Kwanini ccm wachezee elimu kiasi hki???

NGONYA NM

Member
Jan 8, 2012
39
15
Inasikitisha kuona Elimu ya Tanzania inachezewa na wanasiasa wa ccm, nikweli wanasiasa ni wadau kwenye maswala ya elimu lkn hila lakuchezea elimu ya vijana we2 tunalipinga kwa nguvu zote. Walipogundua kukosa kura kwenye uchaguz mkuu Maghembe akatangaza kuondoa ada ya mitihan kwa elimu ya secondary mwaka 1 baada yakujitangaza washndi wa uchaguzi wazir mlugo anatangaza kurudisha ada ya mitihani. Je 2014 watafuta tena ili kupata kura 2015?? Mbaya zaidi ni hli la kufuta mtihani wa fom 2 ulikuwa mtihan muhmu sana kwa matokeo mazuri ya kidato cha nne wakahamu kufuta ili washnde uchaguzi matokeo yake asilimi 80 yawanafunzi waliopita bila kuchujwa fom 2 wamefeli mtihan wa fom 4 je tuseme hawa walaghai wa ccm hawakujua yatatokea matokeo mabovu? Eti wanajidai wamerudish mtihani baada yautafiti kubaini kufel kwa fom 4 nikutokana nakuondolewa kwa mtihan wa fom 2! Hamkulijua hlo ACHENI KUCHEZA NA ELIMU YA VIJANA WE2 Wana jf nawasilisha!
 
Sasa hivi wanadai wamefanya utafiti na kugundua umuhimu wa mtihani wa kidato cha 2!Swali la kujiuliza:Je wakati wanaufuta hawakufanya utafiti?Siasa inaiumiza hii nchi ki ukweli.
 
Kwenye suala la elimu kila waziri wa elimu huibuka na lake kwa wakati wake. Yupo aliyepiga marufuku michezo mashuleni. Akaibuka mwingine akafuta masomo ya biashara sekondari akidai kuwa watayakuta hayo masomo vyuoni! Yaani sijui huwa wanawaza nini wakati wanafanya maamuzi kama hayo!
 
Mnashangaa nini? uongozi wa tz ni kila mtu kuongoza jinsi anavyojua. hakuna sera ya elimu tz. sera iliyopo iko too general. hivyo kila anayekuja anatafsiri anavyojua.
 
Elimu ya tanzania chini ya serikali ya ccm inatolewa kama bidhaa za kichina.
 
hivi matokeo ya form mwakaa huu watatangaza lini? Tegemea madudu kwa kasi zaidi
 
Tuliwahi kulijadili hili hapa na ninakumbuka niliwahi andika 'tuache kusiasisha elimu' elimu ni sekta pekee ambayo wafanya maamuzi wanapaswa kuwa objective na maslahi yao yote waliyonayo yalenge kunufaisha taifa na si nafasi zao za kisiasa (tunajua wanashika nafasi hizi kunufaisha matumbo na viuno vyao- wengi wao).

Jiulize, unarudisha mtihani huu, sawa, itawezekana vp mitihani hii ikafanyika mwaka huu, je wameangalia wanafuzi wamesoma nini kipindi hiki, suala la waalimu na vifaa limeangaliwa kwa shule zote za sekondari?

Sitaki kuwa mtabiri, uhalisia unajieleza bayana, elimu yetu inachezwa sana, matokeo ya kidato cha nne miaka mitatu iliyopita yanajieleza kuwa, kuna kundi linaandaliwa kunyonywa hadi damu.

Wakati wao wakichezea eliu yetu, wanawakimbiza watoto wao kusoma elimu bora nje ya nchi ili wakija waweze kuwa na mbinu bora za kuajiiriwa na kujiajiri ilhali wengi tunabaki na bora elimu ili tuweze kutabasamu pindi wanapopita na kutumwagia pilau na wanapotuambia tupige mbizi.
Sekta zote ni muhimu, kuweka siasa za ubinafsi kwenye elimu na tiba ni upumbavu unaoweza kueleweka kwa watanzania tu. Inakera sana, naweza kuweka swali hapa,

Hivi tunapoenda kwenye uchaguzi, huwa tunajiuliza nini tunachagua, tuna viapumbele ambavyo tunataka tunaowapatia dhamani ya kutuongoza watimize au ni mapenzi mfu
 
Back
Top Bottom