Kwanini amtongoze rafiki yangu

G70

JF-Expert Member
Jul 13, 2022
1,109
2,252
Kuna wanaume wenye tabia kama ya huyu wa kwangu?

Siku nilipomfumania akipiga nyeto alijitetea kuwa alizidiwa na kujikuta akifanya hivyo. Nilimtaka aache mara moja hiyo tabia na ikiwa hawezi basi awe ananiita nimhudumie kila anapozidiwa na si kupiga nyeto. Tuliyamaliza na akasema ameacha kabisa hiyo tabia.

Baada ya kustaajabu ya Musa, sasa nimeanza kuyaona ya firauni.
Huyu shemeji yenu kaweka kambi kwa shoga angu Pamela, ameanza kumtongoza kimapenzi, kila siku yupo kiguu na njia kwa kuwasiliana na kwenda kwa Pamela kuwasilisha akitakacho, kesha toa ahadi ya kumkodishia fremu ya biashara na mtaji juu wa kumuanzishia salon iwapo atamkubalia ombi lake.

My shosti Pamela tumetoka naye mbali sana hivyo kwa kuniheshimu amemsikiliza na kumpotezea tu huyo mwanaume.

Pamela sio mwanamke malaya, ana mtu wake mmoja tu ampendaye kiukweli, hivyo alipopata ugeni usio na kikomo wenye viashiria vyote vya kushawishiwa kuzini na my man aliamua kufanya kitu.

My shosti Pamela alinipa info zote kuhusu mwanaume wangu anayo wasilisha ombi lake la kutaka afanye naye mapenzi na kutimiza ahadi ya mtaji aliouahidi.

Baada ya kupata info zote nilijiuliza sana kuhusu huyu mwanaume inakuwaje anatamani kutoka na rafiki yangu tena ni mwanamke wa mtu?

Mwanamke wake nipo na huwa namuachia yote, hatulalagi mzungu wa nne, simbaniagi kitu kabisa, iweje akitoka tu home anaenda kumtongoza shoga angu?

Yaani sikuweza kumuelewa kabisa huyu mwanaume anatafuta nini kwa shoga angu wakati mie nipo.

Ninahisi kuwa hajakomea kumtongoza Pamela tu bali kuna foleni ya wadada wengi huko kawapanga huko mtaani. Hivi hawa wanaume wenye tabia hizi tuwaite mbwa au fisi?

Nimetulia kama sijui kitu kinachoendelea kwa huyu mwanaume na tabia yake mbovu, nina zoom tu Ila baadae nitachukua uamuzi wa kusuka ama kunyoa. Nitachukua uamuzi baada ya kupata uhakika kwamba hanifai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom