enzi za zamani haikuwa rahisi mzazi kupima uzito wa mtoto wake klinik mara kwa mara.
Kamba ile nyeusi anayovalishwa mtoto kiunoni na au mkononi, ilikuwa ni katika kusaidia kupima ukuaji wa mtoto.
Kama ikiendelea kumbana mtoto, mzazi anajua mtoto anendelea vema, ila kama ikianza kupwaya, anajua kuna shida mahala.
Pia katika kamba hizo, kuna baadhi ya mila wanazitengenezea pamoja na kitovu cha mtoto, sijawahi kujua kwa nini.
Ila siamini kama kuna ushirikina hivyo, halafu kamba kuwa nyeusi nsdhani ni pamoja na kuficha uchafu ama rangi kubadilika ukilinganisha na rangi zingine.
Sasa hivi hata usipotumia kamba, klinik zipo kwa wingi.