Kwanini baada ya kuoana tumeachana?

Kwanini baada ya kuoana tumeachana?

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Habari za jioni?

Ntumai mpo poa .....

Kama kawaida huwa siji na hoja hapa bila kuifanyia utafiti angalau kidogo na kupata mwanga,niliwahi kusikia na kusoma sana kwenye majarida na magazeti na zaidi nimeshuhudia watu wakiniambi jambo hili kuwa,kama kuna watu waliishi kwenye mahusiano kwa muda mrefu na kupendana na kuishi kwa amani kama mke na mume lakini hakukuwa na ndoa yaani yale makaratasi na ikaja wakaoana hupita muda mfupi na wanaachana

Nimekutana ma mahusiano ya aina hii ma 5 yaani watu walikuwa hawajaoana na waliishi maisha ya furaha kabisa lakini baada tu ya kuoana walitengana

Nilijaribu kuwauliza sababu hakuna aliyenipa sababu ya kushikika lakini kila mtu alikuwa anamtupia lawama mwenzake kuwa ndiuo alisababisha ndoa kufa,ukiwauliza kama ni mwenzake ni kitu gani kiliwafanya wasiachane wakati ule hawajafunga ndoa kunakuwa hakuna jibu

Hadi sasa sijapata jibu lakini kitu ambacho nina uhakika nacho kuna idadi kubwa sana ya mahusiano ambayo yamechukua muda mrefu nayalipokuja kubadilika na kuwa ndoa watu hawa ambao waliishi kwa amani muda mrefu sana wanaachana

Inawezekana kuna mtu ambae anaweza kuwa ana jibu ya hili naomba anijibu .....!!
 
^^
Imperfect matches... Unakutana na mtu, unavutika, anakulima masharti, unakubali, unaingia kwenye ndoa, leo hili, kesho lile, kesho kutwa vile, mnasuluhishwa, mnashauriwa, Lakini njia ni kutengana!
Yote ni imperfect matches!
^^
 
Marriage(ndoa) is the last stage of relationship ,what do you expect after reaching peak(rise)?sensibly fall ,binadamu we are damn so creative you see baada ya ndoa hamna kitu kinafuatia ,ila kwenye uchumba wanakua bado hawajafikia hatua ya mwisho
Hili ni wazo langu binafsi ,katibu mwenezi kutoka teamB
 
Kwanini watu wa aina hii huwa ni wakristo tu?

Yani mnawekana kinyumba kama baba na mama huku hamjawa verified, inatokea mara nyingi kwa dini hii tu,

Nani kahalisha huu utamaduni?
 
Namfahamu jamaa yetu mmoja alimpa binti mmoja (jirani yake) ujauzito... then wakaamua kuishi pamoja bila kufunga ndoa (kuirasimisha) wakazaa na mtoto wa pili. Baadae wakashauriwa wakafunge ndoa. Wamefunga ndoa Jumapili tukala na kunywa wiki ilioanza kesho yake ikafika ijumaa wakakorofishana (sikumbuki kisa ni nini) Mtoto wa kwanza alikua darasa la kwanza hadi leo yupo la saba HAWAJAWAHI KURUDIANA toka siku ile. Kila mmoja hataki na kila mmoja anasema mwenzake hawezi kuoa/olewa as far as ndoa ya kikristo is concerned. (tuseme ndoa rasmi ilidumu kwa siku nne ne nusu). Matokeo yake sasa watoto wamekosa mlezi ya wazazi.

Nami navutiwa kujua ni nini kinachotokea apa? ni either kiburi cha kuwa kwa kuwa tumefunga ndoa hawezi tena kuniacha au ni nini? Maana pengine alikua akiishi akitengeneza mazingira ya kuolewa rasmi ila baadae yakishatimia malengo ndio mwisho wa ndoa au ni nini? Kwani kuna ulazima gani wa ndoa kama haupo tayari?

Nafikiri ntajifunza kitu kipya apa.
 
Mkuu sana Eiyer binafsi nimeishi katika nadharia hii, unakuta mpo kwenye mahusiano ya muda mrefu na yenye malengo na ndoto nyingi nyingi za badae ila tragedy inatokea pale mnapotaka kumaanisha kwa kufunga ndoa! Sijui ni sababu gani hasa ila mara nyingi nadhani inatokea kwa sababu it happen to be!
 
Kwanini watu wa aina hii huwa ni wakristo tu?

Yani mnawekana kinyumba kama baba na mama huku hamjawa verified, inatokea mara nyingi kwa dini hii tu,

Nani kahalisha huu utamaduni?
Kwani pacha miss neddy tulishakula mpunga?lol
 
Last edited by a moderator:
^^
Imperfect matches... Unakutana na mtu, unavutika, anakulima masharti, unakubali, unaingia kwenye ndoa, leo hili, kesho lile, kesho kutwa vile, mnasuluhishwa, mnashauriwa, Lakini njia ni kutengana!
Yote ni imperfect matches!
^^

Na huo muda mliokaa kabla ya ndoa haya masharti hayakuwepo?
 
