Kwa wenye tatizo la PUMU, jaribu tiba hii inaweza kukusaidia ama kukuponyesha kabisa

Norshad

JF-Expert Member
Jun 3, 2013
5,128
12,216
Salaam,

Natumai wote mmeamka salama.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika je unasumbuliwa na Pumu? Basi inawezekana leo upo mahali sahihi pa kupata tiba ambayo inaweza ondoa kabisa hilo tatizo lako na ni tiba isiyohusisha madawa ya hospitalini, bali chakula tu.

Chukua kweme, kwa wenyeji wa kaskazini mnazifahamu hizi.
(kokwa za kweme zapatikana sokoni ama kwenye maduka ya Tiba asili, pamoja na kipande cha Papa - SAMAKI (vipande) inategemea mwenyewe unatakaje kulingana na usugu wa tatizo lako

Saga kweme zako mfano wa karanga za kusaga kisha chemshia na hicho kipande ama vipande vya papa, kisha kunywa ile Supu yake, unaweza rudia kutumia hii kitu sababu pia ni kama Supu tu, lakini wewe mwenye tatizo hilo kwako itakuwa ni Supu Tiba.

Inaweza kukusaidia sana ama ukapona kabisa kulingana na usugu wa hilo tatizo, na hii unaweza tumia hata mwenye Pumu ya kurithi.

Kwa wale ambao watatumia tiba hii msisite kuleta mrejesho kwenye uzi huu ili na wengine wafaidike na Tiba hii mujarabu kabisa.

Nimeona kuna umuhimu wa kuweka hapa ili kusaidia na wengine wenye shida hiyo, binafsi nimewasaidia watu kadhaa kwa kuwapa tu maelekezo haya haya na nashukuru wengi wao kwa sasa wapo vizuri na wengine wanasema tatizo hilo limeisha kabisa.

Kila la kheri..

NB: Mimi si mtaalamu wa Tiba Asili bali tiba hii nimefundishwa na Bibi mmoja shamba huko na mimi nimeileta hapa kwenu. Kwa upande wangu nina watu 10nambao wametumia na kati ya hao wapo waliopona kwa maelezo yao na wapo ambao wanasikilizia mpaka sasa kama itarudi tena ama vipi.

Hivyo basi kama tujuavyo inaweza mfaa huyu na mwinyine isimfae lakini unaweza kujarib7 sababu ni kama mboga tu, kweme unaweza tumia kuungia mboga mfano wa nazi na Papa nadhani wote tunamfahamu. (Papa samaki sio Papa wa Gigy Money.

Shukran
 
Salaam.

Natumai wote mmeamka salama.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika je unasumbuliwa na Pumu? Basi inawezekana leo upo mahali sahihi pa kupata tiba ambayo inaweza ondoa kabisa hilo tatizo lako na ni tiba isiyohusisha madawa ya hospitalini, bali chakula tu.

Chukua kweme, kwa wenyeji wa kaskazini mnazifahamu hizi.
( kokwa za kweme zapatikana sokoni ama kwenye maduka ya Tiba asili, pamoja na kipande cha Papa - SAMAKI ( vipande ) inategemea mwenyewe unatakaje kulingana na usugu wa tatizo lako

Saga kweme zako mfano wa karanga za kusaga kisha chemshia na hicho kipande ama vipande vya papa, kisha kunywa ile Supu yake, unaweza rudia kutumia hii kitu sababu pia ni kama Supu tu, lakini wewe mwenye tatizo hilo kwako itakuwa ni Supu Tiba.


Inaweza kukusaidia sana ama ukapona kabisa kulingana na usugu wa hilo tatizo, na hii unaweza tumia hata mwenye Pumu ya kurithi.

Kwa wale ambao watatumia tiba hii msisite kuleta mrejesho kwenye uzi huu ili na wengine wafaidike na Tiba hii mujarabu kabisa.

Nimeona kuna umuhimu wa kuweka hapa ili kusaidia na wengine wenye shida hiyo, binafsi nimewasaidia watu kadhaa kwa kuwapa tu maelekezo haya haya na nashukuru wengi wao kwa sasa wapo vizuri na wengine wanasema tatizo hilo limeisha kabisa.

Kila la kheri..


NB: mimi si mtaalamu wa Tiba Asili bali tiba hii nimefundishwa na Bibi mmoja shamba huko na mimi nimeileta hapa kwenu. Kwa upande wangu nina watu 10nambao wametumia na kati ya hao wapo waliopona kwa maelezo yao na wapo ambao wanasikilizia mpaka sasa kama itarudi tena ama vipi...

