scramble
JF-Expert Member
- Nov 29, 2012
- 1,593
- 257
kwanza napenda kuwapongeza UDASA kwa kuandaa kongamano leo katika ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam! Lengo kuu lilikua kujadili amani hapa nchini. Pili nawapongeza wote waliohudhuria ktk kongamano hilo.
Miongoni mwa walio hudhuria ni katibu mkuu wa chadema Dkt. Slaa na Waziri wa Mambo ya ndani Muh. Emanuel Nchimbi. Miongoni mwa waliowasilisha mada ni Dkt. Ayoub Rioba na Prof. Killian. Dkt. Slaa alipopata wasaa wa kuchangia alionesha ukandamizaji wa vyombo vya dola kwa raia. Alimgeukia waziri Nchimbi na kumshambulia kuwa vile anasimamia polisi, hafai kuemo ukumbini. Ni heri akatoka nje. Slaa alifanya hivyo ili kuharibu amani iliyokua inaendelea.
Alitaka kuishawishi hadhira ili ipoteze imani kwa Nchimbi. Slaa alilenga kuishawishi hadhira kumzomea Nchimbi pindi atakapo hutubia. Tofauti na matarajio ya Slaa, Nchimbi alishangiliwa kwa ushirikiano alioutoa kwa kuahidi kufanyia kazi changamoto na matatizo alio yasikia.
Hivyo najiuliza: Je Slaa alichukizwa na uwepo wa Nchimbi? Je Slaa alitaka Ncchimbi azomewe ili apate nini? Je Slaa anapenda viongozi wa serikali wanavyo kwepa kuhudhuria midahalo na makongamano mbambali? hadhani kuwa Nchimbi anastahiki pongezi angalau kwa kuhudhuria? Namalizia kwa kuuliza: kwa kujaribu kuchafua hali ya hewa ukumbini, je Slaa kweli anapenda amani?
Miongoni mwa walio hudhuria ni katibu mkuu wa chadema Dkt. Slaa na Waziri wa Mambo ya ndani Muh. Emanuel Nchimbi. Miongoni mwa waliowasilisha mada ni Dkt. Ayoub Rioba na Prof. Killian. Dkt. Slaa alipopata wasaa wa kuchangia alionesha ukandamizaji wa vyombo vya dola kwa raia. Alimgeukia waziri Nchimbi na kumshambulia kuwa vile anasimamia polisi, hafai kuemo ukumbini. Ni heri akatoka nje. Slaa alifanya hivyo ili kuharibu amani iliyokua inaendelea.
Alitaka kuishawishi hadhira ili ipoteze imani kwa Nchimbi. Slaa alilenga kuishawishi hadhira kumzomea Nchimbi pindi atakapo hutubia. Tofauti na matarajio ya Slaa, Nchimbi alishangiliwa kwa ushirikiano alioutoa kwa kuahidi kufanyia kazi changamoto na matatizo alio yasikia.
Hivyo najiuliza: Je Slaa alichukizwa na uwepo wa Nchimbi? Je Slaa alitaka Ncchimbi azomewe ili apate nini? Je Slaa anapenda viongozi wa serikali wanavyo kwepa kuhudhuria midahalo na makongamano mbambali? hadhani kuwa Nchimbi anastahiki pongezi angalau kwa kuhudhuria? Namalizia kwa kuuliza: kwa kujaribu kuchafua hali ya hewa ukumbini, je Slaa kweli anapenda amani?