Kwanini iwe vazi jeusi katika msiba?

Kwanini iwe vazi jeusi katika msiba?

Makamee

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2013
Posts
2,029
Reaction score
1,201
Wadau habari zenu!
Nini kinachopelekea watu walio wengi kuvaa vazi jeusi ktk misiba?
Kuna uhusiano gani rangi hiyo na msiba?
 
Shemejiiiiiiiiiiii........
Nichafue mada?
 
Aaah,tayari disko lishavamiwa, unatoka wapi saa hizi shemeji hebu tulia kwanza

Nimekusamehe shemeji.
Sichafui.
Sikuulizi swali nililotaka kukuuliza kuwa madrasa sheikh alikufundisha nini kuhusu vazi jeusi na misiba?
 
Ndo nataka kujua hivi watu wana imani gani kuhusu vazi jeusi na msiba?
1.Ni kuonyesha upendo kwa marehemu?
2.Ni kuonyesha majonzi?
 
pia na mimi mnisaidie kwa rangi nyekundu inamaana gan?
Maana leo tarehe 14 feb wengi wanavaa nyekundu wakidai n rangi ya upendo.
Kwenye bendera ukiikuta nyekundu inaashiria hatari au umwagaj damu.
Hapo ndipo ninapochanganyikiwa.
Nijuzen
 
pia na mimi mnisaidie kwa rangi nyekundu inamaana gan?
Maana leo tarehe 14 feb wengi wanavaa nyekundu wakidai n rangi ya upendo.
Kwenye bendera ukiikuta nyekundu inaashiria hatari au umwagaj damu.
Hapo ndipo ninapochanganyikiwa.
Nijuzen

kutokuelewa ni mwanzo wa kuelewa,ngoja tuwasubiria wadau waje watupe elim juu ya hili swala.
 
Nyeusi=giza,kuzimu
Nyekundu=damu,upendo,hatari
Blue=anga,maji
Kijani=ccm
 
pia na mimi mnisaidie kwa rangi nyekundu inamaana gan?
Maana leo tarehe 14 feb wengi wanavaa nyekundu wakidai n rangi ya upendo.
Kwenye bendera ukiikuta nyekundu inaashiria hatari au umwagaj damu.
Hapo ndipo ninapochanganyikiwa.
Nijuzen

Kwenye bendera ya wapi kama Tanzania sawa, lakini si kila nchi inamaanisha hayo mliyokaririshwa kwenye shule zenu za mwembeni. Sina uhakika kama kule Cuba, etc rangi nyeusi kwenye bendera maana yake rangi za watu, anyway .....
 
Enzi za malkia wa uingereza Queen Victoria ndio walianza kuvaa rangi nyeusi baada ya kifo cha baba yake ni kuonyesha heshima na maombolezo ya msiba. Kwa wahindi na wajapani ni rangi nyeupe ingawa Nao wajapani wanavaa nyeusi kimono siku hizi kwa waislam hakuna rangi ila wanawake hawaruhusiwi kujipamba au kuvaa dhahabu nk kwa hiyo ni utamaduni tu kuvaa nyeusi wakati wa msiba
 
tunaogopa arubadiri,kwani ulishawahi kuona mwanamke wa dini amevaa mabuibui meupe?
mkuu unataka kusema hawa wanawake wanaovaa mabuibui meusi ni misiba kuzimu au giza?na ni kwa nini waume zao huvaa nyeupe tu?mbo na tunaona na wachungaji wakivaa kanzu nyeusi je,hao ni kina nani?
 
Halafu ni kwa nini misiba hasa ya wakristo wanawake wengi huvaa mavazi meupe? Je,huashiria nini?
 
Wadau habari zenu!
Nini kinachopelekea watu walio wengi kuvaa vazi jeusi ktk misiba?
Kuna uhusiano gani rangi hiyo na msiba?
Huu ni utamaduni wa kimagharibi zaidi. Vazi jeusi ni official color, misiba kwa wenzetu huwa ni shughuli rasmi Kama ilivyo kwa official meetings ambazo Mara nyingi kwa wamagharibi vazi rasmi ni black suit. Hii ni kwa tangu zamani ingawa Siku hizi kumekuwa na mabadiliko ambapo hata brown color inafanywa kuwa official. Sasa wabongo tunachofanya ni kuiga tu maana hata kwa wale waumini wa dini zetu zote, tunaagizwa kuvaa vazi la rangi nyeupe. I stand to be corrected endapo sijawa sahihi
 
Kama kuvaa nyeusi ni giza au kuzimu
Kuvaa nyeupe ni amani....
Wamagharibi huvaa nyeusi na Wahindi huvaa nyeupe kwenye misiba yao...sijui tushike lipi.

ndo mana sisi Watanganyika tunavaa chochote kile ndo utamaduni wetu.
 
Huu ni utamaduni wa kimagharibi zaidi. Vazi jeusi ni official color, misiba kwa wenzetu huwa ni shughuli rasmi Kama ilivyo kwa official meetings ambazo Mara nyingi kwa wamagharibi vazi rasmi ni black suit. Hii ni kwa tangu zamani ingawa Siku hizi kumekuwa na mabadiliko ambapo hata brown color inafanywa kuwa official. Sasa wabongo tunachofanya ni kuiga tu maana hata kwa wale waumini wa dini zetu zote, tunaagizwa kuvaa vazi la rangi nyeupe. I stand to be corrected endapo sijawa sahihi

Uko sahihi mwanafyale . Ila naona kuna watu watu wanataka kuchafua uzi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom