The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 4,780
- 8,155
----------------------------------
Tanzania ina visima vya gesi asilia kama vile:
👉 Songosongo
👉 Mnazi Bay
Ajabu ni kuwa bado Hatuwezi kuzalisha gesi yetu ya majumbani (Liquified Petroleum Gas). Badala yake tumekuwa waagizaji wakubwa wa gesi kutoka Mataifa kama vile UAE, kenya, India n.k.
MBONA HATUTUMII GESI YETU?
Gesi inayozalishwa hapa Tanzania ni CNG ( Compressed Natural Gas), na sio LPG (Liquified Petroleum Gas).
📌 Compressed Natural Gas na Liquified Petroleum Gas (CNG na LPG ) ni gesi tofauti kabisa kwa muundo wa kemikali, haiwezekani kubadili CNG kuwa LPG kirahisi kwa sababu ni gesi mbili tofauti kabisa.
👉CNG huwa ni Methane (CH4)
👉LPG huwa ni propane ( C3H8)
📌CNG (methane) haiwezi kubadilishwa kuwa LPG (propane/butane) kwa njia ya kawaida au ya kibiashara. Ni gesi mbili tofauti kabisa kwa muundo na matumizi. Gesi ya Tanzania haina mchanganyiko unaoweza kutoa LPG moja kwa moja, na hakuna kiwanda kinachoweza kubadilisha methane kuwa LPG.
KWANI HII GESI TUNAYOTUMIA MAJUMBANI HUTOKANA NA NINI?
Ukweli ni kuwa Mataifa yanayoagiza LPG kama Oryx, Mihan n.k., huchukua hiyo gesi kutoka Nchi zinazochakata mafuta (refineries), Ambapo LPG inapatikana kwa urahisi kama bidhaa ya pembeni (byproduct) wakati wa usindikaji wa mafuta.
Kumbe basi wao huwa tayari wana propane tayari — si methane (CNG) kama ilivyo kwetu Tanzania.
Kwa lugha rahisi kuweza kueleweka ni kuwa, Gesi ya majumbani hutokana na uchakatwaji wa Mafuta asili Na si uchakatwaji wa gesi asili.
LAKINI MBONA TUNA VISIMA VYA MAFUTA HAPA NCHINI?
Ujuwe Tanzania ina visima vya mafuta.
Visima hivi viko hasa maeneo ya
Ziwa Tanganyika (Katavi, Kigoma, na maeneo ya Ziwa Eyasi na Eyasi Wembere Basin).
Lakini ajabu ni kuwa:
👉hata mafuta hatujaanza kuchakata.
👉 Hakuna refinery (kiwanda cha kusafisha mafuta) nchini
Ukiuliza, utaskia mwamba mmoja akijibu:
⏩Kujenga refinery ni gharama kubwa sana. Inahitaji zaidi ya USD milioni 500 hadi bilioni 1, kulingana na ukubwa na teknolojia.
⏩LPG inatokana na usindikaji wa mafuta ya kiwango kikubwa sana.
Unahitaji kiwango kikubwa sana cha mafuta ghafi ili upate hata kiasi kidogo cha LPG.
KWA HIYO TUSEME
TANZANIA HAINA MAFUTA YA KUTOSHA KUJENGA REFINERY?
Unaskia mwamba kutoka kijani akijibu tena na bass nzito nzito:
Tanzania ina mafuta lakini hayatoshi kwa kiwango cha kibiashara cha uzalishaji wa mafuta na bidhaa zake (kama LPG, dizeli, petroli).
Lakini swali linakuja:
Tanzania ina kiwango kidogo cha Mafuta ama ina kiwango kidogo cha nguvu ya utafiti juu ya mafuta?
Nasema hivi kwasababu:
🎯 Taasisi na makampuni ya utafiti wa mafuta nchini Tanzania ni wachache sana, na wengi wao wamepunguza kasi au kujiondoa kabisa kutokana na changamoto nyingi.
🎯Technology inayotumika katika utafiti wa mafuta bado ni duni. TPDC (Tanzania Petroleum Development Corporation) taasisi ya serikali inayosimamia na kuendeleza sekta ya mafuta na gesi nchini haina uwezo wa kifedha wala teknolojia kufanya utafiti wa kina peke yake bila ubia na wawekezaji
Kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa mafuta zaidi nchini, lakini hayajachunguzwa vya kutosha
Eneo la Tanzania lina mabonde ya kijiolojia (basins) ambayo kihistoria huashiria uwepo wa mafuta, kama:
👉Rufiji Basin
👉Selous Basin
👉Mandawa Basin
👉Eyasi-Wembere Basin
👉Ziwa Tanganyika Basin
Haya ni maeneo ambayo kijiolojia yanafanana na maeneo yenye mafuta mengi duniani (kama Sudan, Angola, Nigeria).
✅ Hii inamaanisha: mafuta yanaweza kuwepo kwa wingi, lakini hatujayatafuta vya kutosha.
Kwa hiyo tusemeje hapa?
Naoendekeza tuseme hivi:
📌Tanzania haina uhakika wa kuwa na mafuta kidogo — bali ina kiwango KIDOGO CHA UTAFITI na UCHIMBAJI.
NINI KIFANYIKE?
wachumia Tumbo wa kijani waachie ngazi vijana tushike nchi tufaidike na Rasilimali zetu.. Tafiti zifanyike, Viwanda vifunguliwe, bei za bidhaa zishuke, kodi za kishenzi zifutwe, wanunuzi kutoka nje wapatikane, uchumi upande na mwisho kabisa Tanzania tusiwe wanunuzi kutoka nje, bali tuwe wauzaji kwenda nje.
