Msolo
JF-Expert Member
- Oct 19, 2008
- 3,829
- 5,269
Kila siku habari kuu na mijadala iliyopo mtandaoni ikiwepo hapa JF ni kuhusu Chadema kuliko vyama vingine, ni kama ambavyo CCM inapata airtime kubwa kwenye TV na Radio ila kwenye social medial ni Chadema zaidi pamoja na kuwa na kundi kubwa la watu wenye ushawishi na majina wakiwepo wasanii.
Sababu hizi zinawapa Chadema uhai mitandaoni:
1. Chadema ina wanachama na wafuasi wengi vijana, kundi ambalo linatumia sana mitandao ya kijamii kama X, JF, FB na mingine. Wengi ni hodari wa kujieleza, kupambana na hoja, na kushiriki mijadala kwa haraka, kuliko wafuasi wa vyama vingine.
2. Chadema mara nyingi huibua hoja zinazogusa maisha ya kawaida ya watu kama haki za binadamu, elimu, afya, ajira, katiba mpya, na uwajibikaji wa serikali. Hoja hizi hujenga mjadala na kuwavutia watu kushiriki.
Vijana wa vyama vingine wanajificha kujadili ishu zinazoendelea kwenye jamii kwa uwazi.
3. Mara nyingi vyombo vya habari vya kawaida hasa TV, radio na magazetu, vinakosa kutoa nafasi kwa upinzani kwa uwiano sawa, Chadema na wafuasi wake hutumia mitandao kama njia mbadala ya kusambaza taarifa, hotuba, au mikutano yao.
Sababu hizi zinawapa Chadema uhai mitandaoni:
1. Chadema ina wanachama na wafuasi wengi vijana, kundi ambalo linatumia sana mitandao ya kijamii kama X, JF, FB na mingine. Wengi ni hodari wa kujieleza, kupambana na hoja, na kushiriki mijadala kwa haraka, kuliko wafuasi wa vyama vingine.
2. Chadema mara nyingi huibua hoja zinazogusa maisha ya kawaida ya watu kama haki za binadamu, elimu, afya, ajira, katiba mpya, na uwajibikaji wa serikali. Hoja hizi hujenga mjadala na kuwavutia watu kushiriki.
Vijana wa vyama vingine wanajificha kujadili ishu zinazoendelea kwenye jamii kwa uwazi.
3. Mara nyingi vyombo vya habari vya kawaida hasa TV, radio na magazetu, vinakosa kutoa nafasi kwa upinzani kwa uwiano sawa, Chadema na wafuasi wake hutumia mitandao kama njia mbadala ya kusambaza taarifa, hotuba, au mikutano yao.