Nchi Kavu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 4,271
- 2,401
Kwanza nikupongeze kwa habari nazozisoma mitandaoni kuwa utawalipia kodi waathirika 500 wa corona kodi ya miezi mitatu. Hongera sana sana. Pamoja na aina yako ya maisha bado kuna sehemu unajitengenezea hazina isiyooza. Utakumbukwa kwa mengi siku maisha yakonyakitimia hapa duniani. Siombei yatimie leo wala kesho, bali Mungu mwenyewe anajua.
Nina play list yangu hapa ya bongo fleva ambayo huwa naisikiliza wakati na wakati, japo mi sio umri wa bongo fleva. Napaswa zaidi kusikiliza nyimbo za kina Jaydee, Kidumu, Kamilioni, prof J, n.k kwa upande wa bongo fleva. Ila baadhi ya nyimbo za wasanii wa bongo fleva ni nzuri kiasi huwezi acha kuzisikiliza. Wapo kina Barnaba, Baraka Prince, Ben Pol, wewe, Ditto, na wengine
List yangu so far ina nyimbo kumi na tisa. Wewe katika list hii una nyimbo tano!; Sikomi, Ntampata wapi, Ukimwona, Salima ft Mjeda, na hii ya mwisho ambayo ndio nayotaka kuizungumzia. Utanipenda.
Baada ya wimbo huu sidhani kama baada ya hapo kuna wimbo wowote ambao naweza sema nitauweka kwenye list za kuusikiliza, iwe ni faraghani au hadharani. Hizo mnawezana wenyewe maana zinanisuta japo kuna muda natupia vibwagizo kama Jeje. Yah, zipo kadhaa hivi baada ya hapo ila zimenitoka jina. Mijawapo ni ile unaimba kwenye reli ukpiga simu. Nyingine ambayo naweza iongeza ni ile ya shetani kaingiaje sijui wapi.
Sasa wakati nausikiliza huu wa Utanipenda nikaona lipo jambo moja tayari limeshatimia. Nalo nibkuachana na mwanamke ambaye katika nojawapo ya nyimbo zako umesema Zari akakutunuku kidume na mwali. Nadhani ni katika Sikomi. Zari aliyekupa heshima ya kuwa baba wa wana wawili (sijui mmekosana nini) leo mmeshaachana.
Kwenye wimbo humo umeimba mambo mengi ambayo ni hasi juu yako. Wakati nausikiliza ndio nikawa natafakari hayo. Niliupenda huu wimbo kwa audio na video, hasa pale uwanja wa ndege, na pale unashuka na Zari kwenye gari jamaa anakufungulia mlango.
Singependa kuona utabiri wako unaendelea kutimia mmoja baada ya mwingine, hivyo basi, cha kufanya ni kutengeneza wimbo mwingine wa kusawazisha utabiri wako. Ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utakufikia kwa wakati. Tusingependa kumwona tena mama Dangote akiranda mitaani kutafuta ahueni ya maisha wakati tayari maisha anayo. Tusingependa kuona wanao wanaachana na ukwasi walio nao na kuungana na kina kayumba, kisa tu umeshajitabiria. Tengeneza wimbo mwingine.
Mwisho, nyimbo zako za kileo kina Jeje na nduguze zinatuondoa kenye kundi la wasikilizaji wako. Unapiga pesa ndio ila kuna kundi unalipoteza. Ni hayo tu kwa leo. Nawatakia waislam wote mfungo mwema
Sent using Jamii Forums mobile app
Nina play list yangu hapa ya bongo fleva ambayo huwa naisikiliza wakati na wakati, japo mi sio umri wa bongo fleva. Napaswa zaidi kusikiliza nyimbo za kina Jaydee, Kidumu, Kamilioni, prof J, n.k kwa upande wa bongo fleva. Ila baadhi ya nyimbo za wasanii wa bongo fleva ni nzuri kiasi huwezi acha kuzisikiliza. Wapo kina Barnaba, Baraka Prince, Ben Pol, wewe, Ditto, na wengine
List yangu so far ina nyimbo kumi na tisa. Wewe katika list hii una nyimbo tano!; Sikomi, Ntampata wapi, Ukimwona, Salima ft Mjeda, na hii ya mwisho ambayo ndio nayotaka kuizungumzia. Utanipenda.
Baada ya wimbo huu sidhani kama baada ya hapo kuna wimbo wowote ambao naweza sema nitauweka kwenye list za kuusikiliza, iwe ni faraghani au hadharani. Hizo mnawezana wenyewe maana zinanisuta japo kuna muda natupia vibwagizo kama Jeje. Yah, zipo kadhaa hivi baada ya hapo ila zimenitoka jina. Mijawapo ni ile unaimba kwenye reli ukpiga simu. Nyingine ambayo naweza iongeza ni ile ya shetani kaingiaje sijui wapi.
Sasa wakati nausikiliza huu wa Utanipenda nikaona lipo jambo moja tayari limeshatimia. Nalo nibkuachana na mwanamke ambaye katika nojawapo ya nyimbo zako umesema Zari akakutunuku kidume na mwali. Nadhani ni katika Sikomi. Zari aliyekupa heshima ya kuwa baba wa wana wawili (sijui mmekosana nini) leo mmeshaachana.
Kwenye wimbo humo umeimba mambo mengi ambayo ni hasi juu yako. Wakati nausikiliza ndio nikawa natafakari hayo. Niliupenda huu wimbo kwa audio na video, hasa pale uwanja wa ndege, na pale unashuka na Zari kwenye gari jamaa anakufungulia mlango.
Singependa kuona utabiri wako unaendelea kutimia mmoja baada ya mwingine, hivyo basi, cha kufanya ni kutengeneza wimbo mwingine wa kusawazisha utabiri wako. Ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utakufikia kwa wakati. Tusingependa kumwona tena mama Dangote akiranda mitaani kutafuta ahueni ya maisha wakati tayari maisha anayo. Tusingependa kuona wanao wanaachana na ukwasi walio nao na kuungana na kina kayumba, kisa tu umeshajitabiria. Tengeneza wimbo mwingine.
Mwisho, nyimbo zako za kileo kina Jeje na nduguze zinatuondoa kenye kundi la wasikilizaji wako. Unapiga pesa ndio ila kuna kundi unalipoteza. Ni hayo tu kwa leo. Nawatakia waislam wote mfungo mwema
Sent using Jamii Forums mobile app