Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,621
- 3,514
Kwa wadada wenzangu....wanasema experience is the best teacher....leo tu share experience na tupeane ushauri......
Wengi wetu tutakuwa tumekutana na wanaume ambao mimi ninawaita wanaume malengo ya mbele na wanaume waharakisha mambo na wanaume maneno.....
Mwanaume ya malengo mbele ni Yule ambaye kupitia maneno yake anakujengea picha ya baadaye ili apate mahitaji yake ya sasa.Yeye anakujengea picha ya nyie mkiwa na familia yenu,watoto,ndoa nzuri,mkienda matembezi pamoja mwisho wa mwaka nk....hii yote ni ili kukujengea picha kuwa wewe ni sehemu ya maisha yake na kwamba kila analoliwaza analiwaza kulifanya akiwa na wewe siku za mbeleni.
Kwa furaha wanawake walio wengi huwapokea wanaume wa aina hii kwa mikono miwili na wengine wetu huenda hata kutoa sadaka maombi yetu yamejibiwa na kuanza kuwaweka maanani aina hii ya wanaume......
Wanaume waharakisha mambo ni wale ambao wana haraka sana utafikiri wanakimbizwa na moto...hawa ni wale unakutana nae na mara moja anahakikisha umekuwa nae karibu sana kwa wakati mfupi....anahakikisha huoni wala huzifahamu tabia zake chafu.hawa tofauti na wanaume malengo mbele,kwa muda mfupi sana wanahakikisha umewaweka kwenye akili yako,kila saa wanapiga simu,wanaandika message,wanataka kuwa pamoja nawe kila saa,wanakutambulisha kwa ndugu wale kama binamu,mpwa na si wazazi na marafiki zao,wanakupa funguo za nyumba zao na ujanja mwingine wa aina hiyo.
Hawa wanajenga hisia za msichana kwao haraka na wanataka muwe na uhusiano wa kimapenzi haraka.....
Kwa akilo ya kawaida utajiona hakuna kama wewe hapa duniani na una bahati sana,ila baada ya muda mfupi sana watakuliza vibaya walio wengi.
Wanaume maneno.....hawa ni wanaume wazuri sana kwenye kusema...yaani anaweza kuahidi kila awezacho na atakujengea mazingira ya kuamini anaweza kufanya hivyo....ila hawatekelezi na hawana uwezo huo wa kufanya hivyo ,na wengine hata kama wanao uwezo hawafikirii ndani ya roho zao kufanya hivyo,wanaahidi wapate wakitakacho........
Ushauri wangu sasa:
1.Wasichana tuwe makini na tuchukue muda kuwafahamu wanaume wanaokuja kutaka mahusiano na sisi....haraka haraka haina baraka.....mtu hata jina lako la pili halijui anakuahidi ndoa sijui nini....tuweni makini....there is no fire,you do not have to rush kutoa akili.moyo na mwili wako kwa mwanaume usiyemfahamu vizuri. Kile kipindi cha dating tukitumia vizuri kuwasoma na kuwafahamu wanaume...na si wakati wa dating umeshatoa mwili na akili yako na hata moyo wako.....open your ears and eyes and intelligency 100% and not your legs.
2.Tuache tabia ya kuamini ovyo,mtu anakuahidi hiki hafanyi,kile hafanyi....he does not keep promises....wewe nawe umo tu unaendelea nae ukiamini atabadilika au amesahau au unaogopa kumuuliza.....mtu anayekupenda atatenda lile alisemalo kwa wakati,na kama atashindwa utakuwa wa kwanza kujua sababu na zitaeleweka......tuwe wakali kidogo na tuhoji....unamuogopa oh,nikimuuliza ataniacha,kama ni wakukuacha atakuacha tu.
3.Tukubali kuwa tumedanganywa na tuwe wajasiri wa kusonga mbele.Mara kibao unasikia msichana anasema najua ananidanganya ila sasa nifanyeje ndo nimeshalala nae,nimezaa nae,siwezi muacha,tutabanana hapo hapo hadi anioe.....we si wa kwanza kudanganywa,kaa chini lia kama inakubidi,fikiria ulivyodanganywa na ukadanganyika na jifunze then tulia kwa muda na chukua uamuzi wa kuondoka kwenye utumwa wa kosa la kudanganyika then songa mbele kwa kujiamini,kuwa makini na kumuomba Mungu kwa sana.
