsheni yake ya tano
Mbili katoa Monduli
Mbili Ikulu
Hii ya tano
 
Wadau!
Leo Arusha Amiri jeshi mkuu anawapa kamisheni wanajeshi zaidi ya 400! Kila mwaka si chini ya idadi hiyo wanakuwa maafisa. Mshahara unapanda, wanapewa vikundi vya jeshi vya kuongoza, wanapewa nyota moja na kisha kupangiwa vituo vya kazi!

Je, kwa hatua hii, jeshi si linakuwa na maafisa wengi zaidi ya mahitaji? Je, bajeti ya nchi si inakuwa kubwa? Je, hii ni picha ya ukubwa wa jeshi letu ambalo linahitaji maafisa wengi zaidi?

Nawatakia kazi njema maruteni Usu wapya!!

Karibuni kazini sasa!!!

Uzalendo kwanza.
Unajua idadi ya maafisa wanaostaafu jeshi kwa mwaka?Unajua mahitaji ya jeshi kwa upande wa maafisa?

Unajua wangapi wanafariki ama kufukuzwa kaz kwa mwaka?

Unajua mahitaji ya ulinzi wa amani sudani, kongo, lebanoni, ivory coast n.k?

Unajua idadi yao kwa ujumla?

Baada ya kujua hayo basi rudi darasani ukasome uelimike
 
Unajua idadi ya maafisa wanaostaafu jeshi kwa mwaka?Unajua mahitaji ya jeshi kwa upande wa maafisa?

Unajua wangapi wanafariki ama kufukuzwa kaz kwa mwaka?

Unajua mahitaji ya ulinzi wa amani sudani, kongo, lebanoni, ivory coast n.k?

Unajua idadi yao kwa ujumla?

Baada ya kujua hayo basi rudi darasani ukasome uelimike
Ndio maana nikauliza! Assume kwa mwaka wakapewa kamisheni askari 800, je inamaanisha kuna wastaafu na vifo vya idadi hiyo?
 
Ndio maana nikauliza! Assume kwa mwaka wakapewa kamisheni askari 800, je inamaanisha kuna wastaafu na vifo vya idadi hiyo?
Tatizo umeuweka ubongo wako kwamba haiwezekani jibu likawa NDIO lakini ukitaka kukubali basi fungua ubongo wako
 
Taasisi zingine za serikali wastaafu no wachache sana!

Ndio maana mhe, Rais alitoa pendekezo la kufanya uhakiki wa umri kwa watumishi wote, maana kuna vibabu na wabibi wameziba nafasi za vijana hawataki kustaafu.
 
Wadau!
Leo Arusha Amiri jeshi mkuu anawapa kamisheni wanajeshi zaidi ya 400! Kila mwaka si chini ya idadi hiyo wanakuwa maafisa. Mshahara unapanda, wanapewa vikundi vya jeshi vya kuongoza, wanapewa nyota moja na kisha kupangiwa vituo vya kazi!

Je, kwa hatua hii, jeshi si linakuwa na maafisa wengi zaidi ya mahitaji? Je, bajeti ya nchi si inakuwa kubwa? Je, hii ni picha ya ukubwa wa jeshi letu ambalo linahitaji maafisa wengi zaidi?

Nawatakia kazi njema maruteni Usu wapya!!

Karibuni kazini sasa!!!

Uzalendo kwanza.


MBONA HUULIZI WATU WANAOZALIWA KILA SIKU??
 
Jeshi litaajiri kila mwaka au kila baada ya kipindi fulani kwa kadri ya bajeti itakavyoruhusu .
North Korea ina watu jumla ya milioni 25 wanajeshi walioajiriwa kama wanajeshi(askari na maofisa) wanapata jumla ya laki saba. Tanzania tupo watu 50 watumishi wa umma plus wanajeshi jumla inakuwa kama laki 5 hivi.
Unapata picha gani hapo?
Serikali naiomba iongeze maafisa na askari wa majeshi yote kwa nguvu zote kwa kadri ya bajeti yetu.
Security haipaswi kuchezewa wala kujaribiwa.
 
Ndio maana nikauliza! Assume kwa mwaka wakapewa kamisheni askari 800, je inamaanisha kuna wastaafu na vifo vya idadi hiyo?
wengine katika hao wanatoka mataifa Ya Jirani : Comoros, seashells, congo+congo, Kenya, Uganda, Juba et cetera
 
Wadau,

Leo Arusha Amiri jeshi Mkuu anawapa kamisheni wanajeshi zaidi ya 400! Kila mwaka si chini ya idadi hiyo wanakuwa Maafisa.

