Kwanini Bongo Mchango wa Maprofessor na Ma-PHD holders hauonekani?

mkulungwa

Member
Feb 20, 2011
12
1
Hello Wazee kwenye Jukwaa,
Naanza kwa kuwasalim wote. Last week nilikuta mjadala kuhusu kiwango cha elimu kati ya UDSM graduates na vyuo vingine. Mjadala ulikuwa mkali mno but kwangu ulinipelekea kufikiria mchango wa maprofs na PHD holders na other graduates kwenye jamii.

Hivi wanajamii tunaridhishwa na mchango wao or nao ni mavuvuzela tu? sometimes kumekuwa na kauli kwamba wanasomea kupanda vyeo tu na wakimaliza shule husahau kila kitu.. sina hakika.

wadau mwasemaje kuhusu hili? mimi nimetoa mtaani, wenye data watolee maelezo zaidi.

Nawasilisha!!:mullet:
 
Wengi kama c wote ni wabangaizaji wa life shida yao sana2 wana-aspire kumiliki nyumba, gari totoz na uhakika wa ulabu. Nenda mitaa ya Survey utathibitisha ninayosema.
 
Wengi kama c wote ni wabangaizaji wa life shida yao sana2 wana-aspire kumiliki nyumba, gari totoz na uhakika wa ulabu. Nenda mitaa ya Survey, Kambarage kwa SUA na Changarawe utathibitisha ninayosema.
 
Mchango mkubwa wa Maprofesa na PHD holders uko vyuoni. Wanafundisha, Wanatafiti, wanaandika na kutoa ushauri. Jamii inawategemea kwa ushauri nasaha. Lakini pia usisahau kwamba changamoto kubwa kwenye mambo ya kisheria, kisiasa, kiuchumi na kitaaluma kwa ujumla zinatoka kwa hao hao. Wanakumbana na vikwazo vingi ikiwa ni pamoja na jamii kubwa ya Watanzania wasiojua kusoma (illiteracy at all levels).
 
Mwana-JF,
Ni kweli kabisa na ni aibu kwa jamii yetu. Sababu kubwa wasomi na wasio wasomi mradi una kipato hatujui kutumia MUDA (Time Management). Muda mwingi kwenye mabaa na Klabu za vileo badala ya kusoma na kujadiliana na kufanya ugunduzi mpya. Wengi tukitoka kazini (saa 10.00 mpaka 4.00 au 6.00 usiku. Kesho yake asubuhi kazini ana mzigo kichwani na haja jiandaa na ya ofisini - awe Dr. au prof. chuo kikuu au mfanyabiashara wa fedha nyingi. Saa 4.00 atatoka kwenda kwenye supu au mkutanoni. Huo ndio mzunguko wa maisha ya msomi wa Tz. Je, atapata muda wapi wa kufikiri na kufanya ugunduzi? Fikiri sana! mpaka leo hatuna kiwanda cha "office au safety pins" wala "tooth peak" wachilia mbali spea za "power tiller". Tumwe waachia "manchinga" na wafanyabiashara wadogo kufanya ubunifu. Wasomi wamekwenda "Bungeni" kuzitafuta za haraka haraka ili waendeleze viti virefu! Aiubu! Pombe zithibitiwe jamani! Kipi hatari katika taifa - Pombe au Sigara? Leo sigara inapigiwa kelele kuliko pombe. Ni kitu gani hicho? Tafakari sana mwana JF.
 
Hao maprofs na phd holders wanaona kama wamemaliza kila kitu so uwajibikaji unakua wa kujisikia but si ujanja watumie elimu yao kuvumbua mipangilio kimaisha.akina Newton,Socrates au Bill Gates c maprofs ona michango yao
 
Kama ambavyo watanzania wengi tunasoma kwa ajili ya kupata vyeti na kupata kazi, ndivyo walivyo Maprof na wale waliopata PhDs! Wengi wamefikia level hiyo wakiwinda promotion na kujulikana kwamba wana elimu kubwa na si mahitaji ya ufanisi katika shughuli walizokuwa wakizifanya. Utashangaa mtu kapata digrii yake ya kwanza leo, kesho anasoma digrii ya pili mara ana phd. Kazi hajawahi kufanya hata siku moja, changamoto za kazi hazijui, sasa atabuni kitu gani cha kusaidia jamii wakati hajui mazingira ya kazi yakoje? Atakachofanya ni kuangalia jamii inafanya shughuli gani na yeye ataiboresha kidogo kwa uprof wake na huo ndio ubunifu wake! Angalia baa nzuri au mgahawa mzuri, utaambiwa wa prof fulani au dr fulani!

