Kwanini kuna katazo la kutowapa watoto wachanga chini ya miezi sita kitu chochote zaidi ya Maziwa ya Mama?

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Jan 2, 2023
233
563
Nakubaliana kabisa kuwa maziwa ya mama yanavirutubisho vyote anavyohitaji mtoto

Nakubaliana kabisa kuwa maziwa ya mama ni chakula bora na muhimu kwa mtoto mchanga na anatakiwa kunyonyeshwa hadi anapofikisha angalau miaka miwili

Nisichokielewa ni hii kampeni ya miaka ya hivi karibuni ya kuwahimiza kina Mama kutowapa watoto wao kitu chochote isipokuwa maziwa ya mama tu hadi atakapofikisha miezi sita

Kwa umri wetu wengi mlioko jukwaa hili hatukukumbana na hii kampeni kitu kinachomaanisha wazazi wetu walitulisha walivyoona vinafaa sisi kula hata kabla ya miezi sita na tulibaki salama

Hawa wataalamu wa afya wameona madhara gani tuliyoyapata sisi ambayo hawataki hawa watoto wetu wayapate?

Kwanini hii kampeni inahusu watoto wote bila kujali kwamba kila mtoto anazaliwa na utofauti? Ni kweli kuwa mtoto anayezaliwa Kigoma vijijini huko na mama aliyekuwa anashinda shambani toka mimba inatungwa atakuwa sawa na mtoto anayezaliwa Masaki na mama aliyekuwa anashinda kwenye kiyoyozi na kutembelea gari toka mimba inatungwa?

Hawa watoto wanaozaliwa mazingira tofaufi kwanini wapangiwe matumizi sawa ya chakula hadi watakapofikisha miezi sita?

Je, waliofanya tafiti na kuja na haya mapendekezo walifanya tafiti zao Tanzania au yalikuja maandiko tu kutoka kwa wadhamini? Kama yalikuja maandiko, tuna uhakika gani kama mazingira waliyofanyia tafiti zao yanaendana na mazingira yetu?

Karibu tujadili kwa pamoja
 
Kabla ya miezi 6 mfumo wa umeng'enyaji wa chakula unakuwa haujakomaa. Kumpa mtoto chakula kabla ya miezi 6 inaweza kupelekea kuongezeka uzito kupita kiasi, kupaliwa, kukosa choo, kutapika, kuharisha, n.k. na hii yote ni hatari kwa afya ya mtoto.

Maziwa yana virutubisho vyote muhimu kwa ukuaji wa mtoto, kuanza kumpa vyakula vigumu ni kumharakisha mtoto.

Na siyo chakula tu, hata maji ya kunywa mtoto anapaswa kuanza kupewa baada ya miezi 6. Yaani, maziwa yanajitosheleza kwa 100%.
 
Nakubaliana kabisa kuwa maziwa ya mama yanavirutubisho vyote anavyohitaji mtoto

Nakubaliana kabisa kuwa maziwa ya mama ni chakula bora na muhimu kwa mtoto mchanga na anatakiwa kunyonyeshwa hadi anapofikisha angalau miaka miwili

Nisichokielewa ni hii kampeni ya miaka ya hivi karibuni ya kuwahimiza kina Mama kutowapa watoto wao kitu chochote isipokuwa maziwa ya mama tu hadi atakapofikisha miezi sita

Kwa umri wetu wengi mlioko jukwaa hili hatukukumbana na hii kampeni kitu kinachomaanisha wazazi wetu walitulisha walivyoona vinafaa sisi kula hata kabla ya miezi sita na tulibaki salama

Hawa wataalamu wa afya wameona madhara gani tuliyoyapata sisi ambayo hawataki hawa watoto wetu wayapate?

Kwanini hii kampeni inahusu watoto wote bila kujali kwamba kila mtoto anazaliwa na utofauti? Ni kweli kuwa mtoto anayezaliwa Kigoma vijijini huko na mama aliyekuwa anashinda shambani toka mimba inatungwa atakuwa sawa na mtoto anayezaliwa Masaki na mama aliyekuwa anashinda kwenye kiyoyozi na kutembelea gari toka mimba inatungwa?

Hawa watoto wanaozaliwa mazingira tofaufi kwanini wapangiwe matumizi sawa ya chakula hadi watakapofikisha miezi sita?

Je, waliofanya tafiti na kuja na haya mapendekezo walifanya tafiti zao Tanzania au yalikuja maandiko tu kutoka kwa wadhamini? Kama yalikuja maandiko, tuna uhakika gani kama mazingira waliyofanyia tafiti zao yanaendana na mazingira yetu?

Karibu tujadili kwa pamoja

Pamoja na yote yaliyoelezwa hapo juu:
20240505_193318.png


Hivyo, kwa mazuri hapo juu ☝, ni vyema suala hili kuzingatiwa.

Ni vyema kuzingatia:
1: Msisitizo kwa mama mjamzito na aliyejifungua anapohudhulia kliniki ni: kupata mlo bora kulingana na mazingira aliyopo kwaajili ya afya yake na mtoto, pia kupata maziwa bora na ya kutosha wakati wa kunyonyesha.

2: Kinyume cha kutokupata maziwa ya mama ni: ukosefu wa kinga, lishe bora na afya njema.

3: Kuna vyakula ambavyo huweza kuanzisha mzio/mfumo wa kinga wa allergy kirahisi kwa mtoto mchanga, hii kutokana na mfumo wake kuanza kujiandaa kwaajili ya mapambano dhidi ya uvamizi. Vyakula hivyo ni kama maziwa ya ng'ombe nk.

4: Kwa wale wenye wazazi walio na maambuki ya ukimwi ni rahisi kupata maambukizi kutoka kwa mama wanapochanganyiwa vyakula vingine ambavyo huenda kuudhuru mfumo wa chakula na baadaye virusi kutoka kwenye maziwa kuingia mwilini kirahisi.

5: Pia, hali ya usasa iliowaingia wamama wengi, kwa kuelewa au kutokuelewa kuliweka pembeni/kutolipa kipaumbele suala la unyonyeshaji watoto wao wachanga kwa sababu mbalimbali.
 
Kabla ya miezi 6 mfumo wa umeng'enyaji wa chakula unakuwa haujakomaa. Kumpa mtoto chakula kabla ya miezi 6 inaweza kupelekea kuongezeka uzito kupita kiasi, kupaliwa, kukosa choo, kutapika, kuharisha, n.k. na hii yote ni hatari kwa afya ya mtoto.

Maziwa yana virutubisho vyote muhimu kwa ukuaji wa mtoto, kuanza kumpa vyakula vigumu ni kumharakisha mtoto.

Na siyo chakula tu, hata maji ya kunywa mtoto anapaswa kuanza kupewa baada ya miezi 6. Yaani, maziwa yanajitosheleza kwa 100%.
Hizi kampeni zilikuwepo wakati wewe unazaliwa? Kama hazikuwepo, hapo ulipo una madhara gani? Kati ya waliozaliwa zamani na hawakupitia mifumo hii na hawa wa sasa ni wa wakati upi walikuwa/wana afya bora na miili yao inastahilimili magonjwa?

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom