msani
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 1,801
- 1,191
mkuu bujibuji ukinitaka radhi nitakukubalia,sie hatuko hivyo,tunajua mistariMwisho wa yote ni Wakurya, wakiwa wanatongoza utawasikia wakisema " umeorewa au bado unapigapiga umaraya?"
mkuu bujibuji ukinitaka radhi nitakukubalia,sie hatuko hivyo,tunajua mistariMwisho wa yote ni Wakurya, wakiwa wanatongoza utawasikia wakisema " umeorewa au bado unapigapiga umaraya?"
Niliona facebook some people from Congo write NKNC (NaKufa Na Cheko, translated from french for "mort de rire"). Maybe TZ needs to come with its own thing?(Hivi 'LOL' kiswahili utasemaje?)
Body language ndo lugha ya mapenzi))
kasumba imetumeza!
yatajeni hayo maneno hapa km ambavyo mnatoa hiyo mifano ya lugha ya kiingereza
hii inaonesha wazi kuwa hata wanaoshadadia lugha ya kiswahili kwa matumizi yake katika mapenzi nao wamemezwa na hiyo inazoitwa 'lugha ya malkia'
Mwandani,wa ubani,mpenzi ,mahabuba,wa ubavu,la azizi
Mume wangu,bwanangu,asali wa moyo
Tatizo kuna maombi mengine ukitumia lugha ya kiswahili mbele ya watu ni matusi, mfano unaweza kuomba "K" hata mbele za watu kwa kusema "Let us make love tonight".
Je unaweza kuomba "K" mbele za watu kwa kiswahili?
Sabalkheri mpenzi, pambo lenye uwidadi
Ewe tunu mwenye enzi, tawasufi 'so idadi
Shaufu si mwanagenzi, wa kunitia midadi
Stahabu zako malezi, mwingi wa heshima jadi
Zumaridi lako jaha, hata uvikwe hijabu
Moyoni naona raha, kupita mali dhahabu
Sitoweza kukataa, kuwa na wewe thawabu
Chakula n'onapo njaa, la jibu langu jawabu
Mkirimu hakuhini, aliumba kwa sahala
Hakufanya uhaini, kakupa kila pahala
Mpaka naja kubaini, janati iso jalala
Naweka yangu saini, kama katika hawala
Watembea kwa maringo, ya kweli si singiziwa
Jumbo kiasi viringo, tambo lako kuridhiwa
Bashasha lisilo wigo, haiba wakabidhiwa
Hata pande za udigo, sijapata nadhamiwa
Uzuzu ninaupata, kukuona mdiria
Ulimi ninajing'ata, akili kifikiria
Roho inatapatapa, majadi yamenijia
Huba lililotakata, nisoweza malizia
Penzi fumbo la mjinga, na mwerevu kaingimo
Gonjwa lisilo na kinga, wote latuzidi kimo
Kurugenzi na machinga, sote letu hilo shimo
Hakuna ataepinga, kwa kusema "mimi simo"
Tamati na kaditama, ladha nisije chujua
Nimejipinda inama, kukujuza uje jua
Sina hali wala fana, jinsi unavyozuzua
Kujikimu sintofanya, bila yangu kwako dua
Mbele ya watu gani?
Sioni kama kuna tofauti ya hiyo sentensi ya Kiingereza na kusema "ningependa kuwa nawe pekee usiku wa leo"
Ukimkuta aliyelelewa kiseminari kama mimi anakuuliza "ili iweje eti?"...
Tufanye maombi hadi liamba
:A S angel:
thijui mwenzio, ndo matokeo ya codemixing na code switchingsexy ni mvuto, ww wa wapi?
Haina uzito anaweza asielewe bhana.Mbele ya watu gani?
Sioni kama kuna tofauti ya hiyo sentensi ya Kiingereza na kusema "ningependa kuwa nawe pekee usiku wa leo"