Ni hayo tu,.....nawapenda wote na nawatakia wikiendi njema.
Wengi wetu tutakuwa tumekutana na wanaume ambao mimi ninawaita wanaume malengo ya mbele na wanaume waharakisha mambo na wanaume maneno.....
Mwanaume ya malengo mbele ni Yule ambaye kupitia maneno yake anakujengea picha ya baadaye ili apate mahitaji yake ya sasa.Yeye anakujengea picha ya nyie mkiwa na familia yenu,watoto,ndoa nzuri,mkienda matembezi pamoja mwisho wa mwaka nk....hii yote ni ili kukujengea picha kuwa wewe ni sehemu ya maisha yake na kwamba kila analoliwaza analiwaza kulifanya akiwa na wewe siku za mbeleni.
Kwa furaha wanawake walio wengi huwapokea wanaume wa aina hii kwa mikono miwili na wengine wetu huenda hata kutoa sadaka maombi yetu yamejibiwa na kuanza kuwaweka maanani aina hii ya wanaume......
Wanaume waharakisha mambo ni wale ambao wana haraka sana utafikiri wanakimbizwa na moto...hawa ni wale unakutana nae na mara moja anahakikisha umekuwa nae karibu sana kwa wakati mfupi....anahakikisha huoni wala huzifahamu tabia zake chafu.hawa tofauti na wanaume malengo mbele,kwa muda mfupi sana wanahakikisha umewaweka kwenye akili yako,kila saa wanapiga simu,wanaandika message,wanataka kuwa pamoja nawe kila saa,wanakutambulisha kwa ndugu wale kama binamu,mpwa na si wazazi na marafiki zao,wanakupa funguo za nyumba zao na ujanja mwingine wa aina hiyo.
Hawa wanajenga hisia za msichana kwao haraka na wanataka muwe na uhusiano wa kimapenzi haraka.....
Kwa akilo ya kawaida utajiona hakuna kama wewe hapa duniani na una bahati sana,ila baada ya muda mfupi sana watakuliza vibaya walio wengi.
Wanaume maneno.....hawa ni wanaume wazuri sana kwenye kusema...yaani anaweza kuahidi kila awezacho na atakujengea mazingira ya kuamini anaweza kufanya hivyo....ila hawatekelezi na hawana uwezo huo wa kufanya hivyo ,na wengine hata kama wanao uwezo hawafikirii ndani ya roho zao kufanya hivyo,wanaahidi wapate wakitakacho........
Ushauri wangu sasa:
1.Wasichana tuwe makini na tuchukue muda kuwafahamu wanaume wanaokuja kutaka mahusiano na sisi....haraka haraka haina baraka.....mtu hata jina lako la pili halijui anakuahidi ndoa sijui nini....tuweni makini....there is no fire,you do not have to rush kutoa akili.moyo na mwili wako kwa mwanaume usiyemfahamu vizuri. Kile kipindi cha dating tukitumia vizuri kuwasoma na kuwafahamu wanaume...na si wakati wa dating umeshatoa mwili na akili yako na hata moyo wako.....open your ears and eyes and intelligency 100% and not your legs.
2.Tuache tabia ya kuamini ovyo,mtu anakuahidi hiki hafanyi,kile hafanyi....he does not keep promises....wewe nawe umo tu unaendelea nae ukiamini atabadilika au amesahau au unaogopa kumuuliza.....mtu anayekupenda atatenda lile alisemalo kwa wakati,na kama atashindwa utakuwa wa kwanza kujua sababu na zitaeleweka......tuwe wakali kidogo na tuhoji....unamuogopa oh,nikimuuliza ataniacha,kama ni wakukuacha atakuacha tu.
3.Tukubali kuwa tumedanganywa na tuwe wajasiri wa kusonga mbele.Mara kibao unasikia msichana anasema najua ananidanganya ila sasa nifanyeje ndo nimeshalala nae,nimezaa nae,siwezi muacha,tutabanana hapo hapo hadi anioe.....we si wa kwanza kudanganywa,kaa chini lia kama inakubidi,fikiria ulivyodanganywa na ukadanganyika na jifunze then tulia kwa muda na chukua uamuzi wa kuondoka kwenye utumwa wa kosa la kudanganyika then songa mbele kwa kujiamini,kuwa makini na kumuomba Mungu kwa sana.
Ni hayo tu,.....nawapenda wote na nawatakia wikiendi njema.