mansakankanmusa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 4,163
- 787
Kwa kawaida yanapotokea machafuko ya namna kama ile ya Mbagala, Kariakaoo na kuwawa polisi znz, yanasemwa mengi hata yale waliyokuwa wakinong'onwa na watu fulanfulan yanajitokeza leo.
Nimejikuta nakutana na watu wakisema waislam hawakufanikiwa kupata elimu kama walivyo wengine, laa. Ni kosa kubwa.
Ni kosa kubwa na ujinga kuwaza hilo, waliofanikiwa kusoma 1. biBle au Divinity hata theologia na 2. waliofanikiwa kusoma Islamic Knowlegde si lazima awe amefikia sharia, atakubaliana nami kwamba hata siku moja usichanganye haya mambo, siri ya waliosoma haya mambo wanaijua wao. kwa ufupi SANA ELEWA HIVYO
Ninaawasihi watanzania wenzangu msikurupuke kubainisha mambo bila kujua undani wake, usimdharau mtu ukadhani hajui kitu, wewe nde mtumwa wa elimu ya wakoloni. Pamoja na hili, kuwachanganya waislam na fujo zilizotokea si vizuri, kulijudge na kuanza kumnyooshea kidole mtu/binadamu mwingine, eti kwa kuwa ni muislam, watanzania watakuwa wanafanya kosa la kulijutia kuwamulika waislam kama wenye fujo.
Tanzania haitakalika na wewe hutakuwa na amani.Nakutana na watu wengi sana, kuchomwa makanisa pale mbagala, hata ofisini kwangu limeniathiri jambo hili, kwa kawaida halinipendezi... persuation ndio nyenzo sahihi kumbadili imani mtu sio nguvu, uislam uko hivyo, wanaotumia nguvu wanakosea, nguvu kwa maana ya kutukana wengine, achilia mbali kuchoma nk,
Sifurahishwi na linayoyaona ofisini na kwa hili utendaji kazi, uchumi na maendeleo ya nchi hii yatapata anguko kubwa, tulizoea sababu mbalimbali zinazochangia kudidimiza chumi zetu, ikiwa pamoja na vita, ukame, nk lkn hizi fujo na mtafaruku vichwani mwa waislam na wakiristu makazini tusitemee maendeleo ya nchi yetu.
Nasikitika kwamba hata Rais ajae, 2015 swala udini ni jambo kubwa hata kuliko kawaida ya sifa na mvuto wa kumwingiza mtu madarakani, mashuleni, majeshini, hospitalini, magerezani, mahakamani, na ktk huduma nyingi udini utafanya kazi yake kutoka sasa, waislam tunasema huu ni msiba mkubwa, vile utaathiri vizazi vijavyo. basi hata tungekuwa tumeoleana,ingesaidia, mbona ukabila hakuna kwa sana, ni kwa kuwa tuna wakwe na wake na waume ktk makabila yenza,ikasaidia kuondoa hisia mbaya ktk wao, katika mambo mabaya ktk jamii ya kiislam na kikiristo ni kuoa au kuolewa na imani ya pili, ni kama yanga na simba, manchester united na man city, chui na mbuzi. kwa kuwa kuoleana kulishindikana na heko kwa wale walioana. basi chuki haina wa kuiamulia, kwa sabb hata polisi wanadini zao, polisi mwislam na mkiristo, mwana jwtz, hakimu, mwalimu yaani hapa ni fujo na upendeleo hata rushwa haina dhara kubwa kama hili. mungu tulinde na haya mambo. mungu ibariki Nchi hii na watu wake. ameen!
Nimejikuta nakutana na watu wakisema waislam hawakufanikiwa kupata elimu kama walivyo wengine, laa. Ni kosa kubwa.
Ni kosa kubwa na ujinga kuwaza hilo, waliofanikiwa kusoma 1. biBle au Divinity hata theologia na 2. waliofanikiwa kusoma Islamic Knowlegde si lazima awe amefikia sharia, atakubaliana nami kwamba hata siku moja usichanganye haya mambo, siri ya waliosoma haya mambo wanaijua wao. kwa ufupi SANA ELEWA HIVYO
Ninaawasihi watanzania wenzangu msikurupuke kubainisha mambo bila kujua undani wake, usimdharau mtu ukadhani hajui kitu, wewe nde mtumwa wa elimu ya wakoloni. Pamoja na hili, kuwachanganya waislam na fujo zilizotokea si vizuri, kulijudge na kuanza kumnyooshea kidole mtu/binadamu mwingine, eti kwa kuwa ni muislam, watanzania watakuwa wanafanya kosa la kulijutia kuwamulika waislam kama wenye fujo.
Tanzania haitakalika na wewe hutakuwa na amani.Nakutana na watu wengi sana, kuchomwa makanisa pale mbagala, hata ofisini kwangu limeniathiri jambo hili, kwa kawaida halinipendezi... persuation ndio nyenzo sahihi kumbadili imani mtu sio nguvu, uislam uko hivyo, wanaotumia nguvu wanakosea, nguvu kwa maana ya kutukana wengine, achilia mbali kuchoma nk,
Sifurahishwi na linayoyaona ofisini na kwa hili utendaji kazi, uchumi na maendeleo ya nchi hii yatapata anguko kubwa, tulizoea sababu mbalimbali zinazochangia kudidimiza chumi zetu, ikiwa pamoja na vita, ukame, nk lkn hizi fujo na mtafaruku vichwani mwa waislam na wakiristu makazini tusitemee maendeleo ya nchi yetu.
Nasikitika kwamba hata Rais ajae, 2015 swala udini ni jambo kubwa hata kuliko kawaida ya sifa na mvuto wa kumwingiza mtu madarakani, mashuleni, majeshini, hospitalini, magerezani, mahakamani, na ktk huduma nyingi udini utafanya kazi yake kutoka sasa, waislam tunasema huu ni msiba mkubwa, vile utaathiri vizazi vijavyo. basi hata tungekuwa tumeoleana,ingesaidia, mbona ukabila hakuna kwa sana, ni kwa kuwa tuna wakwe na wake na waume ktk makabila yenza,ikasaidia kuondoa hisia mbaya ktk wao, katika mambo mabaya ktk jamii ya kiislam na kikiristo ni kuoa au kuolewa na imani ya pili, ni kama yanga na simba, manchester united na man city, chui na mbuzi. kwa kuwa kuoleana kulishindikana na heko kwa wale walioana. basi chuki haina wa kuiamulia, kwa sabb hata polisi wanadini zao, polisi mwislam na mkiristo, mwana jwtz, hakimu, mwalimu yaani hapa ni fujo na upendeleo hata rushwa haina dhara kubwa kama hili. mungu tulinde na haya mambo. mungu ibariki Nchi hii na watu wake. ameen!