Hivyo basi kama tujuavyo inaweza mfaa huyu na mwinyine isimfae lakini unaweza kujarib7 sababu ni kama mboga tu, kweme unaweza tumia kuungia mboga mfano wa nazi na Papa nadhani wote tunamfahamu. ( Papa samaki sio Papa wa Gigy Money.


Shukran
Asante ila kwa sisi tulio huku Shinyanga uyo papa tutampata wapi....? Asante kwa elimu
 
Safi.
Hao waliotumia imechukua muda gani kupona
Mmoja muhanga wa PUMu ni mke wangu kabisaa na mwanangu, hivi naandika nina miezi miwili haijarudi, yaani tumesumbuka miaka ndugu, alikuwa anaishi kwa vidonge tuu mwisho wakataka kumpa kile kidude cha kupuliza hapo nilikataa, ndipo mama mwenye nyumba hapo nilipopanga akaniambia mwanangu mkeo ana Pumu na akishika mimba anaweza kuwa na hali mbaya zaidi tumia hii dawa, ndio akanielekeza, sasa shida ikawa nilipokuwa na huo upatikanaji wa Papa ikawa ishu, ikabidi niagize Dar, sasa hivi nashukuru tangu atumie mpaka sasa kimyaa analala fresh kabisa na yeye alitumia mara mbili tu. Yule mama anasema yeye na wanawe woote walikuwa nayo na yeye mpaka sasa kapona na watoto wake woote wamepona kabisa. Baada ya hapo nami nimekuwa nikiwasaidia wale wenye Pumu kwa kuwaelekeza kama nilivyofanya hapa.
 
Mmoja muhanga wa PUMu ni mke wangu kabisaa na mwanangu, hivi naandika nina miezi miwili haijarudi, yaani tumesumbuka miaka ndugu, alikuwa anaishi kwa vidonge tuu mwisho wakataka kumpa kile kidude cha kupuliza hapo nilikataa, ndipo mama mwenye nyumba hapo nilipopanga akaniambia mwanangu mkeo ana Pumu na akishika mimba anaweza kuwa na hali mbaya zaidi tumia hii dawa, ndio akanielekeza, sasa shida ikawa nilipokuwa na huo upatikanaji wa Papa ikawa ishu, ikabidi niagize Dar, sasa hivi nashukuru tangu atumie mpaka sasa kimyaa analala fresh kabisa na yeye alitumia mara mbili tu. Yule mama anasema yeye na wanawe woote walikuwa nayo na yeye mpaka sasa kapona na watoto wake woote wamepona kabisa. Baada ya hapo nami nimekuwa nikiwasaidia wale wenye Pumu kwa kuwaelekeza kama nilivyofanya hapa.
Mungu atakulipa sawia na wema wako, barikiwa sana nasi tutawajuza wasiofika humu.
 
Wakuu, salaam.

Katika threads kadhaa humu zihusuzo ugonjwa wa PUMU, nimeona mdau Kisima anatangaza humu tiba yake ya PUMU ambayo anadai kwamba inatibu na kuponya kabisa (permanently) ugonjwa wa pumu kwa mtu yeyote.

Je, kuna wadau humu waliotumia dawa hiyo na ikawaponya kabisa? Share nasi ushuhuda wako.
 
Sasa chifu uzi utoe wewe kisha tena comments zote from first up to about tenth ni za kwako mwenyewe!
 
Sasa chifu uzi utoe wewe kisha tena comments zote from first up to about tenth ni za kwako mwenyewe!

Kwani nini mbaya mkuu?

Hao wadau niliowaalika hapa nimeona kwenye nyuzi kadhaa kwamba walitumia dawa husika ya mkuu Kisima, lakini sikufanikiwa kuona feedback zao kuhusu tiba hiyo.
 
Mkuu Bill , tia neno hapa
Mimi nilivyochukua hii dawa sikuuliza kwa mtu. Haya mambo ni ya kiimani zaidi kwa hiyo fanya kile unaamini. Mimi nikikuambia hapa isitokee vile unategemea kutokana labda na mazingira au imani hata pengine matokeo yakawa na madhara utanilaumu
 
Mimi nilivyochukua hii dawa sikuuliza kwa mtu. Haya mambo ni ya kiimani zaidi kwa hiyo fanya kile unaamini. Mimi nikikuambia hapa isitokee vile unategemea kutokana labda na mazingira au imani hata pengine matokeo yakawa na madhara utanilaumu

Siasa nyiiingi. Unashindwa nini kushea tu experience yako kama tiba iliponya tatizo ama haikuponya? (kwa upande wako ulivyoitumia).

Unaanza risala za imani.
 
Back
Top Bottom