KWANINI KUKU WANAKUFA?

KWANINI KUKU WANAKUFA?

Dom boy

Member
Joined
Jan 24, 2018
Posts
99
Reaction score
64
Habari wahenga, naomba ushauri wa kitaalamu kutoka kwenu hasa kwa wale ambao ni wafugaji wa kuku. Nina mradi wa kufuga kuku wa kienyeji, napata changamoto wakati kuku wanapoumwa ugonjwa wa homa ya tumboni, nilishauriwa dawa inayotumika kutibu ni Esb3 30%, lakini ajabu ninapochanganya na dawa inayoitwa Vitalyte baada ya muda mfupi kuku hupoteza uhai, pamoja na kufuata vipimo vilivyopendekezwa lakini bado anapoteza uhai, je nauliza hizi dawa hazitakiwi kuchanganywa katika chombo kimoja au kuna nini kinatokea? naomba ufafanuzi.
 
Wape tetracycline tu ile ya binadamu...habari zote za tumboni zitakaa sawa.
 
wape typhoprim .... Esb3 ni nzuri lakini si kwa ugonjwa mkali wa typhoid ....
 
Ww ni daktari au umetumia akili ya nyuma
Kama wewe unatumiaga akili ya nyuma usifikiri ni kila mtu.

Mimi nimetumia experience kwasababu pia nilikuwa na kuku wanaoharisha kutokana na homa ya matumbo na walikuwa hawali chakula, nilishauriwa niwape OTC 20% au 50% kama walianza muda mrefu.

Hata hiyo Amilyte aliyosema ni vitamin tu wala si dawa moja kwa moja.

Baadae nikapigiwa simu na daktari na mfugaji mwingine kuwa niwape tetracycline vidoge na baada ya muda mfupi sana walirecover.
 
Back
Top Bottom