Tanzania ina visima vya gesi asilia kama vile:
👉 Songosongo
👉 Mnazi Bay
Ajabu ni kuwa bado Hatuwezi kuzalisha gesi yetu ya majumbani (Liquified Petroleum Gas). Badala yake tumekuwa waagizaji wakubwa wa gesi kutoka Mataifa kama vile UAE, kenya, India n.k.
MBONA HATUTUMII GESI YETU?
Gesi inayozalishwa hapa Tanzania ni CNG ( Compressed Natural Gas), na sio LPG (Liquified Petroleum Gas).
📌 Compressed Natural Gas na Liquified Petroleum Gas (CNG na LPG ) ni gesi tofauti kabisa kwa muundo wa kemikali, haiwezekani kubadili CNG kuwa LPG kirahisi kwa sababu ni gesi mbili tofauti kabisa.
👉CNG huwa ni Methane (CH4)
👉LPG huwa ni propane ( C3H8)
📌CNG (methane) haiwezi kubadilishwa kuwa LPG (propane/butane) kwa njia ya kawaida au ya kibiashara. Ni gesi mbili tofauti kabisa kwa muundo na matumizi. Gesi ya Tanzania haina mchanganyiko unaoweza kutoa LPG moja kwa moja, na hakuna kiwanda kinachoweza kubadilisha methane kuwa LPG.
KWANI HII GESI TUNAYOTUMIA MAJUMBANI HUTOKANA NA NINI?
Ukweli ni kuwa Mataifa yanayoagiza LPG kama Oryx, Mihan n.k., huchukua hiyo gesi kutoka Nchi zinazochakata mafuta (refineries), Ambapo LPG inapatikana kwa urahisi kama bidhaa ya pembeni (byproduct) wakati wa usindikaji wa mafuta.
Kumbe basi wao huwa tayari wana propane tayari — si methane (CNG) kama ilivyo kwetu Tanzania.
Kwa lugha rahisi kuweza kueleweka ni kuwa, Gesi ya majumbani hutokana na uchakatwaji wa Mafuta asili Na si uchakatwaji wa gesi asili.
LAKINI MBONA TUNA VISIMA VYA MAFUTA HAPA NCHINI?
Ujuwe Tanzania ina visima vya mafuta.
Visima hivi viko hasa maeneo ya
Ziwa Tanganyika (Katavi, Kigoma, na maeneo ya Ziwa Eyasi na Eyasi Wembere Basin).
Lakini ajabu ni kuwa:
👉hata mafuta hatujaanza kuchakata.
👉 Hakuna refinery (kiwanda cha kusafisha mafuta) nchini
Ukiuliza, utaskia mwamba mmoja akijibu:
⏩Kujenga refinery ni gharama kubwa sana. Inahitaji zaidi ya USD milioni 500 hadi bilioni 1, kulingana na ukubwa na teknolojia.
⏩LPG inatokana na usindikaji wa mafuta ya kiwango kikubwa sana.
Unahitaji kiwango kikubwa sana cha mafuta ghafi ili upate hata kiasi kidogo cha LPG.
KWA HIYO TUSEME
TANZANIA HAINA MAFUTA YA KUTOSHA KUJENGA REFINERY?
Unaskia mwamba kutoka kijani akijibu tena na bass nzito nzito:
Tanzania ina mafuta lakini hayatoshi kwa kiwango cha kibiashara cha uzalishaji wa mafuta na bidhaa zake (kama LPG, dizeli, petroli).
Lakini swali linakuja:
Tanzania ina kiwango kidogo cha Mafuta ama ina kiwango kidogo cha nguvu ya utafiti juu ya mafuta?
Nasema hivi kwasababu:
🎯 Taasisi na makampuni ya utafiti wa mafuta nchini Tanzania ni wachache sana, na wengi wao wamepunguza kasi au kujiondoa kabisa kutokana na changamoto nyingi.
🎯Technology inayotumika katika utafiti wa mafuta bado ni duni. TPDC (Tanzania Petroleum Development Corporation) taasisi ya serikali inayosimamia na kuendeleza sekta ya mafuta na gesi nchini haina uwezo wa kifedha wala teknolojia kufanya utafiti wa kina peke yake bila ubia na wawekezaji
Kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa mafuta zaidi nchini, lakini hayajachunguzwa vya kutosha
Eneo la Tanzania lina mabonde ya kijiolojia (basins) ambayo kihistoria huashiria uwepo wa mafuta, kama:
👉Rufiji Basin
👉Selous Basin
👉Mandawa Basin
👉Eyasi-Wembere Basin
👉Ziwa Tanganyika Basin
Haya ni maeneo ambayo kijiolojia yanafanana na maeneo yenye mafuta mengi duniani (kama Sudan, Angola, Nigeria).
✅ Hii inamaanisha: mafuta yanaweza kuwepo kwa wingi, lakini hatujayatafuta vya kutosha.
Kwa hiyo tusemeje hapa?
Naoendekeza tuseme hivi:
📌Tanzania haina uhakika wa kuwa na mafuta kidogo — bali ina kiwango KIDOGO CHA UTAFITI na UCHIMBAJI.
NINI KIFANYIKE?
wachumia Tumbo wa kijani waachie ngazi vijana tushike nchi tufaidike na Rasilimali zetu.. Tafiti zifanyike, Viwanda vifunguliwe, bei za bidhaa zishuke, kodi za kishenzi zifutwe, wanunuzi kutoka nje wapatikane, uchumi upande na mwisho kabisa Tanzania tusiwe wanunuzi kutoka nje, bali tuwe wauzaji kwenda nje.