Binafsi sina shida na aina yeyote ya muungano itakayoonekana kuwa sawa na pande zote mbili. Iwe serikali moja, mbili hata tatu ni sawa tu. Nina sababu mbili tu za kuupenda na kutojali sana aina ya muungano wetu.
1- Ni muungano pekee ambao bado uu hai hapa Afrika baada ya wengi kushindwa kama wale wa Senegambia.
2- Tupo katika hatua za kuungana (integration) na nchi nyingine za Adrika mashariki kwa hiyo baada ya miaka ishirini toka sasa, muungano wa Tanzania utakua ndani ya muungano mkubwa zaidi wa kifederali Inshallah.