bornagain
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 3,383
- 1,354
Jamani mimi ni kijana wa kiume nimeoa miezi mitatu iliyopita, naomben wadau mnisaidie kina jambo linanitatiza. Mimi kwetu ni Dar es Salaam na wazazi wangu wanakaa Dar es Salaam. Lakini mke wangu yeye kwao ni mkoani na wazazi wake wanaishi huko mkoani. Swali langu ni hili, hivi naweza kwenda nyumbani kuwasalimia wazazi wangu bila kuwa na mke wangu mfano nimetoka kazini halafu nikapitia nyumbani then nikamwambia mke wangu kuwa nimepitia kwetu, hiyo itakua mbaya au inatakiwa kila nikienda nyumbani niwe na mke wangu au nimfahamishe mapema kabla ya safari? Naombeni ushauri wenu na namna ya kuhandle hili suala maana mimi bado mchanga kwenye ndoa.