Huo ndio mchango wao na hilo ndilo tatizo la kusoma bila malengo ya kimahitaji!
 
Kama ambavyo watanzania wengi tunasoma kwa ajili ya kupata vyeti na kupata kazi, ndivyo walivyo Maprof na wale waliopata PhDs! Wengi wamefikia level hiyo wakiwinda promotion na kujulikana kwamba wana elimu kubwa na si mahitaji ya ufanisi katika shughuli walizokuwa wakizifanya. Utashangaa mtu kapata digrii yake ya kwanza leo, kesho anasoma digrii ya pili mara ana phd. Kazi hajawahi kufanya hata siku moja, changamoto za kazi hazijui, sasa atabuni kitu gani cha kusaidia jamii wakati hajui mazingira ya kazi yakoje? Atakachofanya ni kuangalia jamii inafanya shughuli gani na yeye ataiboresha kidogo kwa uprof wake na huo ndio ubunifu wake! Angalia baa nzuri au mgahawa mzuri, utaambiwa wa prof fulani au dr fulani! Huo ndio mchango wao na hilo ndilo tatizo la kusoma bila malengo ya kimahitaji!
Usemalo ndo ukweli wa wabongo na tatizo limekwenda mbali zaidi hadi kwa kizazi cha sasa.
 
Hao maprofs na phd holders wanaona kama wamemaliza kila kitu so uwajibikaji unakua wa kujisikia but si ujanja watumie elimu yao kuvumbua mipangilio kimaisha.akina Newton,Socrates au Bill Gates c maprofs ona michango yao
Tatizo si maprofessor au Ph.Ds. Tatizo ni jamii ambayo haijajipanga vizuri kuwahamasisha watu wake kuwa wabunifu, wagunduzi na kuthamini taaluma. Katika nchi zilizoendelea vyuo vikuu siyo taasisi za kufundisha peke yake bali ni mahali pa kutafiti na kugundua maarifa au teknolojia mpya. Inventions nyingi ambazo baadae zinakuja kuwa na matumizi ya kila siku (innovations) nyingi zinaanzia kwenye tafiti katika vyuo vikuu. Hapa kwetu sivyo ilivyo. Vyuo vikuu ni shule tu. Hata pale ambapo utafiti/ugunduzi unafanyika (kwa mfano pale CoET ya UDSM) matokeo yake huyaoni yakiwekwa katika matumizi ya kupunguza shida/changamoto zinazoikabili jamii. Watafiti wanapata Ph.D zao au wanapata promotion na kuwa maProf. yanabaki hapo kwenye makaratasi. Hata kuitangazia jamii ili iweze kujua nini wanafanya ili wajasiriamali watumie hayo maarifa mapya haifanyiki. Kwa nini? Labda ni kwa sababu biashara za baa, n.k. zina returns nzuri na mapema zaidi kuliko hizo za kitaaluma na kitafiti. Kama kuna maprofesa na wasomi wengine hapa JF watupe upande wao wa sarafu.
 
hivii UDSM,MZUMBE,SUA,OUT,IFM,kuna ugunduziii wowote ambao unatumika kwa manufaa ya jamiiiii?????
 
Wengi kama c wote ni wabangaizaji wa life shida yao sana2 wana-aspire kumiliki nyumba, gari totoz na uhakika wa ulabu. Nenda mitaa ya Survey, Kambarage kwa SUA na Changarawe utathibitisha ninayosema.

Umenikumbusha mbabali sana na hayo maeneo ----- Survey, Kambarage - cku imechoka sana lkn na Changarawe a.k.a Cheng'
 
Back
Top Bottom