Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,559
- 41,071
Mtawala shetani ni laana kwa watu wake, ni laana kwa majirani na Dunia nzima.
Hatukuwahi kushuhudia wala kusikia hata mara moja kuna kombora au hata risasi moja imerushwa toka Ukraine au nchi yoyote ya NATO kuishambulia Urusi.
Lakini mwanzoni mwa mwakajana, Dunia ilishuhudia kiongozi shetani wa Russia, Putin, akienda kuivamia Ukraine kwa vile tu aliamini Taifa lake lina nguvu kubwa za kijeshi, na hivyo anaweza kufanya chochote dhidi ya Taifa lolote.
Putin akasababisha mauaji ya kinyama ya watoto, wazee na watu wengine wengi wa rika zote, kwa maelfu nchini Ukraine. Putin pia amesababisha mauaji ya askari wengi wa nchini mwake na Ukraine, bila ulazima.
Mtu mmoja tu, Putin kasababisha roho za watu maelfu zipotee, na watu kwa maelfu kuwa wakimbizi. Bila shaka, watu wengi ndani ya Ukraine, na sisi wengine tulikumbushwa kuwaombea wananchi wa Ukraine walioingizwa kwenye mauaji na mateso ya vita.
Mungu hujibu maombi ya mwanadamu kwa wakati wake ufaao, na kwa namna ile ifaayo, na wakati fulani hata kwa namna ambayo haikutegemewa.
Leo, Dunia nzima, habari kuu, ni maasi ya askari wa kundi la Wagner dhidi ya jeshi la Urusi. Mpaka sasa kundi la Wagner limekwisha ua baashi ya wanajeshi, wamekwishadungua ndege 5 na jeshi la serikali zilizokuwa zimelenga kuwashambulia.
Wapiganaji wa Wagner wanaelekea Moscow huku wanajeshi wa Serikali wakiamua kusalimu amri. Ndege ya Rais Putin imeruka na kuelekea kusikofahamika, lakini Serikali imesema Putin bado yupo Moscow (ni kweli au uwongo, hatujui). Putin, mapema amelihutubia Taifa, kwa sauti na kauli ya kinyonge, na kusema kuwa hili ni pigo kubwa.
Hivi ndivyo Mungu wa haki anavyotenda kazi, akitaka kumpa ushindi mnyonge anayeonewa. Leo siyo Ukraine inayopambana na jeshi la Urusi, bali ni warusi dhidi ya warusi. Hii ni kumkaanga samaki kwa mafuta yake mwenyewe.
Wana wa Mungu, tumshukuru Mungu kwaajili ya maisha ya wasio na hatia huko Ukraine. Tuzidi kuomba ukuu wa Mungu dhidi ya Putin na wauaji wengine wote.
Hatukuwahi kushuhudia wala kusikia hata mara moja kuna kombora au hata risasi moja imerushwa toka Ukraine au nchi yoyote ya NATO kuishambulia Urusi.
Lakini mwanzoni mwa mwakajana, Dunia ilishuhudia kiongozi shetani wa Russia, Putin, akienda kuivamia Ukraine kwa vile tu aliamini Taifa lake lina nguvu kubwa za kijeshi, na hivyo anaweza kufanya chochote dhidi ya Taifa lolote.
Putin akasababisha mauaji ya kinyama ya watoto, wazee na watu wengine wengi wa rika zote, kwa maelfu nchini Ukraine. Putin pia amesababisha mauaji ya askari wengi wa nchini mwake na Ukraine, bila ulazima.
Mtu mmoja tu, Putin kasababisha roho za watu maelfu zipotee, na watu kwa maelfu kuwa wakimbizi. Bila shaka, watu wengi ndani ya Ukraine, na sisi wengine tulikumbushwa kuwaombea wananchi wa Ukraine walioingizwa kwenye mauaji na mateso ya vita.
Mungu hujibu maombi ya mwanadamu kwa wakati wake ufaao, na kwa namna ile ifaayo, na wakati fulani hata kwa namna ambayo haikutegemewa.
Leo, Dunia nzima, habari kuu, ni maasi ya askari wa kundi la Wagner dhidi ya jeshi la Urusi. Mpaka sasa kundi la Wagner limekwisha ua baashi ya wanajeshi, wamekwishadungua ndege 5 na jeshi la serikali zilizokuwa zimelenga kuwashambulia.
Wapiganaji wa Wagner wanaelekea Moscow huku wanajeshi wa Serikali wakiamua kusalimu amri. Ndege ya Rais Putin imeruka na kuelekea kusikofahamika, lakini Serikali imesema Putin bado yupo Moscow (ni kweli au uwongo, hatujui). Putin, mapema amelihutubia Taifa, kwa sauti na kauli ya kinyonge, na kusema kuwa hili ni pigo kubwa.
Hivi ndivyo Mungu wa haki anavyotenda kazi, akitaka kumpa ushindi mnyonge anayeonewa. Leo siyo Ukraine inayopambana na jeshi la Urusi, bali ni warusi dhidi ya warusi. Hii ni kumkaanga samaki kwa mafuta yake mwenyewe.
Wana wa Mungu, tumshukuru Mungu kwaajili ya maisha ya wasio na hatia huko Ukraine. Tuzidi kuomba ukuu wa Mungu dhidi ya Putin na wauaji wengine wote.