Mshahara unapanda, wanapewa vikundi vya jeshi vya kuongoza, wanapewa nyota moja na kisha kupangiwa vituo vya kazi.

Je, kwa hatua hii, jeshi si linakuwa na maafisa wengi zaidi ya mahitaji? Je, bajeti ya nchi si inakuwa kubwa? Je, hii ni picha ya ukubwa wa jeshi letu ambalo linahitaji Maafisa wengi zaidi?

Nawatakia kazi njema Maluteni Usu wapya!

Karibuni kazini sasa!

Uzalendo kwanza.

Bahati nzuri sana hata Sheria za nchi haziruhusu Mtu yoyote kuhoji ama Bajeti au matumizi ya Wizara ya Ulinzi na ile Idara nyeti ya ( Eagle Wing House Oysterbay ) tena ni mwiko hivyo nikuombe tu usipoteze muda wako kutaka kuyajua mengi ya hizo Taasisi Kuu na Nyeti za Kimedani hapa nchini Tanzania.

Uwingi wa Maaskari pia hutegemea na nguvu Kazi ama iliyopotea au ile inayokaribia Kustaafu lakini kama haitoshi Tanzania ni nchi kubwa na Kiufundi zaidi hata hawa Wanajeshi unaodhani ni wengi nao hawatoshi vile vile na hata hao ambao tumesikika kuwa wataajiriwa na Wao pia hawatotosha.

Unaposema kuwa unaona uwepo Wao kuwa wengi kutaitia nchi hasara hasa kwa kuwalipa Mishahara mingi kidogo napatwa na mshtuko kama kweli Wewe ni Great Thinker uliyetukuka. Kuna kauli moja ya Mwingereza isemayo ' if you think eduacation is expensive then try ignorance '. Kipaumbele namba moja cha Tanzania yetu hii ni Ulinzi na Usalama hivyo hakuna jinsi zaidi ya kuwa na Wanajeshi wa kutosha ambao watailinda ipasavyo nchi yetu na mipaka yake. Na kama haitoshi hawa hawa Wanajeshi watakuwa pia wanatumika katika kuzilinda vilivyo rasilimali zetu ambazo kama zikilindwa vizuri na kuuzwa vile inavyotakiwa Tanzania inaweza kupata Kipato zaidi kutokana na Rasilimali zake kisha kusaidia kuongeza thamani na kukua kwa Uchumi hali ambayo itasaidia hata kuweza kuwalipa Mishahara hao Wanajeshi na Chenji ikabaki ikajenga nchi.

Jeshi na Usalama ndiyo Viungo muhimu katika nchi yoyote ile inayojitambua / inayojielewa kwani bila uimara wao thabiti sidhani kama hata Mimi na Wewe tungekuwa huru hivi hadi tunajiachia kutiririka na kuserereka humu Jamvini JF tofauti na mataifa mengine wao machafuko Kwao ni lazima kama vile Mkatoliki kufanya ishara ya Msalaba kila mara.

Mchana mwema.
 
Wadau,

Leo Arusha Amiri jeshi Mkuu anawapa kamisheni wanajeshi zaidi ya 400! Kila mwaka si chini ya idadi hiyo wanakuwa Maafisa.

Mshahara unapanda, wanapewa vikundi vya jeshi vya kuongoza, wanapewa nyota moja na kisha kupangiwa vituo vya kazi.

Je, kwa hatua hii, jeshi si linakuwa na maafisa wengi zaidi ya mahitaji? Je, bajeti ya nchi si inakuwa kubwa? Je, hii ni picha ya ukubwa wa jeshi letu ambalo linahitaji Maafisa wengi zaidi?

Nawatakia kazi njema Maluteni Usu wapya!

Karibuni kazini sasa!

Uzalendo kwanza.
Mkuu wewe ni zero kwenye mambo ya jeshi. Kwani makada wa ccm hamuongezeki kila mwaka?
 
Mkuu naomba tofauti kati ya kufa na kufariki Tafadhali.

7f0d3bbcb63b15c7fee5bc6b2238840e.jpg
 
Back
Top Bottom