unajua kwa nini leo nimeitembelea hii thread baada ya takribani siku 10 kupita?
jibu ni rahisi, nahitaji nikusaidie drama nyengine ya kuangalia kwa sababu nimeshaona dalili za uanaharakati kutoka kwako, ila tu chonde chonde karata zako zichange vizuri dada yangu yasije yakakutokezea ya bwana
jung do jeon a.k.a sambong.
Kabla hujaanza kuifuatilia historical drama nyengineyo basi itafute hii lakini bahati mbaya kissasian haipo.
- Jeong Do Jeon at Dramanice
ukiiangalia hii picha kwa macho yote mawili utakutana na veterani actor watupu ambao wanafahamu maana halisi ya kuigiza historical drama. kama ilivyo
jing bi rok drama na humu ndani vile vile hamuna muda wa mapenzi bali ni ubabe wa wanasiasa.
kama umewahi kuiangalia
six flying dragons drama na ukaiangalia na hii itakuwa unatembea mule mule ila kwa asiyefahamu
six flying dragons ni project ya mwaka 2015 wakati hii ni project ya mwaka 2014.
mwandishi wa
six flying dragons kwa kiasi kikubwa anatulazimisha tuamini ya kwamba shujaa aliyefanikiwa kuiangusha goryeo na kuzaliwa joseon alikuwa ni
yi bang won ambaye baadaye anakuwa mfalme wa tatu wa joseon (taejong) baada ya kufanya mapinduzi ya damu kwa ndugu zake na wapinzani wake, lakini shujaa wa ukweli ni huyu jamaa anayeitwa jung do jeon(sambong)
humu ndani utaona jinsi gani sambong alivyoweza kupambana kutoka mwanasiasa asiyekuwa na nguvu hadi akafanikiwa kumshinda waziri mkuu wa goryeo na mpaka kufikia hatua ya kuiangusha Goryeo kingdom na kuzaliwa Joseon akishirikiana na
general yi seong gye. Kuna tabu nyingi sana alizipitia ikiwemo kugombana na rafiki yake kipenzi jung moong jo
best historical drama na hutojutia kuitazama nakuahidi.
- Jeong Do-jeon alizaliwa na kufariki (1337-1398), alikuwa ni mwanasiasa na mwanamapinduzi wa ukweli nyakati hizo za goryeo hadi joseon.
- ndiye alikuwa bwana mipango wa general yi seong gye ambaye ndiye mfalme wa kwanza wa joseon (taejo).Wawili hao walikutana kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 1383 maeneo ya hamgyeong.
- walipofanikiwa kuiangusha goryeo alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa kwanza wa joseon.
- wakati joseon makao makuu yake yalipojengwa hanyang, sambong ndiye aliyependekeza ikulu ipewe jina la Gyeong bokgung.
sambong alijikuta akiingia kwenye mgogoro na
Yi Bang-won kwa sababu ya vita ya urithi wa madaraka ambapo sambong kiupande wake hakuvutiwa na mtazamo wa kiuongozi aliyokuwa nao yi bang won.
- sambong aliamini ya kwamba serikali bora ni ile inayoongozwa na watu wote wakiwa na uhuru wa kutoa mawazo yao mbele ya kiongozi mkuu, sambong aliamini ya kwamba pindi kiongozi mkuu wa nchi anapoongoza nchi kwa ushirikiano wa watumishi bora aliowachagua basi hata kama mfalme ni mediocre basi siasa ataiweza. Dhana hii kiupande fulani ilipingwa na wapinzani wake ambao waliamini ya kwamba sambong alikuwa na mpango wa kujimilikisha madaraka kwa kumtumia mtoto mdogo wa yi seong gye. lakini hoja zao alizijibu ya kwamba mfalme ndiye mwenye mamlaka ya kunichagua mimi na pia ana mamlaka ya kuniondoa mimi hivyo basi kama ataniona ni tishio basi atakuwa na haki ya kuniondoa madarakani.hivyo basi aliamini kama yi bang won atashika madaraka ataongoza kwa mkono wa chuma.
