Kwanini Kikao Cha UKAWA hakina msisimko?

Kwanini Kikao Cha UKAWA hakina msisimko?

Profesa anadai alipwe mshahara wa rais ili amuachie dr nafasi..
 
Hawana scandal za kukamatwa na mabegi ya fedha.

Hawapigani wala kupingana kwa ngumi.

Kiufupi kuna mambo Yanayotifautisha ccmna ukawa na zaidi vha ccmkilikuwa na makundi ndani ya ccm huku ni vyama..sasa kwa mazngira Hayo utataka ufananono gani?

Lakin zaidi mlikusanya watu toka kwenye harmashaur NCHINI huku wamekutana viongozi wakuu wa chama kutakuwaje sawa?

Jaman tatizo la mtanzania huwa anataka anavyoishi yeye kwake na wengine waishi vilevile..hawa hawAcopy na kupaste kama ccm..kina vitu chungu mzima vinavyotofautisha ccm na ukawa conference!!
 
Watanzania na Dunia nzima ilikuwa ikifuatilia kwa karibu saana mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi ya CCM, hali hii imekuwa tofauti kabisa na michakato ya CDM, NCCR,NLD na CUF na hatimaye UKAWA. Bila shaka Watanzania kwa ujumla wao wameulinganisha michakato ya UKAWA kuwa ni sawa na Vikao vya Kamati za HARUSI tu, kwani watu wenyewe wachaaache, tena hata kamera za Wandishi wa habari kutoka Mataifa makubwa Duniani kama ilivyotokea kwa CCM hawapo kwenye Mchakato wa UKAWA. Je kuna haja gani kwa mtu mwenye busara na hekima kuamini kuwa kuna vyama vya upinzani vyenye nguvu Tanzania? au kuna vyama vya kutafutia Ruzuku na umaarufu kama wanavyofanya akina Sugu, Lisu, Mbowe, Mnyika, Wenje n.k ?

Kweli sikio la kufa halisikii dawa.endeleeni kudanganyika na media.R.I.P CCM
 
Nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa siasa za UKAWA, hasa baada ya kuona na kusikia dhamira yao ya kuunganisha nguvu ili kuingoma CCM madarakani.

Lakini nashangazwa na ahadi za uongozo zinazotolewa na wasemaji wa UKAWA, maana tarehe 11 walidai kwamba mgombea URAISI kupita umoja huo atatangazwa mnamo tarehe 14 July 2015, hadi kufikia jana blah blah kibao na hadi kupelekea baadhi ya viongozi waandamizi kutoonekana kwenye mkutano wao.

Sasa leo mnakuja tena mnatuambia kwamba tusubiri siku saba, kama sio ubabaishaji ni nini? Mnapunguza nguvu maana sisi tunasubiri makubwa kutoka kwenu lakini kama nyie hamuelewani semeni moja.

Nawasilisha.
 
kwani yale ma ccm yalikuwa hayabadili ratiba? . kitu kizuri hakitaki haraka
 
Nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa siasa za UKAWA, hasa baada ya kuona na kusikia dhamira yao ya kuunganisha nguvu ili kuingoma CCM madarakani. Lakini nashangazwa na ahadi za uongozo zinazotolewa na wasemaji wa UKAWA, maana tarehe 11 walidai kwamba mgombea URAISI kupita umoja huo atatangazwa mmnamo tarehe 14 July 2015, hadi kufikia jana blah blah kibao na hadi kupelekea baadhi ya viongozi waandamizi kutoonekana kwenye mkutano wao, sasa leo mnakuja tena mnatuambia kwamba tusubiri siku saba, kama sio ubabaishaji ni nini? Mnapunguza nguvu maana sisi tunasubiri makubwa kutoka kwenu lakini kama nyie hamuelewani semeni moja

Nawasilisha.
Acha papala bushlawyer, Makene amatoa Maelezo ambayo yanaeleweka vizuri.Wakati ukawa wanatoa taarifa ya kutangaza wagombea wao kulikuwa tayari na maelewano kwa asilimia kubwa lakini ghfla Sikh moja kabla, time ya uchaguzi imetangaza majimbo mapya 26. Ili ukawa itoe tangazo lake kwa umma ni muhimu kujadiliana na kupata wagombea ktk majimbo mapya pia. Acha papala subiri muda ulioahidiwa
 
Watoto waliokuzwa na pesa za laana utawajua tu. Hakika hiyo laana itawatafuna mpaka kizazi cha tatu watoto wa makada.
Hiyo laana ikosekuku andam wewe unae msujudia MBOWE kama munguwako huna la kushauri wala kukosoa pale ambapo haikustahili! jitambue
 
tuwape muda wajadiliane wakishindwana watatuambia
 
Hawa watu hawafai hata kuwa mabalozi wa nyumba kumi kumi.Uchu wa madaraka na njaa walizonazo ndio zinawaponza.
 
kwani yale ma ccm yalikuwa hayabadili ratiba? . kitu kizuri hakitaki haraka

Ratiba za ccm zilikuwa zinabadilika kwa mtiririko wa matukio na walivyoanza hadi wamemaliza jibu likapatikana, sasa hawa wenzetu vipi? Kila siku kalenda?
 
Msisimko utatoka wapi wakati rais ameshajulikana? Wao cha kufanya wajipange vizuri kwenye safu za ubunge na udiwani.
 
Poleni ukiwa maana baadhi ya viongozi wa umoja wenu huo mmekuwa na utapia demokrasia na uroho wa madaraka, ushauri wangu kwenu jielekezeni kwenye ubunge na udiwani na hii ni kwasababu huo Urais mnaogombania hamtoshinda hata kwa bahati mbaya.
 
Back
Top Bottom