Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,862
Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi, hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na wala hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
 
Hii issue kheri upambane wewe na familia yako tu. Kama una uwezo wa chakula na vitu vingine fanya hivyo, protect your family tu.
Wengine washaelimishwa na bado wanasubiri masia atakaeiponya nchi baada ya siku tatu za maombi, then waache waamini hivyo.
 
Hivi mbaka sasa hiv, wameshakufa wangapi? Hapa Tz


Sent from my iPhone using JamiiForums

Mkuu suala si kuwa wamekufa wangapi. Suala ni uhusiano wa wanaoambukizwa kulinganisha na wanaopona kwa siku au kwa kipindi fulani.

Hapo itakupa hali ya ugonjwa bila kujali wanaokufa ni wengi au kidogo.

USA, Spain, Germany, Italy, China na kote waliko udhibiti maambukizi ni kidogo kuliko wanaopona.

Uganda, Rwanda na Kenya ni hivyo pia.

Mkuu namba ya wanaokufa haina maana yoyote (irrelevant).

Ila kumbuka mgonjwa hadi kufa au kupona ataambukiza wengine kama 90 kwa hali yetu iliyopo hivi sasa.

Ndani ya wiki 2 - 3 mgonjwa atapona au atakufa kutegemeana na huduma za afya zilivyo alipo au katika nchi.

Pia 5% - 10% ya walioambukizwa watakufa kwa ugonjwa huu.

Kasi ya maambukizi itafanya namba ya wafu kuwa kubwa mno katika kipindi kifupi kama maambukizi hayadhibitiwi.
 
Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndiyo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, wala hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekukuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu mafanikio wala kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevulia kweli hadi tumekabiliwa kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa?

Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali.

Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!
 
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa? Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali. Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!
Lete takwimu hapa kabla na baada ya lockdown hali ipoje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Rais linapokuja suala la majanga anakuwa wa hovyo kwelikweli. Sijui huo upendo anaohubiri ni upi zaidi ya kupambana na majanga kwa watu wake. Ila sishangai maana kwenye utawala wake yamefanyika mambo mengi sana ya kikatili dhidi ya binadamu.

Rais anapokea fedha za kuyakabili majanga yeye anaenda kuzihifadhi BoT ili zi boost uchumi! Sijawahi kuona aisee!
 
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa? Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali. Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!

Kwa sababu hujasoma lolote huna ulichoelewa. Huna ulichojadili. Huna hoja. Huna lolote.

Hakuna povu lolote kwenye bandiko langu bali povu (au pumba) unaloliongelea unalo wewe na lipo kwenye bandiko lako.

Msitutishe. Hii nchi ni yetu sote. Ikibidi paka tutamfunga kengele. Hatuwezi kusubiria kufa tukiona ati kuwa tuondoke. Ondokeni nyinyi.
 
Back
Top Bottom