Kwa waliosoma secondary kabla ya simu za mkononi tu.

Kwa waliosoma secondary kabla ya simu za mkononi tu.

Nakumbuka masurufu kama mkate na orange squash wakati wa kwenda likizo pia kufuta tiketi za basi kwa mafuta ya break na sabuni ili kujipatia nauli kuliko ile halali. Mambo ya autograph nilikuwa naangalia kwa wenzangu tu
 
me nilikua mtu wa ajabu sana kwakweli, hivi vitu nilikua navionatu kwa wenzangu sikuwah kua daftari, sio la autography wala nyimbo....!
wewe ni pacha yangu. Furaha yangu mimi ilikuwa tu niwe top ten nipate trip za waliofaulu.
 
Mwenzangu,
Je unakumbuka wakati tunamaliza secondary iwe O level au A level tulikwa
na kitu kinaitwa autograph. Unachukua
daftari jipya unabandika picha za magazeti na kuwapa rafiki zako wakupe
data zao kama vile

Full name

Home Addrress

Best food

Best Actor

Best movie

Best football team

Best player

Best song

Best school

etc etc

Unakumbuka enzi hizo????????

mie mpk leo nina madaftari mawili nlobandika pics na watu wakatoa adress zao...huwa natunza nije kuwaonyesha watoto wangu na vijukuu hahha ulikuwa ulimwengu wa analogy
 
Mi ninachokikumbuka ni kuwa enzi hzo hakuna cha Tigo pesa,mpesa na transaction za hvyo. Tulitumia sana TMO,AIRFORM na kufuta stamp kwa mate ili uitumie tena.

Ahahahahahaaaaaaaaaa umenikumbusha mambo yangu.
 
Nakumbuka masurufu kama mkate na orange squash wakati wa kwenda likizo pia kufuta tiketi za basi kwa mafuta ya break na sabuni ili kujipatia nauli kuliko ile halali. Mambo ya autograph nilikuwa naangalia kwa wenzangu tu

Eeh bhana natamani kulia. Lakini bado tulikuwa tunalalama serikali haitujali...RIP JK NYERERE,RIP EM SOKOINE,RIP R KAWAWA.
 
Ni kweli stamp tulifuta kwa dawa ya meno...
Nikweli kipindi hcho ukiwa na email we mjanja.
Vp ukiwa na penpal kutoka mamtoni...?
,hata ukipata rafiki wa mamtoni hata akiwa nursery,we ndo mjanja...
 
§wala la tiketi ukifika form one watu mnaotoka Mkoa / Wilaya moja walioko form za juu lazima wakupe darasa lauchakachuaji nauli ili wote zilingane
la sivyo mtatia kitumbua mchanga.
 
Yaani kuna mdada aliibaga autograph yangu sijamsamehe hadi leo. She is a lecturer if, hadi leo tukikutana namkumbusha nakudai! Mbaya zaidi hakuitunza. Ningekuwa nayo mwenyewe could have been a good memory!
Mdai, utakuta humo kuna rafiki hujawahi kuwasiliana nae years, ukimtumie barua tu tayari mnaanza mawasiliano upya
 
Kuna dogo ni mwanamziki siku hizi yeye alikuwa haendi darasani kazi yake kuandika nyimbo za bob marley. Ila mziki umemuweka mjini na kwa siku yuko kwene kundi la wakongwe wa bongo flava
 
kwa tuliyosoma boys schools ukipata barua ya kutoka kwa dada wa sekondary duh ilikuwa bongo la issue, unakuta barua imepuliziwa fumu na karatasi ina maua maua ndani, halafu imeandikwa kwa utaalam zile art sijui kama siku hizi sipo. Barua inakuja ina umbo la moyo weee
 
Tmo unaenda posta unaambiwa hela Hakuna njoo wiki ijayo na ni elf 20 tu.kulikuwq na reverse call ttcl unapiga home wanalipia kwny bill ni hapo unaumbuka anapokea beki tatu katoka shamba anakataa kuwa hawako tayari kukulipia kuzamia gtaduation za shule za kike kujichanganya na wanandugu na kula ubwabwa pilau na keki za dezo kusubiri barua ijumaa ukipata iliyotoka ulaya unaishika kama tai watu waone imetoka USA ulikuwa ujiiikooo kutembea na walkman hadi class unsikiliza nyimbo za vanila ice ice ice babby
 
Mwenzangu,
Je unakumbuka wakati tunamaliza secondary iwe O level au A level tulikwa na kitu kinaitwa autograph. Unachukua daftari jipya unabandika picha za magazeti na kuwapa rafiki zako wakupe data zao kama vile

Full name

Home Addrress

Best food

Best Actor

Best movie

Best football team

Best player

Best song

Best school

etc etc

Unakumbuka enzi hizo????????

Natumia nafasi hii kuwaomba radhi mabinti wote walikuwa wanasoma shule ya sekondari Rubale 1991-94 ambao Autograph zao ziliibiwa. Mwizi wa 'phonebooks' zao nilikuwa mimi pamoja na kijana mwingine.

Wivu tu wa kukosa demu ndio ulionitutuma kufanya hivyo!.
Nashukuru kwa kunisamehe.

Ndebile,
P. O. BOX Private Bag, Mwashilalage- Kwimba,
Mwanza.
 
Natumia nafasi hii kuwaomba radhi mabinti wote walikuwa wanasoma shule ya sekondari Rubale 1991-94 ambao Autograph zao ziliibiwa. Mwizi wa 'phonebooks' zao nilikuwa mimi pamoja na kijana mwingine.

Wivu tu wa kukosa demu ndio ulionitutuma kufanya hivyo!.
Nashukuru kwa kunisamehe.

Ndebile,
P. O. BOX Private Bag, Mwashilalage- Kwimba,
Mwanza.

Ha ha ha ha nafikiri watakuseme maana sasa wameshakuwa watu wazima na wanaelewa vizuri maana na akili ya kijana kwa wakati ule ilikuwaje
 
nakumbuka nilikuwa na daftari kubwa limejaa nyimbo za kizungu jioni baada ya msosi 2naanza kuimba! i mic it.
 
Back
Top Bottom