- yi bang won na washirika wake waliamini ya kwamba kwa kuwa joseon bado ni taifa changa basi linamhitaji zaidi kiongozi atakayekuwa na msimamo ili aweze kulivukisha mbali taifa hilo kwa sababu bado waliendelea kujitokeza wanaharakati waliotaka kuirudisha goryeo. Vita ya watu hawa wawili wenye akili nyingi ilimalizwa kwa mapinduzi ambapo yi bang won aliwaua ndugu zake ambao walikuwa hawakubaliani kimtazamo na vile vile alimuua sambong na watu wake na kumtangaza kama ni msaliti wa nchi. yale aliyoyahofia sambong ndiye yaliotokezea wakati wa utawala wa mfalme taejong kwa miaka 18 ya utawala wake kwa sababu alitawala kidikteta, japokuwa alifanikiwa kuifanya joseon kuwa taifa imara kabla hajamuachia madaraka yote mtoto wake yi do (sejong the great). Nilichowapendelea zaidi wanasiasa hawa wawili ni kwamba wote walitaka kuyapigania maslahi ya wananchi na si matumbo yao
great thinker
jeong mong ju na
jung do jeon walikuwa ni marafiki sana nyakati hizo wanasoma pamoja mpaka kujiingiza kwenye siasa nyakati za goryeo. wawili hao kwa pamoja walikuwa na ndoto ya kuleta mageuzi kwenye utawala wa goryeo ambao uligubikwa na rushwa na ubadhirifu wa rasilimali nyakati za mwishoni.
bahati mbaya sana wawili hao walipoteana njia baada ya sambong kubadili msimamo wake wa kutaka kuirudishi heshima goryeo hadi kufikia hatua ya kuizamisha goryeo na kuanzisha joseon.
- sambong aliamini ya kwamba kwa hatua iliofikia goryeo hakuna uwezekano wa kuirudisha katika njia ilionyooka kama ndoto zao zinavyowaaminisha, bali njia pekee ni kuizamisha goryeo iliotawaliwa na ukoo wa WANG ( from emperoe wangun to.....). sambong aliamini ya kwamba taifa jipya chini ya kiongozi mpya atakayekuwa chini ya wanasiasa wanaokwenda na wakati ndiyo ukombozi wa wananchi.
- great thinker jeong mong ju aliamini ya kwamba kubadilisha jina la taifa kusingeliondoa uhalisia wa dhiki wanazokumbana nazo wananchi, kiupande wake aliamini goryeo hii inayoonekana kuchoka kama atapatikana kiongozi bora basi wananchi watayafurahi maisha, hivyo basi alikataa maoni ya sambong na wafuasi wake mpaka kufa kwake, bwana yule aliamini ya kwamba Tanzania kuipa jina jipya la Dubai haimaanishi chochote kiuhalisia kama viongozi wake hawaendani na jina la Dubai. msimamo wa bwana huyu ulikuwa ni mwiba mchungu sana kwa upande wa sambong na wafuasi wake kwa sababu yeye aliyekuwa ndio nguzo ya mwisho ya goryeo, hivyo basi kama jeong mong jo angeliachana na mkakati wa kuipigania goryeo na kuungana na sambong basi urafiki wao ungeliendelea kuwepo kama mwanzoni.
hatimaye Jeong Mong-ju aliuliwa mnamo mwaka 1392 kwenye daraja la sonjuk na aliyeongoza mauaji hayo ni yi bang won, nyakati hizo sambong alikuwa kifungoni kutokana na harakati zake za kuiangusha goryeo.
historia hadi leo inamtaja Jeong Mong-ju kama ni mzalendo wa ukweli aliyeamua kufa kwa ajili ya nchi yake ya Goryeo. kifo chake ndio ulikuwa mwisho wa taifa la goryeo kuendelea kuwepo kwani mwaka huo ndio taifa la joseon lilipoanzishwa.
siku chache kabla ya kifo chake vita ya maneno kati ya pande mbili hizo ilizuka ila kwa njia ya ushairi
yi bang won aliandika shairi lifuatalo
What shall it be: this or that?
The walls behind the temple of the city's deity* has fallen - shall it be this?
Or if we survive together nonetheless - shall it be that?
jeong mong ju naye akajibu
Though I die and die again a hundred times,
That my bones turn to dust, whether my soul remains or not,
Ever loyal to my Lord, how can this red heart ever fade away?
KBS DRAMA AWARDS:2014
- Daesang awards (muigizaji bora wa mwaka) : Yoo Dong Geun ambaye pia mwaka huu amebeba tunzo hii
- High Excellence Award in Acting :Jo Jae Hyun
- Excellence Award in Acting park Young Gyu
- Best Screenwriter :Jeong Hyun Min
ina maana hii drama ndio ilibeba tunzo ya ubora kwa mwaka 2014, mwaka 2015 drama ya
jing bi rok the memoir of imjin war ndio ilibeba drama bora ya mwaka.
kwa maelezo zaidi tembelea tovuti hii
anyeong