Aggrey86
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 853
- 155
Kisha akawaambia "Tuseme mmoja wenu anaye rafiki,akaenda kwake usiku wa manane,akamwambia Rafiki tafadhali niazime mikate mitatu kwa kuwa rafiki yangu amepitia kwangu akiwa safarini nami sina cha kumpa,Naye akiwa ndani angemjibu "usinisumbue! Nimekwisha funga mlango.Mimi na watoto wangu tumelala siwezi kuamka nikupe! Hakika ingawa hataamka ampe kwa sababu yeye ni rafiki yake lakini,kwa sababu ya huyo mtu kuendelea kumwomba ataamka ampe chochote,kwa hiyo ombeni nanyi mtapewa,tafuteni nanyi mtapata,bisheni nanyi mtafunguliwa.Luka 11-5-13. Ninachotaka kuwaambia ndugu zangu ni kwamba msikate tamaa hata siku moja kwenye kutafuta kwenu endeleeni kugonga mbele ya Mungu wako unayemwabudu mwambie Mungu akufungulie mlango wa ajira mlilie Mungu wako,mtolee sauti Mungu wako,mwambie Mungu wako hakika nawaambieni mtaona Mungu alivyo mwema na atafungua tu usikatishwe tamaa eti sehemu fulani ukiomba kuna udini,kuna ukabira,kuna kujuana hapana wewe tuma tu barua zako mara kwa mara na unafanya juhudi za kutafuta kazi hakika maombi yako yatajibiwa tu..si umeona mfn, wa huyu rafiki aliyeenda kuomba mkate kwa rafiki yake usiku wa manane,japo jamaa alimjibu kwamba amekwisha lala lakini yeye aliendelea kugonga tu na kuomba jamaa baada ya kuona usumbufu akaamua kuamka na kumpa tu..najua hatuwezi kupata wote kwa pamoja ajira lakini yatupasa kupambana hadi mwisho hakika tutafanikiwa..kwa hiyo ndugu zangu msikatishwe tamaa na chochote kile..nawatakieni kila la kheri kwenye mapambano haya.Mungu awabariki sana Mungu ibariki JF iendelee kudumu.