Nyamizi
Platinum Member
- Feb 19, 2009
- 9,190
- 13,734
Chochote kinaweza kutokea kwa Yanga kupata matokeo mpira hauna nyumbani ni kujipanga kwa mbinu sahihi na kuchagua wachezaji sahihi. Yanga mechi ya Dar walikuwa wamewapa nafasi sana wapinzani wafanye wanavyotaka hawakufanya pressing tokea juu ili kutowapa nafasi wapinzani wao.
Wamewaacha Rivers wacheze kwa ku relax tu huku Yanga wakikabia kwa macho. Kwa mchezo uliochezwa Dar Rivers walipaswa kuondoka na ushindi mnono ila waneshindwa kutumia nafasi nyingi walizopata hilo ni tatizo pia kwa Rivers.
Upande wa Yanga wachotakiwa kufanya ni kuongeza viungo kati ikibidi Feisal arudi nafasi yake, kocha achague wachezaji wazuri mbona wachezaji wazuri wapo japokuwa bado timu haijawa nzuri. Yule Moloko asipangwe Yacouba asipangwe.
Yusuph Athuman anaweza kusaidiana vizuri sana na Makambo. Bangala pia sio wakuwekwa benchi. La muhimu zaidi wapambanie ITC ya Djuma na Aucho wanaweza kuongeza kitu kwa Yanga wachezaji wa. Yanga waongeze umakini kwenye kukaba na kutengeneza nafasi na kuzitimua nafasi chache zinazopatikana.
Yanga wana tatizo kubwa la kutoweza kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani. Ila mechi ya away bado naona Yanga kuna kitu wakikifanya wanaweza kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza
ITC ya Djuma haina msaada kwa sasa,endapo itapatikana ataruhusiwa kucheza round inayofuata kama Yanga itafuzu.Lakini kwa mechi ya marudiano haruhusiwi,kama nilimwelewa vizuri Mwanasheria wa Yanga alilitolea maelezo hili.