Labda kwa sababu kabla ya ndoa kila mtu alikuwa anajiona hana wajibu na majukumu mazito kwa mwenzie, labda kila mtu alikuwa anapuuzia maudhi madogo madogo na hata makubwa kwa kujipa moyo anaweza kumuacha mwenzie muda wowote...na akawa free

Baada ya ndoa labda ndo anastuka kwamba huyo ndo wake, tena milele, ana wajibu juu yake.....hapa ndo mtu anaanza kuyapa uzito hata yale yalokuwa hayampi shida na alokuwa anayadharau....
 
Marriage(ndoa) is the last stage of relationship ,what do you expect after reaching peak(rise)?sensibly fall ,binadamu we are damn so creative you see baada ya ndoa hamna kitu kinafuatia ,ila kwenye uchumba wanakua bado hawajafikia hatua ya mwisho
Hili ni wazo langu binafsi ,katibu mwenezi kutoka teamB

Kwahiyo mkuu raha ya safari sio kufika unakoenda bali ni kabla ya kufika?
 
Kwanini watu wa aina hii huwa ni wakristo tu?

Yani mnawekana kinyumba kama baba na mama huku hamjawa verified, inatokea mara nyingi kwa dini hii tu,

Nani kahalisha huu utamaduni?

Hii nadhani inatokana na masharti ya ndoa kwenye Ukristo!
 
Na huo muda mliokaa kabla ya ndoa haya masharti hayakuwepo?

^^
Kuna tofauti ya maisha kabla ya ndoa, ndani, na baada ya ndoa. Kabla ya ndoa ni kukubaliana ili usipoteze penzi, ndani ya ndoa ni sheria, na baada ya ndoa ni kanuni ya majuto na lawama.
^^
 
^^
Kuna tofauti ya maisha kabla ya ndoa, ndani, na baada ya ndoa. Kabla ya ndoa ni kukubaliana ili usipoteze penzi, ndani ya ndoa ni sheria, na baada ya ndoa ni kanuni ya majuto na lawama.
^^

So ushauri ni kuoana na mtu ambaye hamjawahi kukaa kwenye mahusiano ya muda mrefu kabla ya ndoa au?
 
Namfahamu jamaa yetu mmoja alimpa binti mmoja (jirani yake) ujauzito... then wakaamua kuishi pamoja bila kufunga ndoa (kuirasimisha) wakazaa na mtoto wa pili. Baadae wakashauriwa wakafunge ndoa. Wamefunga ndoa Jumapili tukala na kunywa wiki ilioanza kesho yake ikafika ijumaa wakakorofishana (sikumbuki kisa ni nini) Mtoto wa kwanza alikua darasa la kwanza hadi leo yupo la saba HAWAJAWAHI KURUDIANA toka siku ile. Kila mmoja hataki na kila mmoja anasema mwenzake hawezi kuoa/olewa as far as ndoa ya kikristo is concerned. (tuseme ndoa rasmi ilidumu kwa siku nne ne nusu). Matokeo yake sasa watoto wamekosa mlezi ya wazazi.

Nami navutiwa kujua ni nini kinachotokea apa? ni either kiburi cha kuwa kwa kuwa tumefunga ndoa hawezi tena kuniacha au ni nini? Maana pengine alikua akiishi akitengeneza mazingira ya kuolewa rasmi ila baadae yakishatimia malengo ndio mwisho wa ndoa au ni nini? Kwani kuna ulazima gani wa ndoa kama haupo tayari?

Nafikiri ntajifunza kitu kipya apa.

Mkuu ngoja nibalance Gender hapo .....

Uliposema ni kutengeneza mazingira ya kuolewa basi ni vyema tukasema kuna wanaotengeneza mazingira ya kuwafanya wanawake wao wawaoe halafu baada ya hapo tu kiburi kinaanza!
 
Mkuu sana Eiyer binafsi nimeishi katika nadharia hii, unakuta mpo kwenye mahusiano ya muda mrefu na yenye malengo na ndoto nyingi nyingi za badae ila tragedy inatokea pale mnapotaka kumaanisha kwa kufunga ndoa! Sijui ni sababu gani hasa ila mara nyingi nadhani inatokea kwa sababu it happen to be!

Mkuu sidhani kama hakuna sababu ....

Nadhani ipo ngoja tusubirie majibu yatapatikana tu!
 
Labda kwa sababu kabla ya ndoa kila mtu alikuwa anajiona hana wajibu na majukumu mazito kwa mwenzie, labda kila mtu alikuwa anapuuzia maudhi madogo madogo na hata makubwa kwa kujipa moyo anaweza kumuacha mwenzie muda wowote...na akawa free

Baada ya ndoa labda ndo anastuka kwamba huyo ndo wake, tena milele, ana wajibu juu yake.....hapa ndo mtu anaanza kuyapa uzito hata yale yalokuwa hayampi shida na alokuwa anayadharau....

Mkuu sidhani ...

Kwenye mahusiano ndio mahali ambapo unamuangalia mwenzako kama anakufaa,sasa mnapoingia kwenye ndoa hapo ni kufa na kuzikana na hapo ndipo ambapo uvumilivu unahitajika

Inakuwaje mmeishi kwa miaka mi 5 halafu mkisha funga ndoa tu hata mwaka hauishi mnakuwa mmeachana?
 
Back
Top Bottom