Kwanini CHADEMA ina ushawishi zaidi mitandaoni

Kwanini CHADEMA ina ushawishi zaidi mitandaoni

Screenshot_20250514_184114_Google Play Store.jpg
 
Asilimia kubwa ya watu wanaotumia mitandao wanashabikia cdm.
Asilimia kubwa pia ya watu wasiotumia mitandao pia wanaiunga mkono cdm.
Asilimia kubwa ya watz wanaunga mkono mabadiliko kwani ccm wameonekana matapeli na wanyonyaji
 
Kila siku habari kuu na mijadala iliyopo mtandaoni ikiwepo hapa JF ni kuhusu Chadema kuliko vyama vingine, ni kama ambavyo CCM inapata airtime kubwa kwenye TV na Radio ila kwenye social medial ni Chadema zaidi pamoja na kuwa na kundi kubwa la watu wenye ushawishi na majina wakiwepo wasanii.

Sababu hizi zinawapa Chadema uhai mitandaoni:

1. Chadema ina wanachama na wafuasi wengi vijana, kundi ambalo linatumia sana mitandao ya kijamii kama X, JF, FB na mingine. Wengi ni hodari wa kujieleza, kupambana na hoja, na kushiriki mijadala kwa haraka, kuliko wafuasi wa vyama vingine.

2. Chadema mara nyingi huibua hoja zinazogusa maisha ya kawaida ya watu kama haki za binadamu, elimu, afya, ajira, katiba mpya, na uwajibikaji wa serikali. Hoja hizi hujenga mjadala na kuwavutia watu kushiriki.
Vijana wa vyama vingine wanajificha kujadili ishu zinazoendelea kwenye jamii kwa uwazi.

3. Mara nyingi vyombo vya habari vya kawaida hasa TV, radio na magazetu, vinakosa kutoa nafasi kwa upinzani kwa uwiano sawa, Chadema na wafuasi wake hutumia mitandao kama njia mbadala ya kusambaza taarifa, hotuba, au mikutano yao.
Mkuu huogopi kutukanwa?!!!
Ukiwa jf, unaweza kutoka mbio na kwenda kujificha vunguni mwa kitanda kama ni mwanachama wa Chama kingine. Njoo mtaani Huku Sasa; utachoka na kucheka. Nikijibu swali lako, kwa mtazamo wangu, hii inatokana na ukweli kuwa Wana muda zaidi huko au niseme wamewekeza zaidi huko. Mfano, humu Kila baada ya dakika Moja dada Erythrocyte au Lord Denning wanaanzisha mada ya kujihakilishia kushika nchi🤣🤣🤣
Ukisoma mada zao, kama upo karibu na ikulu unaweza kutoka nje ukachungulia maana unaweza dhani lissu yupo ikulu tayari na mama Samia anatoka mbio na miguu kama alivyownda Nape kuomba msamaha.
 
Mkuu huogopi kutukanwa?!!!
Ukiwa jf, unaweza kutoka mbio na kwenda kujificha vunguni mwa kitanda kama ni mwanachama wa Chama kingine
Unaogopaje maoni ya mtu mwingine kwenye jukwaa huru kama JF! Niko hapa toka 2008 sijwahi umizwa wala kukasirishwa na maoni tofauti na yangu.
 
Hakuna watanzania wengi mtandaoni
Watanzania walioko mitandaoni wako huru zaidi kutoa ukweli wa moyoni.
Hii inamaanisha kuwa hata wasio kwenye mitandao wengi wao wanaipenda CHADEMA.
CCM tubadilishe sera na mfumo wetu wa kuendesha chama.
 
Kila siku habari kuu na mijadala iliyopo mtandaoni ikiwepo hapa JF ni kuhusu Chadema kuliko vyama vingine, ni kama ambavyo CCM inapata airtime kubwa kwenye TV na Radio ila kwenye social medial ni Chadema zaidi pamoja na kuwa na kundi kubwa la watu wenye ushawishi na majina wakiwepo wasanii.

Sababu hizi zinawapa Chadema uhai mitandaoni:

1. Chadema ina wanachama na wafuasi wengi vijana, kundi ambalo linatumia sana mitandao ya kijamii kama X, JF, FB na mingine. Wengi ni hodari wa kujieleza, kupambana na hoja, na kushiriki mijadala kwa haraka, kuliko wafuasi wa vyama vingine.

2. Chadema mara nyingi huibua hoja zinazogusa maisha ya kawaida ya watu kama haki za binadamu, elimu, afya, ajira, katiba mpya, na uwajibikaji wa serikali. Hoja hizi hujenga mjadala na kuwavutia watu kushiriki.
Vijana wa vyama vingine wanajificha kujadili ishu zinazoendelea kwenye jamii kwa uwazi.

3. Mara nyingi vyombo vya habari vya kawaida hasa TV, radio na magazetu, vinakosa kutoa nafasi kwa upinzani kwa uwiano sawa, Chadema na wafuasi wake hutumia mitandao kama njia mbadala ya kusambaza taarifa, hotuba, au mikutano yao.
Hoja zako ni kweli tupu
 
Utekaji, uonevu na unyanyasaji unaofanywa na watawala ndio chanzo kikuu cha nguvu kubwa kubaki mitandaoni.

Siasa za wazi zenye usawa kujinadi Kwa wananchi CCM haiwezi kutoboa ndio maana Kwa kuliona hili wamewekeza kwenye uhalamia wa kuumiza watu.
Watu wengi kwasababu ya uoga na kujali maisha yao wameamua kubaki mitandaoni.

Ni suala la muda tu, watu uoga utawaisha na ikifikia hii siku kama CCM hawatobadili mbinu kuna hatari yakutokea machafuko mabaya sana, CCM itambue tu hakuna uonevu wa milele na siasa ni science sio mabavu.
 
Mitandaoni ndio kuna jamii ya wasomi zaidi...utafiti wa TWAWEZA ulipata kurhibitisha kwamba CHADEMA inapendwa zaidi na wasomi kuliko ilivyo CCM.
 
Back
Top Bottom