Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Asubuhi hii Paul Makonda (UVCCM- Moshi Mjini) karudia maneno yake ya jana kupitia ITV lakini kwa msisitizo mpya kuwa RA akionwa popote AOMBWE KWA UPOLE aondoke nchini kwani ndiye chanzo cha ufisadi wote na kwamba ana uhakika kuwa ameshahamisha familia yake na yuko katika mazingira ya kuwa na uraia zaidi ya nchi moja.
Maswali:
1. Ndg. Paul hivi mtu akithibitika kuwa amefisadi nchi na kukidhoofisha chama adhabu yake ni kumwomba kwa upole ahame nchini? Yaani huku ndio unasema kuwa wewe na wenzako (UVCCM) mnakwenda si kujivua gamba tu bali kuchuna ngozi?
2. Ndg. Paul hivi kama una uthibitisho wa mtu kuwa na uraia wa nchi zaidi ya moja ukiwemo wa TZ (wakati huu), umechukuwa hatua gani kumripoti Uhamiaji au Polisi au hata Usalama wa Taifa (maana hatujui makusudi yake) na utupe maelezo hatua gani zimechukuliwa au hazichachukuliwa na ni kwa nini wakati hilo ni kosa la jinai.
3. Kama leo unaweza kutoka mbele ya TV na kusema huyu ndiye Dowans na madudu yote je unaweza kutuaminisha kuwa yeye mwenyewe tu kama mtu mmoja ndiye alikuwa mbunifu, mpangaji na mtekelezaji wa ufisadi wote kila mahala huko bila usaidizi wa wengine? Na kama unasema uchunguzi unaendelea kuwatafuta wengine, sasa utakamilishaje uchunguzi wako wakati huyu umeshamwomba aondoke!
Zaidi ya yote, alipouzwa swali kuwa mna mazoea ya kuwa wambea wambea hivi na kutumwa na watu fulani fulani, akajibu straight kuwa hilo analikubali kabisa!!
Sasa nami nahitimisha kuwa naona nawe kijana Paul umetumwa kuanzisha propoganda za kumtorosha mtuhumiwa lakini hujui kuwa katika karne hii uelewa wa watu uko juu sana.
Yaani anataka baadaye tukisikia kua jamaa katoweka basi amseme tulishakubaliana kuwa tumwombe atupishe nchini kwetu. Mimi sitakuwa sehemu ya makubaliano hayo ya kipuuzi!
Mimi natoa taarifa katika vyombo vya usalama popote kuwa mkiwaona Paul na RA msiwaombe chochote wakamateni wakaanze kutoa maelezo yao kuwasaidia Polisi uchunguzi kabla ya kuwafikisha mahakamani waliotufisadi na wale waliozembea kutoa taarifa au kushiriki kuwaficha mafisadi kwa namna moja au nyingine.
Jamani ni ajabu sana katika karne hii mtu anakwenda mbele ya TV na kuongea aliyoyasema Paul na bado waTZ tuko kimya tu tunashangaa shangaa na kusema kijana huyu shujaa!! n.k
Kwa nini Mtuhumiwa asikamatwe na vijana kama hawa wenye fast hand infomation wakaisaidia Polisi? Hata wezi wa kuku vijini sijasikia wanaambiwa kuwa waombwe waame kijiji wanakamatwa na sheria inachukua mkondo wake.
Maelezo yaliyotolewa mbele ya TV na Paul ni MATAMU SANA lakini nasikitika kusema si MAZURI na yanakosa welezi katika kuchambua mambo.
Maswali:
1. Ndg. Paul hivi mtu akithibitika kuwa amefisadi nchi na kukidhoofisha chama adhabu yake ni kumwomba kwa upole ahame nchini? Yaani huku ndio unasema kuwa wewe na wenzako (UVCCM) mnakwenda si kujivua gamba tu bali kuchuna ngozi?
2. Ndg. Paul hivi kama una uthibitisho wa mtu kuwa na uraia wa nchi zaidi ya moja ukiwemo wa TZ (wakati huu), umechukuwa hatua gani kumripoti Uhamiaji au Polisi au hata Usalama wa Taifa (maana hatujui makusudi yake) na utupe maelezo hatua gani zimechukuliwa au hazichachukuliwa na ni kwa nini wakati hilo ni kosa la jinai.
3. Kama leo unaweza kutoka mbele ya TV na kusema huyu ndiye Dowans na madudu yote je unaweza kutuaminisha kuwa yeye mwenyewe tu kama mtu mmoja ndiye alikuwa mbunifu, mpangaji na mtekelezaji wa ufisadi wote kila mahala huko bila usaidizi wa wengine? Na kama unasema uchunguzi unaendelea kuwatafuta wengine, sasa utakamilishaje uchunguzi wako wakati huyu umeshamwomba aondoke!
Zaidi ya yote, alipouzwa swali kuwa mna mazoea ya kuwa wambea wambea hivi na kutumwa na watu fulani fulani, akajibu straight kuwa hilo analikubali kabisa!!
Sasa nami nahitimisha kuwa naona nawe kijana Paul umetumwa kuanzisha propoganda za kumtorosha mtuhumiwa lakini hujui kuwa katika karne hii uelewa wa watu uko juu sana.
Yaani anataka baadaye tukisikia kua jamaa katoweka basi amseme tulishakubaliana kuwa tumwombe atupishe nchini kwetu. Mimi sitakuwa sehemu ya makubaliano hayo ya kipuuzi!
Mimi natoa taarifa katika vyombo vya usalama popote kuwa mkiwaona Paul na RA msiwaombe chochote wakamateni wakaanze kutoa maelezo yao kuwasaidia Polisi uchunguzi kabla ya kuwafikisha mahakamani waliotufisadi na wale waliozembea kutoa taarifa au kushiriki kuwaficha mafisadi kwa namna moja au nyingine.
Jamani ni ajabu sana katika karne hii mtu anakwenda mbele ya TV na kuongea aliyoyasema Paul na bado waTZ tuko kimya tu tunashangaa shangaa na kusema kijana huyu shujaa!! n.k
Kwa nini Mtuhumiwa asikamatwe na vijana kama hawa wenye fast hand infomation wakaisaidia Polisi? Hata wezi wa kuku vijini sijasikia wanaambiwa kuwa waombwe waame kijiji wanakamatwa na sheria inachukua mkondo wake.
Maelezo yaliyotolewa mbele ya TV na Paul ni MATAMU SANA lakini nasikitika kusema si MAZURI na yanakosa welezi katika kuchambua mambo.