Kwa waoaji na waolewaji

Kwa waoaji na waolewaji

nasi

Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
47
Reaction score
20
Utasikia.

Siku ya harusi nitavaa suti gani kali? Nitavaa shela gani la nguvu? Nitatembeaje wakati naingia ukumbini? Tutatumia style gani ya kulishana keki? Nitaanzaje kulivua lile shela lake tukifika hotelini?

Hakuna anayewaza, Hivi akifukuzwa kazi akawa hana mshahara bado nitamuheshimu? Akijifungua halafu akanenepeana kupitiliza bado nitamwita baby? Akiumwa halafu nguvu zake za nanihii zikapotea bado ntakuwa mwaminifu? Akipata ajali na kuwa na kilema cha maisha hivi bado nitamuenzi?

Kama unatumia muda mwingi kufikiria harusi ya siku moja kuliko ndoa ya miaka hamsini, pole sana, inawezekana unataka kuwa bibi/bwana harusi lakini hutaki kuwa mke/mume. Kupanga ni kuchagua.

SHAKE WELL BEFORE USE.
 
Usiishi kama utakufa kesho ishi kama utaishi milele
 
Maji ulishayaamulia kuyavulia nguo kwa nin unawe
 
One day at a time, One thing at a time.

Unawaza hivyo vyoote halafu ufanyeje sasa? Hata utumie miaka mingapi kufikiri, waweza kujua lisaa limoja mbele kitatokea nini? Ndio maana tunaangalia na kusonga mbele kwamatumaini na kwa kutegemea mazuri.

Mtu akiishi kwa woga na kuwaza mabaya, atakaribisha mabaya. Akiishi kwa kufikiri na kukiri mazuri nayo yatakua sehemu yake.

Utasikia...............
Hakuna anayewaza, Hivi akifukuzwa kazi akawa hana mshahara bado nitamuheshimu? Akijifungua halafu akanenepeana kupitiliza bado nitamwita baby? Akiumwa halafu nguvu zake za nanihii zikapotea bado ntakuwa mwaminifu? Akipata ajali na kuwa na kilema cha maisha hivi bado nitamuenzi?......
SHAKE WELL BEFORE USE!
 
Gari za Kwenda mOSHI uchagani zimeanza kuwa za SHEEEEdaaah.
 
Ukiona hivi, ujue umetawanya ikulu ya maharusi.
Excellent
^^
 
Hasa wadada ndo zao,walio wengi wanawaza na kuthamini HARUSI kuliko NDOA.
Wanashindwa kutambua kuwa NDOA ni kitu kikubwa kuliko HARUSI. SOMO KWENU.
 
One day at a time, One thing at a time.

Unawaza hivyo vyoote halafu ufanyeje sasa? Hata utumie miaka mingapi kufikiri, waweza kujua lisaa limoja mbele kitatokea nini? Ndio maana tunaangalia na kusonga mbele kwamatumaini na kwa kutegemea mazuri.

Mtu akiishi kwa woga na kuwaza mabaya, atakaribisha mabaya. Akiishi kwa kufikiri na kukiri mazuri nayo yatakua sehemu yake.


I wish nikufahamu, unishauri mambo flan!
 
Back
Top Bottom