Kwanini developers wengi Tanzania wanapenda kutumia PHP?

Kwanini developers wengi Tanzania wanapenda kutumia PHP?

Lodrick Thomas

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
1,339
Reaction score
2,432
Kwanini developers wengi Tanzania wanapenda kutumia PHP?

Habari wana JF!

Ukiangalia websites nyingi hasa za hapa kwetu utaona zimetengezwa kwa kutumia php kwenye server side! Je kwanini developers wengi Tanzania wanapendelea kutumia PHP wakati kuna languages nyingine nyingi tu ambazo wangeweza kutumia kama...

Python(django, flask) inatumika na makampuni makubwa kama Quora, instagram, linkedln, Mozilla, Google(Youtube), IBM

Javascript (Node Js) inatumika na Microsoft, Mozilla

Ruby (RoR) inatumika na Twitter, bloomberg

Na nyingine nyingi tu!!

JF imetengenezwa kwa php, websites zote za serikali zote zimetengenezwa kwa php n.k.

Mgunduzi wa Quora (ambaye pia alikua anafanya kazi facebook) katika moja ya interview zake alisema, kama Facebook ingekua inaanza miaka hii basi wasingetumia PHP!!

Kwanini basi developers wengi Tanzania wanapenda kutumia php na sio python(django, flask, tornado) au ruby (RoR)??
 
Wabongo kwa kukariri! Kila hoja ikiletwa jibu huwa hakuna ubunifu. Really?
Ubunifu na Lugha wapi na wapi?

mbona kwenye mada za tech mara nyingi mtu akiwasema nyinyi developers huwa unakuja juu bila kutoa majibu sahihi?
mtoa mada kasema kuwa kweli tovuti nyingi za tanzania wabunifu wake wametumia php kwa sana na akauliza kwanini hamtumii language nyingine....
wewe ulitakiwa umjibu kuwa hatutumii hizo nyingine sababu 1,2,3.....
 
Python(django, flask) inatumika na makampuni makubwa kama Quora, instagram, linkedln, Mozilla, Google(Youtube), IBM
Javascript (Node Js) inatumika na Microsoft, Mozilla
Ruby (RoR) inatumika na Twitter, bloomberg
Una maana kitu kikiwa kinatumiwa na makampuni makubwa ndio kila mtu atumie? With that Argument, Java EE inakaa wapi hapo?

Mgunduzi wa Quora (ambaye pia alikua anafanya kazi facebook) katika moja ya interview zake alisema, kama Facebook ingekua inaanza miaka hii basi wasingetumia PHP!!
Hayo ni maoni yake wala sio amri kumi! Ukijisikia kuyafuata ruksa lakini yanabaki kuwa maoni ya raia mmoja duniani!

Kwanini basi developers wengi Tanzania wanapenda kutumia php na sio python(django, flask, tornado) au ruby (RoR)??
Ungeeleweka ungesema Kivipi ni jambo baya kutumia PHP badala ya Python au Ruby. PHP ni OO Language sawa na Python na nimetumia zote. Sijawahi kuona umuhimu wa kujifunza Django/Flask na Yii. Naona ni unnecessary redundancy. Chochote Django inafanya naweza kufanya na Yii, so sioni why it is a big deal!

Kusema kwa nini nchi fulani wanatumia teknolojia X na siyo Y kwa maana ya fame then lipo kila mahali na linatokana na background na ecosystem!
 
mbona kwenye mada za tech mara nyingi mtu akiwasema nyinyi developers huwa unakuja juu bila kutoa majibu sahihi?
Sio kila kitu kinapaswa kujibiwa unavyotaka.

mtoa mada kasema kuwa kweli tovuti nyingi za tanzania wabunifu wake wametumia php kwa sana na akauliza kwanini hamtumii language nyingine....
Hilo jibu nililotoa linakwenda kwa nani? Mtoa mada?


wewe ulitakiwa umjibu kuwa hatutumii hizo nyingine sababu 1,2,3.....
Ingekuwa vyema wewe ungejibu hizo 1,2,3....
Maswali ya kitaalamu lazima yaulizwe kitaalamu ili yajibiwe kitaalam!
 
Nafikiri kuna Non PHP websites Tanzania ambazo zimekua Open kufunguliwa kwa end users!
Na hizi zilishawai kuwekwa hapa!

1. TTCL website yake ni ASP.NET
2. TTCL service portal ni Java Servlet
3. Tigo Recharge Portal ASP.NET
4. Vodacom recharge portal ni JSP pia
5. TRA Motor vehicle Tax valuation ni ASP.NET
6....... n.k

hizo ni chache ambazo labda mimi nimekutana nazo na nirahisi ku deduce kutoka kwa nje!
Kwa hiyo observation unaweza ona kuwa web systems nyingi Tanzania zipo kwenye Java na C#

Hizo za serikali unazosema ni PHP labda ni kutoka na age na developers wameamua ku maintain lugha ilotumika mwanzo!

Tukija kwa individual Level PHP is cheap to deploy online unaweza jifunza hizo Djngo sijui vitu gani na ukashindwa au ukahangaika kui deploy online.
Ila a simple google search utapata Host kibao wa PHP na the like.

Nafikiri tusiwe taken up na hizo quotes za hao jamaa kuna reason(S) tuangalie uhalisia wa hapa kwetu!
 
Una maana kitu kikiwa kinatumiwa na makampuni makubwa ndio kila mtu atumie?
No sijamaanisha hivyo! Huo ulikua ni mfano tu kiongozi!
Hayo ni maoni yake wala sio amri kumi! Ukijisikia kuyafuata ruksa lakini yanabaki kuwa maoni ya raia mmoja duniani!
Uko sahihi, lakini ni mmoja wa watu waliokua wanafanya kazi kama top technical leaders,
Swali ni je, kwanini baada ya kuondoka facebook hakuenda kutumia php aliyokua ameizoea kwenye kazi zake akiwa fb?
Kusema kwa nini nchi fulani wanatumia teknolojia X na siyo Y kwa maana ya fame then lipo kila mahali na linatokana na background na ecosystem!
Nilikua tu nataka kujua hasa kutoka kwa wazoefu kama nyie!
 
Nafikiri kuna Non PHP websites Tanzania ambazo zimekua Open kufunguliwa kwa end users!
Na hizi zilishawai kuwekwa hapa!

1. TTCL website yake ni ASP.NET
2. TTCL service portal ni Java Servlet
3. Tigo Recharge Portal ASP.NET
4. Vodacom recharge portal ni JSP pia
5. TRA Motor vehicle Tax valuation ni ASP.NET
6....... n.k

hizo ni chache ambazo labda mimi nimekutana nazo na nirahisi ku deduce kutoka kwa nje!
Kwa hiyo observation unaweza ona kuwa web systems nyingi Tanzania zipo kwenye Java na C#
Nashukuru kwa hii observation yako!!
 
Kwan PHP ina shida gani? Tuanzie hapo. Ni sahihi kufananisha matumizi ya scripting language kwa website kubwa kama Google, Facebook, nk, na website ndogo kama za hapa nchini?

Kwa maoni yangu, japo server side scripting languages zipo nyingi, siyo kweli kwamba kila moja inafaa kwa kila aina ya site. Mfano kulinganisha mahitaji ya language ya forum kama JF na Facebook ni sawa na kulinganisha mlima na kichuguu.
Kwanza bado mnafundisha Pascal au mshaacha??

Niliuliza kutaka tu kujua ndugu!!
 
Back
Top Bottom