emmanuel1976
JF-Expert Member
- Jun 17, 2011
- 301
- 79
Unajua shida yetu wa TZ kubwa ni tabia ya kukubali kuaminishwa, Lowasa ana matatizo kidogo sana ukilinganisha bidii na umahiri wake katika siasa, hatujasema kuwa hakuna wengine ila tujenga hoja kuwa yeye alichafuliwa na anaziidi kuchafuliwa na kwa kuwa ukweli uko wazi si busara kuendelea kumchafua Lowasa. Si katoka madarakani mika 4 iliyopita mbona shida ndo kwanza zinazaliwa na nchi imewashinda, shule alizojenga Lowasa sasa ni mapagara tu yanayoongeza mzigo kwa taifa. Ukweli ni kwamba Lowasa kaonewa na wanazidi kumdharirisha sana, hii haikubaliki hapa. AListuambia kwa ufupi tu kwamba kilichokwa kinatafutwa wakati akiwa waziri mkuu ni uwaziri mkuu wake na tuliona ukichukuliwa machoni pake. Alipigwa shavu akanyamaza mbona wanaendelea kumfuata? Wanataka kumuua? Watanzania tumejua ukweli hatumtupi Lowasa sasa kwani atatusaidia kutuonyesha mlango wa kutokea kwa vyovyote vile