Kwanini ilinibidi niache Shule

Kwanini ilinibidi niache Shule

rudi shule tu sio kwa kuandika hv
Wewe unaejua kuandika ipo siku utamtafuta huyu jamaa akupe kazi ya kuwakatia wateja wake risiti.


Watu Kama wewe ndio wananifanyaga nione kusoma sana ni kupotezeana mda tu.
 
"....upumbavu wa kuchonga fanicha.""

Amen.
Kwaherii CEO mwenye uwerevu.

#YNWA
Mbona wanadamu tunakua na wakati mgumu sana mtu akiongea maneno ambayo hayatufurahishi?

Mkuu,usipaniki ni maneno ya kawaida tu...relax...usitilie maanani..maisha mafupi haya kutilia maanani kila ujinga!

Relax mzee!
 
Siku za karibuni naona kuna ujinga mwingi kampeni ya kuimiza watu wakimbie shule...!!?
upuuzi sana!!!
vijana wanatakiwa kuelewa ya kwamba umuhimu wa elimu sio kupata kazi bali kuongeza maarifa ili uweze kutawala mazingira yanayokuzunguka
 
  • Thanks
Reactions: amu
Wasomi bhana....mpo humu ndani mnapiga kelele wakati asilimia kubwa ya mizunguko wa pesa kwenye mikoa yenu, wilaya zenu, kata zenu mpaka mitaa yenu...inaendeshwa na hawa ambao walichagua mapambano ya kibiashara badala ya haya ya kielimu......!!

Mleta mada alichokosa ni utashi katika uandishi tu, lakini ana maisha yake na ana biashara yake ambayo anaimiliki yeye mwenyewe na kaajiri watu...!!! Haya niambieni ni kipi wateja wake wanakikosa kwake ambacho angekua na degree wangekipata!!???

Elimu ni kitu muhimu lakini sio kwamba usipokua na elimu ndo basi maisha yamekushinda.......!!!!!
In fact, wengi tu humu mna degree zenu makabatini hazina mchongo wowote mtaani, wengine mumebahatika kupata ajira kwa degree zenu na diploma zenu lakini maisha kila mkiyazoom hamuelewi yanawapeleka wapi,,,yani mbili haikai wala tatu haisogei.......!!!

Wengine humu mna shuhuda za kutosha za vile wale Jamaa zenu baadhi walio feli form four na LA saba....mkawaacha nyie mkaendelea na vidato huku mkiwa kebehi......sasa mmerudi mtaani mmekuta wao ndio wana own mitaa....yani biashara zao ni kubwa na zimesimama....na wanawatimulia vumbi kwa tairi za gari kila siku, huku wakibaridhi kwenye majumba ya kifahari walioyajenga kipindi wew uko chuo mwaka wa pili unakaribia kumalizi kidgree chako

Kila mtu na alipopangiwa bhana........!!!! Kila mtu na ridhki yake...!!!!!
 
Mleta mda....achana na hizi kelele za watu kutaka ukasome ma logarithms, ma prokaryotic na ma ekaryotic......hata wao hayawasaidii kitu mpaka Leo......cha msingi hapo tafuta namna ujifunze uandishi na uelewa wa lugha mbili...kiswahili na ki English....then jifue katika mahesabu ya kibiashara.....tafuta wazoefu yani wafanya biashara wakubwa zaidi yako wakufundishe namna nzuri zaidi ya kuendesha na kucontrol biashara kwa njia za kitaalamu au niseme za kisasa zaidi.......!!!! Narudia....usiwafate wasomi ambao hata biashara hawana zaidi ya kuisoma kwenye vitabu...tafuta wafanya biashara wenzio walioanzia chini na sasa biashara zao si haba

Ukishaikuza zaidi biashara yako.......tafuta hawa waliosomea degree mbali mbali ambazo zinaweza kuhitajika kwenye biashara yako then wape ajira waaze kutoa jasho kwenye kampuni au biashara yako ili wew ule.!!!!!
Usijali kuhusu kelele zao...we komaa tu....!!!! Watakuja!!!
 
Kila mtu ana riziki yake kwa mapito yake, si kwamba sababu fulani kafanikiwa kwa kufanya hivi na wewe utafanikiwa, au sababu fulani kashindwa basi na wewe utashindwa.

Hata mm ndugu yangu alikuwa ananikatisha tamaa sana kuhusu kusoma kwa story kama zako akitaka tufanye biashara. Nilimpuuza nikasoma, nikaajiriwa, kwa upande wake biashara iliyumba na hakuweza kusimama tena kama mwanzo. Sasa yeye ndo anaomba msaada kwa ajili ya ada za watoto wake. Maisha ni fumbo ajuaye ni Mwenyezi Mungu tu.
But yule mwenye uwezekano wa kumiliki ela ndefu ni yule ambae anaingia risk katika kuwekeza.Ukiwa umeajiriwa huwezi kupanga jambo likatimia sababu umelimitiwa na aliekuajiri na muda ni mchache Umri unaenda.
 
Na hyo ndio dhana iliyopo kwa vijana wengi wa Tz na hata wazazi wengi yn hili tatizo la ajira kwa ss imekuwa ndiyo excuse ya watu kuchukia shule imefika kipindi msomi anaonekana ni adui wa maendeleo nchini wakati sio kweli.

Hyo kujiajiri imekuwa ss ndo wimbo asbh mchn jioni wkt ilipaswa watu wahimizwe waende shule washauriwe wasomee nn au kulingana na upendeleo wake asome nn zen suala la kujiajiri lifuate cz pesa ipo tu hata kama hujaenda shule but tunajaribu kuchanganya ajira na shule kitu ambacho c sawa na tunakwenda kutengeneza taifa la matahira wengi mtaani.

Watoto waachwe waende shule wapate kujitambua hizi changamoto za ajira zitajitatua automatically.
Inatakiwa sasa Elimu kuanzia Chini ichanganue hili ili watoto wasiache shule kwa sababu ya kutafuta ela kwa Sababu ela ipo lakini tatizo linakua pia ni hilo hilo ela.
 
2000 ukamaliza 2015 darasa la kwanza mpaka la 7 ulikua mtaala wa Cambrige nini?
 
Maisha ya hustle ni mazuri na maisha ya elimu ni mazuri pia, lengo ni kufanikiwa kwahiyo uwe una hustle au unasoma usimbuguze mwenzio maana narudia tena lengo ni KUFANIKIWA.
 
mleta mada pole kwa kukatishwa tamaa na wana jf wasomi wataalamu wa mwandiko wazamivu wa kila taaluma.

najua lengo lako lilikiwa zuri kabisa, kutujuza kwamba shule haipo kwa ajili ya kila mtu, lakini bahati mbaya wajinga fulani wamekulisha maneno, uonekane kama unaisiliba hivii.

hasara si kwako bali ni wao na akili zao zilizoandaliwa kukariri, zisijue baada ya shule na vyeti kinachofuata ni kichwa na mikono ya mhusika. leo hii kama kuna mwanachuo hapa aliyeelimika hata kosa kukuelewa, ila wale wenzangu namimi sasa ndio kelele hizii..... yuko chuo na anaota siku moja ni mama/baba fulani boss kwenye kiti anazunguka.

anasahau hata huko anakoota kuna wakati tinaweka vyeti chini na kuanza kuangaliana usoni, nani anaweza kufanya.......


waliokuelewa wacha wakuelewe, muhimu kaza sana, na Mungu mbele.

Sent from my G3226 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom