Kwa yaliyotokea Mwanza kwa utawala huu kama ilivyokuwa kwa awamu ile, hakuna jipya.
Nisiache kumlilia hayati baba wa Taifa (rip) kiongozi mzalendo aliyejawa haiba zote za haki, uhuru na usawa:
Kudai haki, uhuru, demokrasia na maendeleo hakujawahi kuwa rahisi. Ni jukumu zito la kizalendo na kihistoria linalosongwa vilivyo na kila aina ya shari, uzandiki, vikwazo, hatari, visa, vifungo na hata vifo.
"No easy walk to freedom" -- aliyaona Nelson Mandela.
Ni kujitolea kuliko kwa kiwango cha juu sana kuipita njia hii katika hali ya uaminifu uliotukuka.
"Viva kamanda Mbowe, kamanda Heche na makamanda wote kokote kule mliko. Ama kwa hakika hamko peke yenu."
Hapa tulipo, ni mwanzo tu. Kurudi nyuma siyo uchaguzi. Tuendako ni kugumu zaidi lakini haki haijawahi kushindwa. Inshallah tutafika.
Tangu lini yatima akadeka? Kama ulivyo mtaji wa masikini, mtaji wake ni nguvu zake mwenyewe.
"Tusipowakataa na kuwapinga viongozi kama hawa, basi janga kubwa linakuja na tabia zao ni za kidikteta" -- Julius Nyerere.
Ni dhahiri zaidi sasa kuwa katiba mpya ni muhimu na ya dharura sana kuliko wakati mwingine wowote.
Muhimu mipango mikakati mipya ikaelekezwe kwenye kujilinda na kuwafidia wahanga wote wa harakati hizi tukufu.
Aluta Continua!
Nisiache kumlilia hayati baba wa Taifa (rip) kiongozi mzalendo aliyejawa haiba zote za haki, uhuru na usawa:
Kudai haki, uhuru, demokrasia na maendeleo hakujawahi kuwa rahisi. Ni jukumu zito la kizalendo na kihistoria linalosongwa vilivyo na kila aina ya shari, uzandiki, vikwazo, hatari, visa, vifungo na hata vifo.
"No easy walk to freedom" -- aliyaona Nelson Mandela.
Ni kujitolea kuliko kwa kiwango cha juu sana kuipita njia hii katika hali ya uaminifu uliotukuka.
"Viva kamanda Mbowe, kamanda Heche na makamanda wote kokote kule mliko. Ama kwa hakika hamko peke yenu."
Hapa tulipo, ni mwanzo tu. Kurudi nyuma siyo uchaguzi. Tuendako ni kugumu zaidi lakini haki haijawahi kushindwa. Inshallah tutafika.
Tangu lini yatima akadeka? Kama ulivyo mtaji wa masikini, mtaji wake ni nguvu zake mwenyewe.
"Tusipowakataa na kuwapinga viongozi kama hawa, basi janga kubwa linakuja na tabia zao ni za kidikteta" -- Julius Nyerere.
Ni dhahiri zaidi sasa kuwa katiba mpya ni muhimu na ya dharura sana kuliko wakati mwingine wowote.
Muhimu mipango mikakati mipya ikaelekezwe kwenye kujilinda na kuwafidia wahanga wote wa harakati hizi tukufu.
Aluta Continua!